WANAFUNZI 65 KUONDOKA KWA MASOMO NCHINI CHINA – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home ELIMU

WANAFUNZI 65 KUONDOKA KWA MASOMO NCHINI CHINA

I am Magnifico by I am Magnifico
Oct 26, 2015
in ELIMU
0 0
0
WANAFUNZI 65 KUONDOKA KWA MASOMO NCHINI CHINA
0
SHARES
32
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT


Mkurugenzi Mtendaji wa Global Link Education (GEL), Abdulmaalik Mollel akizungumza na wazazi na wanafunzi wanaotarajia kuondoka Oktoba 28, 2015 kwenda kusoma masomo ya elimu ya juu wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam. 
Wazazi wakimsikiliza Abdulmaalik Mollel wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wazazi na wanafunzi  wanaokwenda nchini China kwa masomo ya elimu ya juu wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Global Link Education (GEL), Abdulmaalik Mollel (hayupo pichani) wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Global Link Education (GEL), Abdulmaalik Mollel akitoa nyaraka za taarifa za wanafunzi wanaokwenda nchini China wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam.
 Wanafunzi wakiuliza swali kwa masomo wanayokwenda kusoma katika vyuo vya nje wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Global Link Education (GEL), Abdulmaalik Mollel akizungumza na mzazi wa mwanafunzi wa anyekwenda kusoma nchini China wakati wa semina elekezi ya kuwajengea uwezo iliyofanyika makao Makuu ya GEL jijini Dar es Salaam. Picha na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

KAMPUNI ya Global Link Education imeendelea kupeleka wanafunzi kwenda kusoma vyuo vya nje vilivyo na uwezo kutoa elimu bora.

Hayo ameyasema Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Link Education (GEL), Abdumaalik Mollel wakati akitoa mafunzo kwa wanafunzi 65 wanaokwenda nchini China kwa masomo ya elimu ya juu.

Mollel amesema vyuo vya nje ambavyo vinashirikiana na GEL vina ubora wa elimu pamoja na kuwa na vitendea kazi vinavyoweza kufanya mwanafunzi afanye vizuri katika masomo yao.

Amesema wanafunzi 500, GEL imesha wadahili katika vyuo vya nje na wanafunzi hao wameona ubora wa vyuo hivyo na kuweza kuleta chachu ya maendeleo nchini kutokana na utaalam wataopata huko.

Mollel amesema kuwa nafasi bado zipo katika vyuo vya China hivyo wazazi wanaweza kuwasiliana na GEL kufanya usajili katika vyuo hivyo.

“Nia ya GEL ni kuona wanafunzi wanafanya vizuri katika matokea na tunafatilia tabia zao hatua kwa hatua tukiwa na lengo ya kupata wasomi wenye ujuzi kwa maendeleo ya taifa”amesema Mollel.

Aidha amesema kuwa wanafunzi wanaonyesha tabia mbaya wanawarudisha nchini katika kuweza kuokoa fedha za mzazi kuendelea kuhudumia mtoto ambaye mwishoni hatafanya vizuri.

ADVERTISEMENT
I am Magnifico

I am Magnifico

Related Posts

Wanafunzi Waliofadhiliwa Shule Binafsi Kuanza Kupewa Mkopo Vyuoni
BODI YA MIKOPO

Wanafunzi Waliofadhiliwa Shule Binafsi Kuanza Kupewa Mkopo Vyuoni

by I am Magnifico
Sep 23, 2019
0

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof....

Read more
Walimu 16 Wakamatwa Kwa Kuruhusu Mwanafunzi Feki Afanye Mtihani

Walimu 16 Wakamatwa Kwa Kuruhusu Mwanafunzi Feki Afanye Mtihani

Sep 13, 2019
Chuo Kikuu UDSM Chakanusha Matokeo Mabaya Kwa Wanafunzi Wake

Chuo Kikuu UDSM Chakanusha Matokeo Mabaya Kwa Wanafunzi Wake

Aug 29, 2019
SERIKALI YAWAPIGA MARUFUKU WALIMU KUINGIA DARASANI NA VIBOKO

SERIKALI YAWAPIGA MARUFUKU WALIMU KUINGIA DARASANI NA VIBOKO

Aug 1, 2019
VYUO VILIVYOKUWA VIMEFUNGIWA KUDAHILI VYAPEWA RUHUSA YA KUDAHILI

VYUO VILIVYOKUWA VIMEFUNGIWA KUDAHILI VYAPEWA RUHUSA YA KUDAHILI

Jul 16, 2019

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA: Je adhabu ya kiboko shuleni iondolewe? Waziri azungumza

Jun 20, 2019
Next Post
MAADHIMISHO YA SIKU YA TAKWIMU DUNIANI YAFANA

MAADHIMISHO YA SIKU YA TAKWIMU DUNIANI YAFANA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

October 2015
M T W T F S S
« Sep   Nov »
 1234
567891011
12131415161718
19202122232425
262728293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In