TAKUKURU YAKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI ZENYE TUHUMA DHIDI YA MAAFISA WAKE – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI TANZANIA

TAKUKURU YAKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI ZENYE TUHUMA DHIDI YA MAAFISA WAKE

I am Magnifico by I am Magnifico
Jun 18, 2019
in HABARI TANZANIA
0 0
0
0
SHARES
45
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imekanusha taarifa za upotoshaji zilizochapishwa katika magazeti mawili ya jana Juni 17, 2019. 
Taarifa hizo zilizochapwa katika gazeti la FAHARI YETU toleo Na 163 la Jumatatu Juni 17, 2019 ukurasa wa kwanza ikiwa na kichwa cha habari VIRUSI WA RUSHWA NDANI YA TAKUKURU HAWA HAPA’ pamoja na Gazeti la TANZANITE Toleo Naa 478 la Jumatatu Juni 17, 2019 ukurasa wa kwanza ikiwa na kichwa cha habari MTANDAO HATARI WA RUSHWA NDANI YA TAKUKURU WABAINIKA’. 
TAKUKURU wameufahamisha umma kwamba taarifa hizo ambazo zimeandikwa kwa kufanana katika magazeti yote mawili ni za upotoshaji wenye lengo la kudhoofisha utendaji kazi wa TAKUKURU hasa katika kipindi hiki cha mapambano na wakwepa kodi, wabadhirifu wa mali za umma pamoja na wahujumu wa uchumi. 
Katika taarifa yao kwa umma TAKUKURU wamesema kuwa wanafahamu fika kwamba wapo vitani na kwamba kadri wanavyoongeza kasi ya mapambano ndivyo vivo hivyo ambavyo wala rushwa pamoja na wanaonufaika na vitendo vya rushwa wanaendelea kutafuta mbinu za kudhoofisha mapambano dhidi ya rushwa na kuwakatisha tamaa watumishi wao. 
Walimalizia kwa kusema kuwa wanapenda kuuhakikishia umma kwamba TAKUKURU ipo imara na itaendelea kuwafichua na kuwashughulikia kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nan 11 ya Mwaka 2007, wale wote wanaojihusisha na vitendo vya rushwa bila ya kujali cheo, wadhifa, jinsia wala itikadi. 
Tags: PCCBRUSHWATAKUKURU
ADVERTISEMENT
I am Magnifico

I am Magnifico

Related Posts

Serikali ya umoja wa kitaifa yaridhia kuendeleza aman, umoja na mshikamano
HABARI

Serikali ya umoja wa kitaifa yaridhia kuendeleza aman, umoja na mshikamano

by Ombeni Osward
Jan 21, 2021
0

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza...

Read more
Viongozi wanne kizimbani kuuza aridhi kinyume na sheria

Viongozi wanne kizimbani kuuza aridhi kinyume na sheria

Jan 21, 2021
Zaidi ya Bilioni 800 kutumika ujenzi wa miundombinu ya maji nchini.

Zaidi ya Bilioni 800 kutumika ujenzi wa miundombinu ya maji nchini.

Jan 20, 2021
Bweni lililochomwa moto 2018 laungua tena,kura zapigwa kubaini mhusika

Bweni lililochomwa moto 2018 laungua tena,kura zapigwa kubaini mhusika

Jan 20, 2021
Dkt. Gwajima Akemea vikali Ubadhirifu wa Dawa

Vituo vya afya vyatakiwa kuwa na mkataba wa huduma Kwa wateja

Jan 20, 2021
Nyaraka za Serikali kuandikwa kwa Kiswahili

Nyaraka za Serikali kuandikwa kwa Kiswahili

Jan 20, 2021
Next Post

Sababu za Wema Kupelekwa Segerea

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

June 2019
M T W T F S S
« May   Jul »
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In