Tigo yaunganisha wateja wa Sumbawanga na mtandao wa 4G – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Tigo yaunganisha wateja wa Sumbawanga na mtandao wa 4G

I am Magnifico by I am Magnifico
Jun 12, 2019
in HABARI
0 0
0
0
SHARES
86
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

  Meneja wa Tigo Kanda ya Kusini Ladislaus Karlo (kushoto) akiongea na wananchi wa Sumbawanga wakati wa uzinduzi wa mnara wa 4G mjini Sumbawanga. Wa pili Kulia ni Katibu Tawala wa Manispaa ya Sumbawanga Christina Mzena akifuatiwa na Meneja Mauzo wa Tigo Rukwa Francis Ndada


Katibu Tawala wa Manispaa ya Sumbawanga Christina Mzena (kati kati) akizungumza wakati wa uzinduzi wa mnara wa Tigo 4G wilayani Sumbawanga jana. Kushoto ni Meneja wa Tigo Kanda ya Kusini Ladislaus Karlo na kulia ni Meneja Mauzo wa Tigo Rukwa, Francis Ndada


  Katibu Tawala wa Manispaa ya Sumbawanga Christina Mzena akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mnara wa 4G wilayani humo. Wanaoshangilia ni baadhi ya wafanyakazi wa Tigo waliohudhuria uzinduzi huo jana.


ADVERTISEMENT
Katibu Tawala wa Manispaa ya Sumbawanga Christina Mzena akionyeshwa baadhi ya bidhaa za mawsiliano kama simu zenye uwezo wa G4 muda mfupi kabla ya uzinduzi wa mnara wa 4G uliofanyika jana. Anayemuelekeza ni Meneja Mauzo wa Tigo Rukwa Francis Ndada 

  
Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya Tigo  imezindua mtandao wenye kasi  wa 4G mjini Sumbawanga, utakaowawezesha wateja wake kupata huduma bora ya intanet, kupiga na kupokea simu, pamoja na ujumbe mfupi wa maneno (SMS). 
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mnara wa 4G mjini Sumbawanga, Meneja Tigo wa Kanda ya KusinI Ladislaus Karlo alisema mnara huo ulioongezwa ufanisi kutoka 3G kwenda 4G umeimarishwa ili kuweza kupitisha mfumo wa data kwa haraka zaidi, hivyo kuwezesha miamala ya fedha na huduma ya intanet kuwa ya kasi zaidi.
“Kama mnavyofahamu, Sumbawanga ni makao makuu ya mkoa wa Rukwa, hivyo kupelekea mji huu kuwa kiungo muhimu wa shughuli za kiuchumi…hapa ndipo faida ya mtandao huu wa 4G unapoweza kudhihirika, katika kuwezesha biashara na kurahisisha upatikanaji wa taarifa na habari kwa kasi zaidi,” alisema Karlo wakati wa uzinduzi wa mnara huo mpya wa 4G.
Katika hotuba yake, Karlo alisisitiza pia kwamba wateja wa Tigo sasa wataweza kutumia mtandao ulioimara, usiokuwa na vikwazo, ambao utawawezesha kufanya shughuli zinazotumia kiwango kikubwa cha intanet, kama kutazama video, kusikiliza muziki, na kutuma na kupokea habari mtandaoni bila wasiwasi wowote.
“Wateja wetu wa hapa Sumbawanga ambao watahudumiwa katika eneo la mnara huu wa 4G watapata ofa maalum, watazawadiwa GB 4 za intanet bure pale wanapobadilisha laini zao za simu kuingia 4G. Wateja wataweza kutumia kifurushi hichi cha intanet kwa muda wa siku 7,” alisema Karlo.
Karlo pia aliwakumbusha wateja wa Tigo Sumbawanga kuwa wanaweza wakapata ofa mpya ya ‘Saizi Yako’ ambayo inamwezesha kila mteja kupata ofa bora ya kupiga, kupokea simu, intanet na SMS iliyo mahususi na kuendana na mahitaji yao binafsi. Kujiunga na ofa hiyo, piga *147*00# or *148*00#.”
“Kipaumbele chetu ni kuhakikisha kwamba wateja wetu wanapata huduma za teknolojia za kisasa kama vile mtandao wa 4G. Pia ni muhimu kutambua kwamba, teknolojia ya 4G imeongeza idadi kubwa ya watu kuunganishwa na intanet kupitia simu na pia imefungulia jamii zilizopo vijijini kuweza kupata huduma za kielektroniki katika nyanja za kibiashara, afya, elimu na serikali ambazo walishindwa kupata huko nyuma,” alisema Karlo. 
Mnara wa Sumbawanga ni wa nne kuzinduliwa baada ya uzinduzi wa minara iliyopo Mpanda, Katavi; Kilolo, Iringa na Bariadi. Jumla ya minara 52 itazinduliwa katika kampeni hii ya nchi nzima kwenye maeneo mbali mbali ikiwa ni pamoja na kanda ya Ziwa, Kaskazini, Pwani na Kusini.  

Tags: TIGO
ADVERTISEMENT
I am Magnifico

I am Magnifico

Related Posts

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar
HABARI

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

by Mhariri
Jan 22, 2021
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP...

Read more
Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Jan 22, 2021
Naibu Waziri Kipanga aagiza Vyuo vya VETA kwenye Wilaya 25 vyote vikamilike kwa wakati

Naibu Waziri Kipanga aagiza Vyuo vya VETA kwenye Wilaya 25 vyote vikamilike kwa wakati

Jan 22, 2021
Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato (+video)

Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato (+video)

Jan 22, 2021
Rais wa Zanzibar akutana na IGP Sirro

Rais wa Zanzibar akutana na IGP Sirro

Jan 22, 2021
Waziri Aweso awaagiza SUMAJKT kuongeza nguvu kazi kwenye ujenzi wa tanki la Maji Chamwino

Waziri Aweso awaagiza SUMAJKT kuongeza nguvu kazi kwenye ujenzi wa tanki la Maji Chamwino

Jan 22, 2021
Next Post

Hamisa Mobetto Afungukia Ishu ya Fobby

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

June 2019
M T W T F S S
« May   Jul »
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In