MHASIBU WA JIJI ARUSHA ATUHUMIWA KUTAFUNA MILIONI 85 KILA MWEZI – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home Arusha

MHASIBU WA JIJI ARUSHA ATUHUMIWA KUTAFUNA MILIONI 85 KILA MWEZI

I am Magnifico by I am Magnifico
Jul 22, 2019
in Arusha, HABARI
0 0
0
MHASIBU WA JIJI ARUSHA ATUHUMIWA KUTAFUNA MILIONI 85 KILA MWEZI
0
SHARES
72
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dk Maulid Madeni amemtaka mhasibu wa jiji hilo, Charles Jacob kujisalimisha polisi kwa madai ya kutafuna Sh 85 milioni za makusanyo ya kila mwezi kuanzia Machi, 2019 katika mizani wa mazao ya chakula.
Amesema tangu mizani hiyo ilipoanzishwa Machi, 2019 imekuwa ikiingiza Sh 3.3 milioni kwa mwezi badala ya Sh 88 milioni, kwamba Sh 85 milioni kila mwezi hazijulikani zinapokwenda.
Jacob, msimamizi wa mizani hiyo pamoja na wafanyakazi wake wawili, Thobias Julius na Agness Loishiye wanadaiwa kusababisha upotevu huo wa fedha.
Madeni amewaweka ndani wafanyakazi hao na kuagiza Jacob ambaye hakuwepo kazini kujisalimisha mwenyewe kituo cha polisi kati Mkoa wa Arusha.
Akizungumza leo Jumamosi Julai 20, 2019 Dk Madeni amesema kituo hicho cha kukusanya ushuru hakifanyi vyema na kusababisha fedha nyingi kuishia mikononi mwa wakusanyaji na mhasibu huyo.
“Nilifuatilia muda mrefu ukusanyaji wa mapato nikagundua kuna ulaji mkubwa wa fedha unaofanywa na mhasibu huyo ndio maana leo hajaja hapa.”
“Anaelewa mchezo anaoufanya na wafanyakazi wake nitahakikisha nawaweka ndani wote wanaojaribu kucheza na fedha ya Serikali sitamwonea mtu yeyote huruma,” amesema Dk Madeni
Amebainisha kuwa kuna wafanyakazi wachache wanaiibia Serikali mapato, kuahidi kupambana nao.
Awali, wafanyakazi hao walipewa nafasi ya kujitetea na kubainisha kuwa wameshindwa kukusanya mapato kutokana na magari kuwa machache, hawafahamu kama fedha wanayokusanya kama inafika au haifiki katika halmashauri.
Mchumi wa Jiji la Arusha, Anna Mwambene amesema wamekuwa wakifuatilia vyanzo vya mapato mbalimbali kuangalia utendaji wa kazi, kubaini upotevu wa fedha unaofanywa na watendaji wasio waaminifu.
ADVERTISEMENT
I am Magnifico

I am Magnifico

Related Posts

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu
HABARI

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu

by I am Krantz
Jan 15, 2021
0

 Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Angelina Nkwingwa...

Read more
RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

Jan 15, 2021
Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Jan 15, 2021
NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

Jan 15, 2021
Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Jan 15, 2021
Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Jan 15, 2021
Next Post
Msanii Q.Chief Apewa Gari na Harmonize

Msanii Q.Chief Apewa Gari na Harmonize

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

July 2019
M T W T F S S
« Jun   Aug »
1234567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In