Hakuna Mtanzania atakayekosa kitambulisho cha taifa – Waziri Mkuu – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Hakuna Mtanzania atakayekosa kitambulisho cha taifa – Waziri Mkuu

Mhariri by Mhariri
Feb 21, 2020
in HABARI
0 0
0
Hakuna Mtanzania atakayekosa kitambulisho cha taifa – Waziri Mkuu
0
SHARES
76
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kila raia wa Tanzania aliyeomba kitambulisho cha Taifa atakipata, hivyo amewataka waombaji ambao bado hawajapata waendelee kuwa na subira.

Amesema waombaji hao watapatiwa vitambulisho hivyo baada ya wahusika kupitia maombi yao na kujiridhisha kwamba wote ni raia wa Tanzania na Serikali inafanya hivyo ili kulinda usalama wa nchi.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Februari 21, 2020) wakati akizungumza katika Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Kigoma. Waziri Mkuu ni mlezi wa CCM wa mkoa wa Kigoma.

ADVERTISEMENT

“Watu wote wanaotaka kuingia nchini ni lazima wafuate taratibu zilizowekwa pia Uhamiaji na vyombo vingine vya dola vijiridhishe kwamba hata hao wanaopitia njia sahihi kama kweli ni watu wema.”

Waziri Mkuu amesema katika mikoa ya mipakani ina tatizo la watu kuingia bila ya kufuata taratibu, hivyo kabla ya kutoa kitambulisho ni lazima Serikali ijiridhishe kama kweli aliyeomba ni raia. “Pale wahusika watakapohitaji kujiridhisha waombaji watoe ushirikiano.”

Waziri Mkuu amesema lazima zoezi hilo lifanyike vizuri na wataharakisha ili wananchi waweze kupata vitambulisho. Tayari Serikali imeshaongeza vifaa na watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Akizungumzia kuhusu taarifa baadhi ya wananchi wakuombwa rushwa ili waweze kupata vitambulisho, Waziri Mkuu amewataka watu wote walioombwa rushwa wakaripoti katika vyombo vya sheria. Amesema marufuku mtu kuomba wala kupokea rushwa.

Waziri Mkuu amesema kuwa suala la kuimarisha ulinzi na usalama katika mikoa ya mipakani ukiwemo na mkoa wa Kigoma ni jambo muhimu kwa sababu bila ya kuimarisha ulinzi mikoa hiyo haitakweza kupata maendeleo. Amevipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka viongozi na wanachama wa CCM washirikiane na wabunge na madiwani waliopo sasa na wasiwavuruge wawaache watekeleze majukumu yao hadi pale muda wao utakapomalizika.

Pia, Waziri Mkuu amewataka viongozi na wanachama wa CCM wajiepushe na suala la ukabila na udini katika kuteua mtu wa kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho na badala yake wateue mtu ambaye anauzika ndani na nje ya chama.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi
HABARI

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi

by Mhariri
Jan 22, 2021
0

Na Amiri Kilagalila,Njombe Jeshi la Polisi mkoani...

Read more
Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Jan 22, 2021
Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Jan 22, 2021
Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Jan 22, 2021
IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

Jan 22, 2021
Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Jan 22, 2021
Next Post
Balozi wa China Afrika Kusini asema Marekani haiwezi kupambana na virusi vya korona kama China

Balozi wa China Afrika Kusini asema Marekani haiwezi kupambana na virusi vya korona kama China

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

February 2020
M T W T F S S
« Jan   Mar »
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
242526272829  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In