RAS Simiyu ataka majengo ya upasuaji, wodi ya wazazi Hospitali ya wilaya Busega yakamilishwe – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

RAS Simiyu ataka majengo ya upasuaji, wodi ya wazazi Hospitali ya wilaya Busega yakamilishwe

Mhariri by Mhariri
Sep 10, 2020
in HABARI, HABARI TANZANIA
0 0
0
RAS Simiyu ataka majengo ya upasuaji, wodi ya wazazi Hospitali ya wilaya Busega yakamilishwe
0
SHARES
36
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa majengo ya upasuaji na wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ili kuboresha hali ya utoaji wa huduma kwa wananchi katika hospitali hiyo.

Mmbaga ametoa agizo hilo Septemba 09, 2020 wakati zoezi la usimamizi shirikishi alipotembelea hospitali hiyo kukagua maendeleo ya ujenzi wa majengo hayo ambayo yanapaswa kukamilika na kuanza kutoa huduma ifikapo Septemba 30, 2020.

“Nampongeza Mkurugenzi kwa kujiongeza, badala ya kusubiri kibali kutoka HAZINA kulipa fedha za kukamilisha ujenzi wa majengo haya, amejiwekea utaratibu wa kuwalipa mafundi wetu, nimeelekeza kuwa aongeze kiwango anachotoa kwa kila juma ili kuongeza kasi ya ujenzi na hatimaye majengo haya yaweze kukamilika na kutumika kwa huduma kusudiwa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga ameongeza kuwa ukamilishaji wa majengo hayo uende sambamba na utunzaji wa mazingira ambao utajumuisha upandaji miti, bustani za maua na utunzaji wa miti asili huku akitoa pongezi kwa Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri hya Wilaya ya Busega kwa usimamizi mzuri katika ujenzi wa hospitali hiyo na kumuagiza Mkurugenzi kumthibitisha katika cheo chake.

Wakati huo huo Mmbaga ameelekeza Timu ya usimamizi wa afya ngazi ya wilaya (CHMT) kuimarisha usimamizi katika mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) uliboreshwa hususani watoa huduma ngazi ya jamii wanaohusika katika usajili ili wananchi waweze kupata huduma zilizokusudiwa na serikali.

ADVERTISEMENT

Katika hatua nyingine Mmbaga ametembelea kikundi kinachojihusisha kilimo cha umwagiliagi kilichopo kijiji cha Chamgasa na kuelekeza wataalam wa fedha na uchumi waweze kutoa elimu kwa wakulima hao juu ya utunzaji na matumizi ya fedha ili wanapopewa mikopo na wadau waweze kutekeleza miradi ambayo itakuwa endelevu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya amesema atahakikisha fedha zinatolewa kwa wakati kwa mafundi wanaoendelea na ujenzi wa majengo ya Upasuaji na wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ili shughuli za ujenzi zisikwame.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba ameipongeza Timu ya usimamizi wa afya ngazi ya wilaya (CHMT) kwa namna inavyotekeleza majukumu yake huku akisisitiza watumishi wote wa afya kuendelea kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

Nao baadhi ya watumishi wa afya katika kituo cha afya Lukungu wameomba miundombinu katika vituo vya kutolea huduma za afya iboreshwe ili kutoa huduma kulingana na hadhi za vituo hivyo na wananchi wapate huduma wanazotarajia kuzipata katika vituo husika.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi
HABARI

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi

by Mhariri
Jan 22, 2021
0

Na Amiri Kilagalila,Njombe Jeshi la Polisi mkoani...

Read more
Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Jan 22, 2021
Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Jan 22, 2021
Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Jan 22, 2021
IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

Jan 22, 2021
Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Jan 22, 2021
Next Post
VIGOGO CCM WALIVYOBANA BILA KONA; MAGAZETINI LEO IJUMAA TAREHE 11 SEPTEMBA

VIGOGO CCM WALIVYOBANA BILA KONA; MAGAZETINI LEO IJUMAA TAREHE 11 SEPTEMBA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

September 2020
M T W T F S S
« Aug   Oct »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
282930  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In