Mashindano ya mbio za mitumbwi (Tanzania Boat Race) kufanyika Mwanza – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Mashindano ya mbio za mitumbwi (Tanzania Boat Race) kufanyika Mwanza

I am Krantz by I am Krantz
Nov 25, 2020
in HABARI
0 0
0
Mashindano ya mbio za mitumbwi (Tanzania Boat Race) kufanyika Mwanza
0
SHARES
73
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter


Mratibu wa mashindano ya mitumbwi Kasile Kasile,akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Mwanza kuhusu mashindano hayo yatakayofanyika jijini humo,kushoto ni Meneja Mauzo wa kampuni ya Bia(TBL) mkoa wa Mwanza lssa Makani na Meneja Mkuu wa The Scope Experience Herbert Rweikiza.


Meneja Mkuu wa The Scope Experience Herbert Rweikiza, akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza kuhusu mashindano ya mitumbwi yatakayofanyika jijini humo,kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha Wapiga Makasia jijini Mwanza Manzese Nkunzu na Meneja Mauzo wa kampuni ya Bia (TBL) mkoa wa Mwanza lssa Makani.

Mashindano maarufu ya mbio za mitumbwi (Tanzania Boat Race) yanayoandaliwa na kampuni ya The Scope yatafanyika Desemba 13 mwaka huu, mkoani Mwanza na yanatarajiwa kujumuisha zaidi ya timu 40 za wavuvi mkoani hapa na kutoka Wilaya za Ilemela, Nyamagana, Ukerewe, Buchosa, Sengerema na visiwa vilivyopo kwenye Ziwa Victoria jirani na mkoa wa Mwanza.

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mashindano haya msimu wa mwaka 2020, Meneja wa The Scope, Herbert Rweikiza, alisema Mashindano haya yataweza kufanyika kutokana na jitihada za wadau mbalimbali ambao ni Chama Cha Wapiga Makasia (Mwanza), Ofisi ya Afisa Utamaduni (Jiji la Mwanza), Umoja wa Wafanyabiashara wa Soko la Mwaloni na kampuni ya TBL kupitia kinywaji cha Balimi Extra Lager.

“Mashindano haya adimu yatakuwa endelevu na kufanyika kila mwaka, mwaka huu  yatafanyika mkoani Mwanza na mwakani yatajumuisha mikoa yote ya kanda ya ziwa ambayo ni Mwanza, Mara, Simiyu, Geita, Kagera na Kigoma kwa upande wa ziwa Tanganyika na tunatarajia kuyaboresha zaidi mwaka hadi mwaka ili yawe na mvuto zaidi na kushirikisha washindani wengi na wadau mbalimbali”, alisema Rweikiza.

ADVERTISEMENT

Aidha Rweikiza alisema mashindano haya mbali na kulenga kutoa burudani kwa wananchi na kunufaisha washiriki watakaojishindia zawadi pia yanalenga kukuza utalii, kutangaza utamaduni wa kitanzania na kutafanyika uhamasishaji wa tabia za afya zinazopewa kipaumbele katika makundi ya wavuvi na jamii inayowazunguka, ili kuepukana na maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI, Ugonjwa hatari wa Malaria, mimba zisiso tarajiwa, nk. hususani kwa vijana ambao wako katika hatari zaidi.

Sambamba na hayo, kutakuwa na promosheni za kinywaji cha Balimi Extra Lager katika maeneo mbali mbali.

Aliwataka wavuvi wengi wanaotaka kushiriki kuendelea kujiandikisha kushiriki kuanzia leo kupitia vituo 10 vya uandikishaji vilivyotengwa katika maeneo mbalimbali,  Vilevile aliwataka wakazi wa jiji la Mwanza kujitokeza kwa wingi katika siku ya mashindano.

Naye  Meneja Mauzo wa kampuni ya bia Tanzania (TBL) kanda ya Mwanza,Issa Makani,amesema kampuni imejitokeza kudhamini mashindano hayo mwaka huu kupitia kinywaji cha bia ya Balimi kwa kuwa imekuwa ikiyadhamini kwa zaidi ya miaka 10 na itandelea kuyadhamini kutokana na kuendelea kupata umaarufu mkubwa na  kuleta burudani  kwa wananchi sambamba na kuwaongeza kipato washiriki.

 

 

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu
HABARI

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu

by I am Krantz
Jan 15, 2021
0

 Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Angelina Nkwingwa...

Read more
RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

Jan 15, 2021
Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Jan 15, 2021
NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

Jan 15, 2021
Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Jan 15, 2021
Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Jan 15, 2021
Next Post
BENKI YA NMB YASAPOTI TAMASHA LA SIKU YA MLIPA KODI MANISPAA YA ILALA

BENKI YA NMB YASAPOTI TAMASHA LA SIKU YA MLIPA KODI MANISPAA YA ILALA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

November 2020
M T W T F S S
« Oct   Dec »
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
30  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In