Sasa waweza kununua tiketi za michezo kidigitali na Tigo Pesa – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home BIASHARA

Sasa waweza kununua tiketi za michezo kidigitali na Tigo Pesa

I am Krantz by I am Krantz
Nov 3, 2020
in BIASHARA
0 0
0
Sasa waweza kununua tiketi za michezo kidigitali na Tigo Pesa
0
SHARES
95
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

Kaimu  Afisa Mkuu wa Tigo Pesa, Angelica Peter, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi mfumo kwa ajili ya kuwarahisishia mashabiki wa soka kununua tiketi kwa njia ya Tigo Pesa katika michezo mbalimbali itakayochezwa Uwanja wa Uhuru na Mkapa, Dar es Salaam.

 

Shukrani: “Natoa shukrani kwa @tigo_tanzania na NIDC kwa hatua ambayo wamechukua ili kumruhusu mtanzania na mwanamichezo awe na urahisi kuweza kuingia uwanjani kupata burudani.” Yusuph Singo-Mkurugenzi wa Michezo Tanzania.
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Kimtandao (NIDC), zimeungana kwa ajili ya kuwarahisishia mashabiki wa soka kununua tiketi kwa njia ya Tigo Pesa katika michezo mbalimbali itakayochezwa Uwanja wa Uhuru na Mkapa, Dar es Salaam.
Mashabiki wa soka wataanza kunufaika na huduma hiyo ya kisasa ili kuhakikisha wanapunguza msongamano wakati wa kukata tiketi kwa ajili ya kwenda kuangalia mechi za soka kwenye viwanja hivyo.
Akizungumza Dar es Salaam, Kaimu  Afisa Mkuu wa Tigo Pesa, Angelica Peter, alisema kuwa wameungana na NIDC kwa ajili ya kuwasaidia mashabiki wa soka kukata tiketi kwa njia ya mtandao.
Alisema kuwa mashabiki wa soka kwa sasa watakuwa wamepunguza suala la kutembea na fedha taslimu na badala yake wataanza kutumia huduma ya kukata tiketi kwa njia ya Tigo Pesa.
“Wateja wetu kwa sasa hawatapata tabu tena au kuhangaika kufanya malipo ya tiketi za michezo, kwani kupitia Tigo Pesa wanaweza kufanya malipo ya tiketi kidijitali kupitia kadi maalumu kutoka kwa washirika wetu kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Kimtandao cha (NIDC).
“Tanzania ni moja ya nchi za kuigwa katika kufanya malipo kidijitali au kielektroniki. Kupitia malipo haya ya N-Card tumeendelea kupeperusha bendera katika nyanja ya malipo ya kidijitali,” alisema.
Afisa Uhusiano wa Kituo cha NIDC, Geophrey Mlelwa, alisema kuwa wamefurahia kuungana na Tigo kwa ajili ya kuleta mapinduzi kwenye michezo.
Alisema kuwa mashabiki wa soka watapata fursa ya kukata tiketi za kuangalia mechi mbalimbali bila tatizo lolote kuanzia sasa.
“Hii ni fursa kwa wapenzi wa michezo hasa mpira wa miguu kuweza kununua tiketi kirahisi na kwa haraka bila bugdha yoyote kupitia kadi hii maalum(N-card) ambapo watafanya malipo kupitia Tigo Pesa.” alisema Mlelwa.
Mkurugenzi wa Fedha wa  Yanga, Mfikirwa Hajji, alisema kuwa mashabiki wa Yanga watumie fursa hiyo hasa katika mechi yao dhidi ya Simba itakayochezwa Jumamosi.
Alisema mechi hiyo hukusanya mashabiki wengi zaidi na kwamba amewataka kununua tiketi zao mapema kwa ajili ya kuahudia mchezo huo.
“Hii ni fursa ya aina yake na kwamba tunawaomba mashabiki wetu waitumie kila wakati kwa kuanzia katika mechi yetu dhidi ya Simba itakayofanyika Jumamosi,” alisema.
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

NMB yazindua Bima ya simu za mkononi
BIASHARA

NMB yazindua Bima ya simu za mkononi

by I am Krantz
Apr 19, 2021
0

 Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi(kulia) na...

Read more
Tigo yaungana na TAPSOA kuwezesha wateja kufanya malipo ya mafuta kwa Tigo Pesa

Tigo yaungana na TAPSOA kuwezesha wateja kufanya malipo ya mafuta kwa Tigo Pesa

Apr 16, 2021
Mawakala wa Tigo Pesa washinda mamilioni

Mawakala wa Tigo Pesa washinda mamilioni

Apr 15, 2021
Zantel yazindua ofa ya mfungo wa Ramadhan

Zantel yazindua ofa ya mfungo wa Ramadhan

Apr 15, 2021
Vodacom yashirikiana na Britam Tanzania kuzindua VodaBima kupitia M-Pesa

Vodacom yashirikiana na Britam Tanzania kuzindua VodaBima kupitia M-Pesa

Apr 13, 2021
Bolt yazindua Web App kupanua huduma za usafiri Tanzania

Bolt yapokea uwekezaji wa Euro 20 milioni kutoka IFC

Apr 11, 2021
Next Post
Video: Polisi Singida wakamata wafuasi 20 wa CHADEMA kwa kuandamana

Video: Polisi Singida wakamata wafuasi 20 wa CHADEMA kwa kuandamana

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

November 2020
M T W T F S S
« Oct   Dec »
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
30  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In