SIDO YAZITAKA HALMASHAURI KUSHIRIKIANA NA CAMFED KUWAWEZESHA WASICHANA – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

SIDO YAZITAKA HALMASHAURI KUSHIRIKIANA NA CAMFED KUWAWEZESHA WASICHANA

I am Krantz by I am Krantz
Nov 27, 2020
in HABARI
0 0
0
SIDO YAZITAKA HALMASHAURI KUSHIRIKIANA NA CAMFED KUWAWEZESHA WASICHANA
0
SHARES
40
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Mgeni rasmi kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, Meneja Mafunzo wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo nchini Tanzania (SIDO), Bw. Stephen Bando (kulia) aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa SIDO akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Ukumbi wa Msimbazi Center jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura akifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.



Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura (kushoto) akipokea zawadi ya moja ya bidhaa zilizoongezwa thamani na wasichana wajasiriamali waliowezeshwa na Shirika la CAMFED walipotembelea maonesho ya bidhaa kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, uliofanyika Msimbazi Center.


Mgeni rasmi kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, Meneja Mafunzo wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo nchini Tanzania (SIDO), Bw. Stephen Bando (kulia) aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa SIDO akitembelea maonesho ya bidhaa kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, uliofanyika Msimbazi Center. Walioambatana naye ni Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura pamoja na Mkurugenzi wa CAMFED, Lydia Wilbard.

Mgeni rasmi kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, Meneja Mafunzo wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo nchini Tanzania (SIDO), Bw. Stephen Bando pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura wakitembelea maonesho ya bidhaa kwenye Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, uliofanyika Msimbazi Center.


Mmoja wa wanufaika wa Shirika la CAMFED, Bi. Eva John akielezea CAMFED ilivyomuwezesha katika kilimo cha nanasi na alianza na heka moja lakini sasa amefanikiwa kufikisha hekari sita za shamba la mananasi.

Na Joachim Mushi, Dar

SHIRIKA la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo nchini Tanzania (SIDO) limeziomba halmashauri zenye miradi ya Shirika la CAMFED inayowasaidia na kuwawezesha wasichana kielimu na uchumi kutoa ushirikiano ili kufanikisha miradi hiyo.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Meneja Mafunzo wa SIDO, Bw. Stephen Bando alipokuwa akifungua Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, ulioshirikisha wasichana wanufaika na miradi anuai ya CAMFED.

“…Nitoe wito kwa kurugenzi tendaji za halmashauri na kamati za wilaya za CAMFED kuendelea kutoa ushirikiano wa dhati katika kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya CAMFED inayoendelea kwa wasichana ili iweze kuleta tija zaidi kwa mtandao wa CAMA na kwa jamii kwa ujumla,” alisema Bw. Stephen Bando.

Pamoja na hayo alitoa wito kwa mashirika mengine kuiga mfano wa CAMFED kwa kuwasaidia vijana kwani vijana ni nguvu kazi muhimu kwa maendeleo ya taifa la leo na la kesho.

Aidha alisisitiza kuwa, Shirika la SIDO litaendelea kushirikiana na CAMFED ili kuhakikisha miradi ya kuwasaidia wasichana hao kupata elimu ya ufundi na ujuzi inafanikiwa zaidi na kuwa na tija ili kundi hilo la vijana liweze kujitegemea.

“…Naomba kuwashukuru sana Shirika la CAMFED na kuwaomba wadau wengine ili kuhakikisha wasichana wanapata fursa za kielimu, kiujuzi, ufundi, mafunzo ya biashara, mikopo ya elimu ya juu, pamoja na kupata shughuli za kujitegemea ili waweze kujikomboa kiuchumi,” alisema Bw. Bando.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura akizungumza katika mkutano huo, alisema shirika hilo tayari limesaidia wasichana 1193 Kwenye mitaji na mikopo yenye thamani ya sh 1,007,120,000/- kutoka wilaya 32 za mradi ndani ya mikoa 9, ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kutekeleza sera ya uchumi wa viwanda.

ADVERTISEMENT

Hata hivyo, alibainisha kuwa CAMFED imetoa mafunzo ya biashara na mbinu mbalimbali za kujikwamua kiuchumi kwa kushirikiana na wadau ikiwemo SIDO na wadau wa halmashauri kwenye halmashauri wanazofanya miradi.

Awali akitoa ushuhuda, katika kuwezeshwa kibiashara msichana Bi. Eva John aliwataka vijana hasa wa kike kutokata tamaa katika kupambana kujikwamua kiuchumi kwani yeye akiwezeshwa na CAMFED alianza kilimo cha nanasi na heka moja lakini sasa amefanikiwa kufikisha hekari sita. “…Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kwamba tusikate tamaa wanawake au wasichana tunaweza ukithubutu unaweza, tuanzishe kile ambacho tunaona tunaweza kukifanya na hatimaye kwa jitihada tunaweza kufikia malengo yetu…,” alisisitiza Bi. Eva John ambaye kwa sasa ni mkulima mzuri wa mananasi Chalinze. 

Mkutano huo ulikwenda sambamba na uzinduzi wa program maalum ya kuwawezesha wasichana kiongozi wa biashara ambao watakwenda kutoa elimu zaidi kwa wasichana katika kata zao na kujikuta kundi kubwa la mabinti wakinufaika kwa kuwa wajasiriamali hivyo kujikwamua kiuchumi na pia kuchangia pato la taifa.


Mmoja wa wanufaika wa Shirika la CAMFED, akielezea CAMFED ilivyomuwezesha katika kilimo cha nanasi na alianza na heka moja lakini sasa amefanikiwa kufikisha hekari sita za shamba la mananasi.


Baadhi ya washiriki Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, wakifuatilia mada anuai zikiwasilishwa katika mkutano huo.


Meneja Miradi wa CAMFED, Anna Sawaki (kushoto) akizungumza na washiriki Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika hilo.




SHIRIKA la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo nchini Tanzania (SIDO) limeziomba halmashauri zenye miradi ya Shirika la CAMFED inayowasaidia na kuwawezesha wasichana kielimu na uchumi kutoa ushirikiano ili kufanikisha miradi hiyo.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Meneja Mafunzo wa SIDO, Bw. Stephen Bando alipokuwa akifungua Mkutano wa Mwaka Kitaifa wa Shirika la CAMFED, ulioshirikisha wasichana wanufaika na miradi anuai ya CAMFED.

“…Nitoe wito kwa kurugenzi tendaji za halmashauri na kamati za wilaya za CAMFED kuendelea kutoa ushirikiano wa dhati katika kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya CAMFED inayoendelea kwa wasichana ili iweze kuleta tija zaidi kwa mtandao wa CAMA na kwa jamii kwa ujumla,” alisema Bw. Stephen Bando.

Pamoja na hayo alitoa wito kwa mashirika mengine kuiga mfano wa CAMFED kwa kuwasaidia vijana kwani vijana ni nguvu kazi muhimu kwa maendeleo ya taifa la leo na la kesho.

Aidha alisisitiza kuwa, Shirika la SIDO litaendelea kushirikiana na CAMFED ili kuhakikisha miradi ya kuwasaidia wasichana hao kupata elimu ya ufundi na ujuzi inafanikiwa zaidi na kuwa na tija ili kundi hilo la vijana liweze kujitegemea.

“…Naomba kuwashukuru sana Shirika la CAMFED na kuwaomba wadau wengine ili kuhakikisha wasichana wanapata fursa za kielimu, kiujuzi, ufundi, mafunzo ya biashara, mikopo ya elimu ya juu, pamoja na kupata shughuli za kujitegemea ili waweze kujikomboa kiuchumi,” alisema Bw. Bando.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya CAMFED, Bi. Jeanne Ndyetabura akizungumza katika mkutano huo, alisema shirika hilo tayari limesaidia wasichana 1193 Kwenye mitaji na mikopo yenye thamani ya sh 1,007,120,000/- kutoka wilaya 32 za mradi ndani ya mikoa 9, ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kutekeleza sera ya uchumi wa viwanda.

Hata hivyo, alibainisha kuwa CAMFED imetoa mafunzo ya biashara na mbinu mbalimbali za kujikwamua kiuchumi kwa kushirikiana na wadau ikiwemo SIDO na wadau wa halmashauri kwenye halmashauri wanazofanya miradi.

Awali akitoa ushuhuda, katika kuwezeshwa kibiashara msichana Bi. Eva John aliwataka vijana hasa wa kike kutokata tamaa katika kupambana kujikwamua kiuchumi kwani yeye akiwezeshwa na CAMFED alianza kilimo cha nanasi na heka moja lakini sasa amefanikiwa kufikisha hekari sita. “…Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kwamba tusikate tamaa wanawake au wasichana tunaweza ukithubutu unaweza, tuanzishe kile ambacho tunaona tunaweza kukifanya na hatimaye kwa jitihada tunaweza kufikia malengo yetu…,” alisisitiza Bi. Eva John ambaye kwa sasa ni mkulima mzuri wa mananasi Chalinze.

Mkutano huo ulikwenda sambamba na uzinduzi wa program maalum ya kuwawezesha wasichana kiongozi wa biashara ambao watakwenda kutoa elimu zaidi kwa wasichana katika kata zao na kujikuta kundi kubwa la mabinti wakinufaika kwa kuwa wajasiriamali hivyo kujikwamua kiuchumi na pia kuchangia pato la taifa.

Mwisho.

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar
HABARI

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

by Mhariri
Jan 22, 2021
0

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP...

Read more
Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Jan 22, 2021
Naibu Waziri Kipanga aagiza Vyuo vya VETA kwenye Wilaya 25 vyote vikamilike kwa wakati

Naibu Waziri Kipanga aagiza Vyuo vya VETA kwenye Wilaya 25 vyote vikamilike kwa wakati

Jan 22, 2021
Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato (+video)

Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato (+video)

Jan 22, 2021
Rais wa Zanzibar akutana na IGP Sirro

Rais wa Zanzibar akutana na IGP Sirro

Jan 22, 2021
Waziri Aweso awaagiza SUMAJKT kuongeza nguvu kazi kwenye ujenzi wa tanki la Maji Chamwino

Waziri Aweso awaagiza SUMAJKT kuongeza nguvu kazi kwenye ujenzi wa tanki la Maji Chamwino

Jan 22, 2021
Next Post
Mawaziri SADC – Troik wakutana kwa dharura Botswana

Mawaziri SADC - Troik wakutana kwa dharura Botswana

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

November 2020
M T W T F S S
« Oct   Dec »
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
30  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In