Bilioni 4 zatengwa kuimarisha miundombinu Jangwani – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Bilioni 4 zatengwa kuimarisha miundombinu Jangwani

Mhariri by Mhariri
Dec 3, 2020
in HABARI
0 0
0
Bilioni 4 zatengwa kuimarisha miundombinu Jangwani
0
SHARES
32
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Serikali kupitia Mfuko wa Barabara (Road fund) imesema ipo tayari kupitisha kiasi cha shilingi bilioni nne kwa ajili ya kumlipa mkandarasi atakaepatikana ili kuboresha miundombinu ya jangwani mara baada ya uhakiki wa makisio hayo kukamilika na kujiridhisha.

Akizungumza kwa niaba ya wajumbe wa Bodi ya mfuko huo, Mwenyekiti wa Bodi Bw. Joseph Haule, amesema kuwa nia ya Serikali ni kuhakikisha inatatua changamoto hiyo haraka kabla ya mvua za masika kuanza.

“Bodi imeona tatizo hili na tumeliona kama suala la dharura, ndio maana tumekuja hapa kujionea hali halisi ili kutafuta njia sahihi ya kutatua tatizo hili ambalo limekuwa kero kwa muda mrefu”, amesema Mwenyekiti wa Bodi.

Aidha, Bw. Haule amefafanua kuwa kweli tatizo ni kubwa, mfereji una kina kifupi na makalvati mawili makubwa yaliyopo hapo yameziba kabisa.

Ameongeza kuwa nia ya Bodi ni kuona wananchi na wasafirishaji wanatumia muindombinu hiyo wakati wote wa mvua na kiangazi

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, amesema kuwa Serikali kupitia Wizara yake imeandaa mkakati wa muda mrefu kuhusu miundombinu hiyo ambapo amesema kuwa kwa sasa wataalamu wanafanya usanifu wa kina kwa ajili ya kuja na suluhisho la kudumu ikiwemo ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 300.

ADVERTISEMENT

Mwakalinga amefafanua kuwa aliagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi wa haraka ikiwemo kutoa mchanga ambao umetuama katika eneo hilo ili kuinusuru miundombinu hiyo.

Naye, Meneja wa TANROADS mkoa wa Dar es salaam, Mhandisi Julius Ngusa, amethibitisha kuwa ofisi yake inaendelea kuhakikisha kuwa michanga inayotuama katika eneo hilo inatolewa kwa wakati ili kuruhusu magari kuweza kupita mara baada ya mvua kunyesha.

Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Barabara wametembelea eneo la Jangwani kujionea hali halisi ya miundombinu katika eneo hilo ambayo imekuwa ikiathiriwa na mvua na kusababisha kufunga mawasiliano ya watumiaji wa barabara ya Morogoro hususani eneo hilo kila mwaka.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Rais Magufuli ashuhudia utiaji saini mkataba wa uchimbaji wa madini ya Nickel
HABARI

Rais Magufuli ashuhudia utiaji saini mkataba wa uchimbaji wa madini ya Nickel

by Ombeni Osward
Jan 19, 2021
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

Read more
Kijana amuua babu yake kumnusuru na mateso

Kijana amuua babu yake kumnusuru na mateso

Jan 19, 2021
Rwanda yaendeleza Lockdown kupunguza maambukizi ya Corona

Rwanda yaendeleza Lockdown kupunguza maambukizi ya Corona

Jan 19, 2021
Lacazette ananisaidia kuongeza ujasiri – Smith Rowe

Lacazette ananisaidia kuongeza ujasiri – Smith Rowe

Jan 19, 2021
Hospitali ya Uhuru yatibu wagonjwa 300

Hospitali ya Uhuru yatibu wagonjwa 300

Jan 19, 2021
Watumishi wa NCAA watakiwa kuweka Malengo ya Utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya chama tawala 2020 – 2025

Watumishi wa NCAA watakiwa kuweka Malengo ya Utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya chama tawala 2020 – 2025

Jan 19, 2021
Next Post
Rais Magufuli aahirisha maadhimisho ya sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara

Rais Magufuli aahirisha maadhimisho ya sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

December 2020
M T W T F S S
« Nov   Jan »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In