Rais wa Ufaransa amwandikia barua Rais Magufuli – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Rais wa Ufaransa amwandikia barua Rais Magufuli

Mhariri by Mhariri
Dec 3, 2020
in HABARI
0 0
0
Rais wa Ufaransa amwandikia barua Rais Magufuli
0
SHARES
39
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Serikali imesema katika kipindi cha pili cha awamu ya pili ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli itajikita zaidi katika kuboresha uwekezaji wa ndani na nje ya nchi na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika kujenga uchumi wa nchi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa hapa Nchini na kuongeza kuwa baada ya kipindi cha kwanza cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Dkt John Pombe Magufuli kujikita katika uwekezaji mkubwa wa maeneo ya miundombinu na nishati pamoja na huduma za kijamii sasa serikali inalenga kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi katika ujenzi wa uchumi.

Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Mhe. Frederic Clavier amemkabidhi Prof Kabudi barua ya iliyoandikwa na Rais wa Ufaransa Mhe Emmanuel Macron kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kumpongeza kwa kuiwezesha Tanzania kuingia katika uchumi wa kati ikiwa ni miaka mitano kabla ya muda uliopangwa.

Pia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa Nchini Mhe Manfred Fanti ambapo Balozi Fanti ameweleza Waziri Kabudi kuwa pamoja na kamati ya mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili masuala mbalimbali yanayoihusu Tanzania bado umoja hakuna maazimio yeyote yaliyofikiwa kuhusu Tanzania na kwamba Umoja wa Ulaya utaendelea kuimarisha mahusiano mazuri na ya kihistoria yaliopo kati ya Tanzania na Umoja huo.

Balozi Fanti ameihakikishia Tanzania kuwa Umoja Ulaya utatekeleza miradi yote iliyopangwa kutekelezwa Nchini kwa ufadhili wa Umoja huo.

ADVERTISEMENT

Katika tukio jingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Kesi Masalia za Mauaji ya Kimbari (International Residual Mechanism for Criminal Tribunals -IRMCT)na Bwana Abubacar Tambadou.

Katika mazungumzo yao Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Kesi Masalia za Mauaji ya Kimbari (International Residual Mechanism for Criminal Tribunals -IRMCT)na Bwana Abubacar Tambadou amemweleza Waziri Kabudi kuwa amefika kujitambulisha baada ya kupata uteuzi huo lakini pia kuishukuru Tanzania kwa ushirikiano unaoutoa kwa Mahakama hiyo na kuomba kuendelea kutoa ushirikiano ili kuiwezesha kutimiza majukumu yake.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi
HABARI

Walimu wamtoa mimba mwanafunzi, wakamatwa na Polisi

by Mhariri
Jan 22, 2021
0

Na Amiri Kilagalila,Njombe Jeshi la Polisi mkoani...

Read more
Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Serikali yajipanga kumaliza changamoto ya uhaba wa mafuta ya kula nchini

Jan 22, 2021
Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Amuua mdogo wake kisa kuku kuingia kwenye shamba lake

Jan 22, 2021
Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Mkuu wa Majeshi ya Malawi kushiriki mashindano ya Golf ya Johnnie Walker Waitara Trophy

Jan 22, 2021
IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

IGP Sirro akemea vitendo vya udhalilishaji Zanzibar

Jan 22, 2021
Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Kiwanda cha Twiga Cement wamkabidhi RC Kunenge mifuko 800 ya Saruji

Jan 22, 2021
Next Post
Benki ya NMB Yakabidhiwa Cheti kwa Kudhamini Kongamano la Ugavi na Ununuzi Arusha

Benki ya NMB Yakabidhiwa Cheti kwa Kudhamini Kongamano la Ugavi na Ununuzi Arusha

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

December 2020
M T W T F S S
« Nov   Jan »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In