Video: Jamii yatakiwa kutowanyanyapaa watu wenye ulemavu – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Video: Jamii yatakiwa kutowanyanyapaa watu wenye ulemavu

Mhariri by Mhariri
Dec 2, 2020
in HABARI
0 0
0
Video: Jamii yatakiwa kutowanyanyapaa watu wenye ulemavu
0
SHARES
33
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Ezekiel Mtonyole – Dodoma.

Kuelekea katika siku ya walemavu duniani ambayo huadhimishwa Disemba 3, kila mwaka jamii imetakiwa kuacha kuwanyanyapaa watu wenye ulemavu bali ione watu wenye ulemavu nao ni miongoni mwa jamii inayotakiwa kupata fulsa sawa na watu wengine.

Hayo yamebainishwa Jijini Dodoma na mwenyekiti wa shirika la Foundation for disabilities hope bwana Michael Silari wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea siku hiyo ambayo kitaifa itafanyika Dodoma amesema bado kundi la watu wenye ulemavu linaachwa nyuma na jamii na kuona kama sio miongoni mwa jamii.

“Tunatoa wito kwa jamii kuona kundi hili nalo ni miongoni mwa jamii na ndio maana hata haya maadhimisho huwa tunapeleka katika mikoa mbalimbali ili kupanua uelewa wa jamii juu ya watu wen ye ulemavu” amesema Silari.

ADVERTISEMENT

Amesema siku hiyo iliwekwa kwa lengo la kuwaunganisha watu wenye ulemavu na kujadili mambo mbalimbali yanayohusu watu wenye ulemavu na kujadili kwa pamoja mambo hayo ili kujenga umoja miongoni mwao.

Amebainisha kuwa bado kuna changamoto nyingi zinazolikabili kundi hilo kwani jamii huliona kundi hilo kuwa haliwezi jambo lolote bali walemavu ni kama watu wengine na wanatakiwa kushirikishwa katika mambo mbalimbali yanayoizunguka jamii.

Amesema changamoto nyingine ni watu wenye ulemavu wenyewe kujinyanyapaa na kuona hawawezi kitu chochote amewataka kubadilika kwani nao ni miongoni mwa watu katika jamii wanaotakiwa kuleta maendeleo kama watu wengine.

“Watu wenye ulemavu wenyewe wamekuwa wakijinyanyapaa na kuona kama sio miongoni mwa jamii nataka wajiamini kwani nao ni miongoni mwa jamii inayotegemewa kuleta maendeleo katika jamii” amesema.

Ameishukuru serikali kwa kuendelea kuwaanini watu wenye ulemavu na kuwateua katika nyanja mbalimbali za uongozi sambamba na kutenga asilimia 2 za makusanyo ya halmashauri kwa ajili kuwawezesha watu wenye ulemavu kuwainua kiuchumi.

“Tuishukuru serikali kwa kuendelea kutuamini imeteua watu wenye ulemavu katika maeneo mbalimbali na tunaona watu wenye ulemavu wamefanya vizuri katika kazi hizo na sisi kama shirika tutaendelea kushirikiana na serikali katika kuhimiza watu wenye ulemavu kujitokeza kwenye mikopo hiyo” amesema.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma
HABARI

Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

by Mhariri
Jan 15, 2021
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano...

Read more
NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

Jan 15, 2021
Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Jan 15, 2021
Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Jan 15, 2021
Serikali yawakaribisha wawekezaji katika sekta ya mawasiliano hapa nchini

Serikali yawakaribisha wawekezaji katika sekta ya mawasiliano hapa nchini

Jan 15, 2021
Waziri Aweso asitisha agizo la EWURA kupandisha Ankara za Maji

Waziri Aweso asitisha agizo la EWURA kupandisha Ankara za Maji

Jan 15, 2021
Next Post
Rais Dk. Mwinyi akutana na mwakilishi wa UNICEF Zanzibar

Rais Dk. Mwinyi akutana na mwakilishi wa UNICEF Zanzibar

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

December 2020
M T W T F S S
« Nov   Jan »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In