Viongozi wa Mikoa wekeni mikakati endelevu ujenzi wa madarasa – Naibu Waziri Silinde – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Viongozi wa Mikoa wekeni mikakati endelevu ujenzi wa madarasa – Naibu Waziri Silinde

Mhariri by Mhariri
Dec 15, 2020
in HABARI
0 0
0
Viongozi wa Mikoa wekeni mikakati endelevu ujenzi wa madarasa – Naibu Waziri Silinde
0
SHARES
78
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe David Silinde amewaagiza Viongozi wa Mikoa yote nchini kuhakikisha zoezi la ujenzi wa madarasa linakuwa endelevu na kuwekewa mikakati maalum ili kupunguza uhaba wa madarasa nchini.

Ametoa agizo hilo leo wakati akikagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Mkoani Rukwa ambapo Mhe. Silinde amesema zoezi la ujenzi wa madarasa si la kushitukiza, hivyo ni vyema viongozi wote ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kuweka mikakati madhibuti ya kuhakikisha madarasa yanajengwa kwa wakati.

“Haiwezekani kila mwaka tunajua idadi ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi lakini bado tunakuwa na uhaba wa madarasa nchini, hali hii inapoteza haki ya watoto waliofaulu vizuri mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi kukosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza” amesisitiza Mhe. Silinde

Mhe. Silinde anafafanua kuwa Serikali itahakikisha inakagua na kujiridhisha utoshelevu wa madarasa kwa watoto wote waliofaulu Mitihani ya kumaliza shule ya msingi na kuwa watahakikisha kuwa wanapangiwa shule.

Amesema Serikali hahitaji maneno mengi kinachohitajika ni kuwa madarasa yamekamilika, kwa kuwa, watoto kujiunga na Kidato cha kwanza si jambo la dharura, hili ni jambo linalofahamika katika kipindi chote, hivyo udharura huihitajiki katika miaka mingine inayokuja “amesisitiza Mhe. Silinde

Mhe Silinde amesema kuwa zoezi la ujenzi wa madarasa linatakiwa kuwa endelevu na kuhakikisha kuwa hakuna uhaba wa madarasa kulingana na wanafunzi wote wanaoongezeka kila mwaka.

“Inafahamika kuwa kunaongezeko kubwa na wanafunzi kila mwaka, wanafunzi wanaofuatia kwa mwaka mwingine, pia ongezeko la idadi ya watu kila mwaka katika taifa letu, hivyo kila Mkoa uhakikishe unajipanga na kuweka mikakati madhubuti ya kutatua tatizo la madarasa” amesema mhe. Silinde.

Mhe. Silinde ametoa Rai maeneo yatakayoonekana na upungufu mkubwa wa madarasa, vifaa ikiwemo madawati Serikali haitasita kuwachukulia hatua viongozi wa eneo hilo kwa kushindwa kutimiza majukumu yao kikamilifu.

Ameendelea kufafanua kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inafuatilia na kuhakikisha hakuna muda wa kupumzika katika kipindi chote mpaka watoto wote waliofaulu na kuchagulliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanasoma madarasani

Wakati huohuo Mkuu wa Wilaya ya Sumabawanga Mhe. Halfani Haule amesema mpaka sasa Halmashauri hiyo imejipanga kukamilisha maboma ya madarasa yaliyopo lengo likiwa kuhakikisha watoto waliofaulu elimu ya msingi wote wanachaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na wanakaa darasani

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Mwl. Nyangi Msema kweli amesema kuwa Halmashauri hiyo imetenga kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya shule ili kuhakikisha wanafunzi zaidi ya 4400 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanaingia darasani ifikapo januari, 2021.

Mhariri

Mhariri

Related Posts

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza kuziuza  kwa Axian consortium
HABARI

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza kuziuza kwa Axian consortium

by I am Krantz
Apr 19, 2021
0

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza...

Read more

Mwanangu kaacha kutumia pombe na dawa za kulevya, hivi ndivyo alivyosaidika

Apr 19, 2021
Waziri Mwambe ahimiza Watanzania kuunga mkono Benki ya CRDB asema ni Benki ya kizalendo yenye nia ya dhati ya kuwakomboaa wananchi kiuchumi

Waziri Mwambe ahimiza Watanzania kuunga mkono Benki ya CRDB asema ni Benki ya kizalendo yenye nia ya dhati ya kuwakomboaa wananchi kiuchumi

Apr 19, 2021
Waajiri Serikalini Watakiwa Kuwa Na Mabaraza Ya Wafanyakazi Yanayofanya Kazi Kikamilifu

Waajiri Serikalini Watakiwa Kuwa Na Mabaraza Ya Wafanyakazi Yanayofanya Kazi Kikamilifu

Apr 16, 2021
Balozi Mulamula Apokea Nakala Ya Hati Za Utambulisho Kutoka Kwa Balozi Mteule Wa Uturuki

Balozi Mulamula Apokea Nakala Ya Hati Za Utambulisho Kutoka Kwa Balozi Mteule Wa Uturuki

Apr 16, 2021
Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Apr 16, 2021
Next Post
Rais Dk. Mwinyi ampongeza Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Rais Dk. Mwinyi ampongeza Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

December 2020
M T W T F S S
« Nov   Jan »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In