Waziri Ndugulile aipa TCRA miezi mitatu kumaliza changamoto za vifurushi na bando kwa wananchi – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Waziri Ndugulile aipa TCRA miezi mitatu kumaliza changamoto za vifurushi na bando kwa wananchi

Mhariri by Mhariri
Dec 28, 2020
in HABARI
0 0
0
Waziri Ndugulile aipa TCRA miezi mitatu kumaliza changamoto za vifurushi na bando kwa wananchi
0
SHARES
119
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt.Faustine Ndugulile ameipa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) miezi mitatu kumaliza changamoto za bando na vifurushi zinazotolewa na kampuni za simu za mkononi kwa wananchi

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo wakati wa ziara yake alipotembelea TCRA ikiwa ni moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa lengo la kufahamiana, kutambua majukumu yao na kuzungumza na Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa taasisi hiyo ili kuwa na uelewa wa pamoja na kushirikiana kwa kufanya kazi kwa pamoja katika kuhudumia wananchi kuelekea Mapinduzi ya Nne ya Viwanda na kuiwezesha Tanzania kuwa na uchumi wa kidijitali

Ameongeza kuwa TCRA ishughulikie malalamiko ya wananchi kwa kuwa wananchi hawana imani na vifurushi na bando, na kuwe na mfumo wa kuhakiki gharama halisi za mawasiliano kuendana na fedha aliyotoa mwananchi na kuwe na namba ya bure ambayo wananchi watapiga ili kuwasilisha malalamiko yao ili kuwawezesha wananchi kuongeza imani yao kwa Serikali

Amesisitiza kuwa ni heri tufanye maamuzi mabaya kuliko kutokufanya maamuzi na amewataka washirikiane na Baraza la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA – CCC) kumaliza changamoto hiyo kwa kuwa watanzania sio wajinga, anataka aone kapata shilingi moja anaitumia shilingi moja yake kupiga simu

Pia, amehimiza wahakikishe kuwa chaneli tano za bure za runinga zinaonekana hata baada ya muda wa kulipia kumalizika kwa kuwa chaneli hizo hazionekani kwenye baadhi ya ving’amuzi.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (wa pili kushoto) na Naibu Waziri wake, Mhandisi Kundo A. Mathew (wa tatu kushoto) wakimsikiliza Mhandisi Jumanne Ikuja akiwaeleza kuhusu gari lenye mitambo maalumu linalofuatilia matumizi ya masafa wakati wa ziara yao Mamlaka ya mawasiliano Tanzania, Dar es Salaam. Wa nne kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Mhandisi James Kilaba

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo A. Mathew ameipongeza TCRA kwa kutengeneza mifumo ya TEHAMA, kutambua changamoto zilizopo na imejipanga kuzifanyia kazi kwa kuwa lazima TEHAMA ichukue nafasi yake na itufikishe watanzania tunakotaka kwenda

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Zainab Chaula amewataka wafanyakazi wa TCRA kujiongeza na kujituma zaidi badala ya kusubiri maagizo na maelekezo kwa kuwa wao ni wataalamu, hivyo washirikiane kwa pamoja ili kuhakikisha kuwa wanaendelea kuwahudumia watoa huduma na watumiaji wa huduma za mawasiliano

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba amekiri uwepo wa changamoto za bando na vifurushi na ameahidi kuzifanyia kazi kwa kuwa TEHAMA imeongeza mnyororo wa thamani kwenye sekta zote na imesogeza huduma mbali mbali viganjani.

Mhariri

Mhariri

Related Posts

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza kuziuza  kwa Axian consortium
HABARI

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza kuziuza kwa Axian consortium

by I am Krantz
Apr 19, 2021
0

Millicom International inayozimiliki Tigo na Zantel yatangaza...

Read more

Mwanangu kaacha kutumia pombe na dawa za kulevya, hivi ndivyo alivyosaidika

Apr 19, 2021
Waziri Mwambe ahimiza Watanzania kuunga mkono Benki ya CRDB asema ni Benki ya kizalendo yenye nia ya dhati ya kuwakomboaa wananchi kiuchumi

Waziri Mwambe ahimiza Watanzania kuunga mkono Benki ya CRDB asema ni Benki ya kizalendo yenye nia ya dhati ya kuwakomboaa wananchi kiuchumi

Apr 19, 2021
Waajiri Serikalini Watakiwa Kuwa Na Mabaraza Ya Wafanyakazi Yanayofanya Kazi Kikamilifu

Waajiri Serikalini Watakiwa Kuwa Na Mabaraza Ya Wafanyakazi Yanayofanya Kazi Kikamilifu

Apr 16, 2021
Balozi Mulamula Apokea Nakala Ya Hati Za Utambulisho Kutoka Kwa Balozi Mteule Wa Uturuki

Balozi Mulamula Apokea Nakala Ya Hati Za Utambulisho Kutoka Kwa Balozi Mteule Wa Uturuki

Apr 16, 2021
Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Apr 16, 2021
Next Post
Waziri wa afya aridhishwa na uzalishaji wa Dawa katika kiwanda cha KEKO

Waziri wa afya aridhishwa na uzalishaji wa Dawa katika kiwanda cha KEKO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

December 2020
M T W T F S S
« Nov   Jan »
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In