RC Njombe asitisha vibali vya ujenzi maeneo ya karibu na uwanja wa Ndege – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

RC Njombe asitisha vibali vya ujenzi maeneo ya karibu na uwanja wa Ndege

Mhariri by Mhariri
Jan 9, 2021
in HABARI
0 0
0
RC Njombe asitisha vibali vya ujenzi maeneo ya karibu na uwanja wa Ndege
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Amiri Kilagalila,Njombe

Halmashauri ya mji wa Njombe imeagizwa kusitisha utoaji wa vibali vya ujenzi wowote kwa wananchi maeneo ya karibu na uwanja wa Ndege ili kupisha utekelezaji wa mradi wa uwanja wa kisasa mkoani humo.

Agizo hilo lilitolewa na mkuu wa mkoa wa Njombe mhandisi Marwa Rubirya katika kikao cha bodi ya barabara ya mkoa kilichofanyika mjini Njombe

Amesema miradi inayotekelezwa na serikali inachukua muda kukamilisha maandalizi yake na Ilani ya Chama cha mapinduzi inaonyesha ni miongoni mwa viwanja ambavyo vipo kwenye mpango wa kujengwa upya na hata mwaka jana Rais Dkt, John Pombe Magufuli akifungua bunge alilizungumza hilo.

ADVERTISEMENT

“Tukiruhusu wananchi kuendelea kujenga sisi wenyewe tutakuwa tunakwamisha utekelezaji wa mradi huu” Alisema Rubirya.

Ameelekeza halmashauri ya mji wa Njombe kusitisha utoaji wa vibali na kuhakikisha kuwa hakuna ujenzi unaoendelea kwenye eneo hilo.

Amesema mpaka sasa eneo pekee lililokubalika kujengwa uwanja wa ndege ni hapo ulipo na iwapo yatatokea maamuzi mbadala basi eneo hilo litabadilishwa matumizi na litatumika kwa shughuli zingine.

“Kwasababu hatujawa na mabadiliko ya matumizi ni bora tukazingatia maelekezo haya ambayo tuliyatoa kwenye kikao chetu ambayo naona yalikuwa maagizo halali kwa ajili ya maendeleo ya mkoa wetu” Alisema Rubirya.

Mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Masafiri amesema kumekuwa na maelezo ya muda mrefu kuwa uwanja huo utajengwa kwa kiwango cha lami ili ndege ziwe zinatua na kuruka uwanjani hapo lakini limekuwa kwenye mazungumzo tu.

Amesema matokeo yake majirani wanaendelea kukarabati nyumba na kuziongezea thamani ambapo kwa namna moja au nyingine suala hilo linaleta mgogoro huku mahitaji ya uwanja wa ndege katika mkoa huo hayazuiliki kwa kuwa kasi ya wananchi kujiletea maendeleo yao ni kubwa.

Alisema ndege inapotua Iringa robo tatu ya abiria wanaoshuka kwenye uwanja huo ni wananchi wa Njombe ambao baada ya hapo wanalazimika kupanda magari kuelekea mkoani Njombe.

“Kutokana na hilo naona tunahitaji sana kiwanja chetu kiliko kutegemea viwanja vingine” Alisema Ruth.

Awali mbunge wa jimbo la Njombe mjini Deo Mwanyika alitaka ufafanuzi juu ya zuio la ujenzi katika maeneo hayo ni kwa magorofa pekee au hata ujenzi wa kawaida.

Alisema kumekuwa na zuio kwa wananchi kusitisha ujenzi lakini kama mbunge zuio hilo lililenga aina gani za majengo kabla ya kupata ufafanuzi uliotolewa.

“Nataka nielewe kwasababu sijui stop order inazungumzia magorofa tu kwakuwa ndiyo naona yamesimama ujenzi lakini naona katika ujenzi wa kawaida maeneo mengine unaendelea” Alisema Mwanyika.

ADVERTISEMENT
Mhariri

Mhariri

Related Posts

Dkt.JPM ampongeza Mseveni kushinda Urais
HABARI

Dkt.JPM ampongeza Mseveni kushinda Urais

by Ombeni Osward
Jan 16, 2021
0

Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania...

Read more
Raia wa Kenya ashikiliwa na TAKUKURU kwa kujaribu kumhonga apatiwe cheti cha COVID 19

Raia wa Kenya ashikiliwa na TAKUKURU kwa kujaribu kumhonga apatiwe cheti cha COVID 19

Jan 16, 2021
Nyumba 6 zaezuliwa na upepo mkali ulioambata na mvua mkoani Njombe

Nyumba 6 zaezuliwa na upepo mkali ulioambata na mvua mkoani Njombe

Jan 16, 2021
Mseveni ashinda Urais tena

Mseveni ashinda Urais tena

Jan 16, 2021
Bilioni 11 zaokolewa chakula cha Wafungwa

Bilioni 11 zaokolewa chakula cha Wafungwa

Jan 16, 2021
Waziri Ndugulile awataka wakuu wa Taasisi zilizochini yake kuwa wabunifu ili kuleta mafanikio

Waziri Ndugulile awataka wakuu wa Taasisi zilizochini yake kuwa wabunifu ili kuleta mafanikio

Jan 16, 2021
Next Post
Hospitali yatangaza kutoa matibabu bure siku ya Mapinduzi ya Zanzibar

Hospitali yatangaza kutoa matibabu bure siku ya Mapinduzi ya Zanzibar

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

January 2021
M T W T F S S
« Dec    
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In