Zanzibar yaokoa mamilioni sherehe za Mapinduzi – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

Zanzibar yaokoa mamilioni sherehe za Mapinduzi

Ombeni Osward by Ombeni Osward
Jan 13, 2021
in HABARI
0 0
0
Zanzibar yaokoa mamilioni sherehe za Mapinduzi
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imelazimika kupunguza baadhi ya shamra shamra za maadhimisho ya kusherehekea miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ili kuokoa fedha na kuzielekeza katika matumizi mengine ya serikali,ikiwemo huduma za kijamii.

Dk. Mwinyi amesema hayo katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilizofanyika leo katika viwanja vya Mnazi mmoja Jijini hapa.

Amesema Serikali ilikuwa na azma ya kuzipamba sherehe hizo kwa shamra shamra mbali mbali kama ilivyozoeleka na Wazanzibari wote, lakini kutokana na hali ya uchumi, sherehe hizo zimetekelezwa kwa njia tofauti na ilivyozoeleka.

Alieleza kuwa hali hiyo ni ya mpito na kubainisha kawa pale itakapotengemaa (katika siku za usoni), utaratibu wa kawaida wa maadhimisho ya sherehe hizo utarejea.

Alisema wakati umefika kwa Wazanzibari kujikita katika Uchumi wa Buluu, kwa kuzingatia shabaha ya Mapinduzi hayo ambayo ni kustawisha maisha ya wananchi wake.

Aidha, alisema Wazanzibari wanapaswa kupata huduma bora na stahili, ikiwemo elimu, afya na maji na kwa wale watakaohitaji kufanya biashara waweze kufanya shughuli zao bila kiuzuizi wala vikwazo vitokanavyo na rushwa.

Alisema Mapinduzi ya kiuchumi ndio mapinduzi yatakayotoa majibu ya changamoto ziliopo na vizazi vijavyo.

Alisema Wazanzibari wanahitaji Mapinduzi katika sheria na taasisi ili kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao bila bughudha wala vikwazo pamoja na kuwepo Mapinduzi katika Sanaa na Michezo ili kila mmoja aweze kutumia uwezo na kipaji chake kucheza na kujiendeleza kimaisha.

ADVERTISEMENT

Katika hatua nyengine, Dk. Mwinyi alisema Mapinduzi yanayohitajika yatawezekana endapo mambo tofauti yatatekelezwa, ikiwemo kuufungua Uchumi kwa kuweka mazingira mazuri .

Alisema ni azma ya serikali anayoiongoza kuvutia Wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi ili kuendeleeza uchumi wa buluu.

Aidha, alisema eneo jengine linalohitaji Mapinduzi ni kuongeza juhudi katika ukusanyaji wa kodi mbali mbali.

(@ikulu_habari)

ADVERTISEMENT
Ombeni Osward

Ombeni Osward

Related Posts

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu
HABARI

NMB yatoa msaada wa mabati kutekeleza agizo la Waziri Mkuu

by I am Krantz
Jan 15, 2021
0

 Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Angelina Nkwingwa...

Read more
RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

RC Mahenge aliagiza Jiji la Dodoma kudhibiti Ujenzi Holela wa makazi

Jan 15, 2021
Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Picha: Makamu wa Rais aongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Chamwino Dodoma

Jan 15, 2021
NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne, zijue shule 10 zilizoongoza

Jan 15, 2021
Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Kisa cha kweli: Mapenzi ya Chuo yawachanganya, waenda kanisani kula kiapo

Jan 15, 2021
Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Rais wa Uturuki apewa chanjo ya Corona

Jan 15, 2021
Next Post
Malawi yatoa siku 3 za Maombolezo

Malawi yatoa siku 3 za Maombolezo

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

January 2021
M T W T F S S
« Dec    
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In