TANZIA: Brigedia Jenerali Emmanuel Edward Maganga (Mstaafu) afariki dunia – Mwanaharakati Mzalendo
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI

TANZIA: Brigedia Jenerali Emmanuel Edward Maganga (Mstaafu) afariki dunia

Mhariri by Mhariri
Jan 23, 2021
in HABARI
0 0
0
TANZIA: Brigedia Jenerali Emmanuel Edward Maganga (Mstaafu) afariki dunia
0
SHARES
39
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo anasikitika kutangaza kifo cha Afisa Mkuu Brigedia Jenerali Emmanuel Edward Maganga (Mstaafu), kilichotokea usiku wa tarehe 21 Januari, 2021 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi ya Kanda, Milambo Mkoani Tabora.

Marehemu Brigedia Jenerali Emmanuel Edward Maganga (Mstaafu) alizaliwa tarehe 18 Aprili, 1955 katika Kijiji cha Mombo, Kata ya Mombo, Tarafa ya Mombo, Wilaya ya Korogwe, katika Mkoa wa Tanga. Alipata Elimu katika ngazi mbalimbali ikiwemo Stashahada ya Uandishi wa Habari (Diploma in Journalism) kutoka Chuo cha Nyegezi Mwanza sasa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania.

Marehemu alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tarehe 01 Januari, 1979. Alihudhuria kozi ya Afisa Mwanafunzi nchini Tanzania na kutunukiwa Kamisheni tarehe 03 Aprili, 1980. Marehemu alipandishwa cheo kuwa Brigedia Jenerali tarehe 02 Septemba, 2011 kulingana na kozi za Kijeshi alizohudhuria katika utumishi wake. Marehemu alitumikia Jeshi kwa muda wa miaka 37 na mwezi 1 hadi alipostaafu utumishi Jeshini kwa umri tarehe 31 Januari, 2016.

Marehemu Brigedia Jenerali Maganga (Mstaafu) alitunukiwa Medali mbalimbali wakati wa utumishi wake ifuatavyo:- Miaka 20 ya JWTZ; Utumishi Mrefu Tanzania; Miaka 40 ya JWTZ; Utumishi Uliotukuka Tanzania; Miaka 50 ya JWTZ; Miaka 50 ya Muungano; Miaka 50 ya Uhuru na Nishani ya Comoro.

Katika Utumishi wake Jeshini, aliwahi kushika madaraka mbalimbali yakiwemo, Afisa Mnadhimu Makao Makuu ya Jeshi; Kaimu Mkurugenzi, Tawi la Usalama na Utambuzi, Makao Makuu ya Jeshi; Mwambata Jeshi nchini Marekani; Mkuu wa Ukaguzi Jeshini, Makao Makuu ya Jeshi; Madaraka aliyohudumu hadi anastaafu tarehe 31 Januari, 2016; Rais na Amiri Jeshi Mkuu alimteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma (Baada ya Kustaafu), tarehe 13 Machi, 2016 hadi tarehe 03 Julai, 2020.

Heshima za mwisho kwa marehemu zitatolewa nyumbani kwa marehemu Yombo Buzza Dar es Salaam tarehe 24 Januari, 2021 Kuanzia saa 2:00 asubuhi. Baada ya hapo Mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda Turiani Mkoani Morogoro kwa mazishi yatakayofanyika Jumatatu tarehe 25 Januari, 2021.

Mhariri

Mhariri

Related Posts

SIMULIZI; Nilivyolinda Familia Yangu Isikamatwe Wakati Wakitengeneza Pombe
HABARI

SIMULIZI; Nilivyolinda Familia Yangu Isikamatwe Wakati Wakitengeneza Pombe

by I am Krantz
Feb 26, 2021
0

Nilizaliwa katika familia masikini sana na wakati...

Read more
Dkt. Ndungulile afurahishwa na huduma ya kufungua akaunti kidijitali kupitia SimBanking

Dkt. Ndungulile afurahishwa na huduma ya kufungua akaunti kidijitali kupitia SimBanking

Feb 26, 2021
Auto Draft

FAINALI NMB MASTABATA WIKI IJAYO, 424 WAZOA ZAWADI

Feb 24, 2021
Mamia wajitokeza kujisajili na Mbio za Kili Marathon Jijini Dar Es Salaam

Mamia wajitokeza kujisajili na Mbio za Kili Marathon Jijini Dar Es Salaam

Feb 23, 2021
BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGO YAHAMASISHA WANAFUNZI KUPENDA FANI HIYO

BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGO YAHAMASISHA WANAFUNZI KUPENDA FANI HIYO

Feb 23, 2021
Wateja wa Vodacom kuvuna Shilingi 4.1 bilioni za faida ya kutumia M-Pesa.

Wateja wa Vodacom kuvuna Shilingi 4.1 bilioni za faida ya kutumia M-Pesa.

Feb 23, 2021
Next Post
Anayedaiwa kumnasa makofi mzazi akutwa na hatia

Anayedaiwa kumnasa makofi mzazi akutwa na hatia

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

January 2021
M T W T F S S
« Dec   Feb »
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In