Wahitimu Chuo Cha Maji Wanaajirika – Aweso – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
Home HABARI TANZANIA

Wahitimu Chuo Cha Maji Wanaajirika – Aweso

Ombeni Osward by Ombeni Osward
Jan 9, 2021
in HABARI TANZANIA
0 0
0
Wahitimu Chuo Cha Maji Wanaajirika – Aweso
0
SHARES
19
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Chuo Cha Maji, kampasi ya Dar es Salaam kimefanya mahafali yake ya 12 katika Viunga vya Mlimani City Jijini Dar es Salaam, ambapo wanafunzi 529 wamehitimu huku miongoni mwao wakitunukiwa astashahada, stashahada na shahada ya kwanza.

Kwa upande wa shahada ni wahitimu 153, stashahada ni 355 na 21 kwa ngazi ya stashahada, kwa idadi yao 529 wanawake waliohitimu ni asilimia 32%.

 

Aidha katika mahafali haya mgeni rasmi alikuwa Waziri mwenye dhamana katika Wizara ya Maji Mh. Jumaa Aweso (Mb) ambaye pamoja naye aliambatana na Naibu wake Mh. MaryPrisca Mahundi (Mb) pamoja watendaji waandamizi wa wizara hiyo.

 

Pia Waziri Aweso wakati wa hotuba yake amegusia mchango adhimu unaotolewa na Chuo cha Maji pamoja na hamu thabiti ya Wizara ya Maji kufanya kazi na Chuo hicho katika kutatua changamoto za maji kwenye maeneo ya Mijini na Vijijni.

 

Zaidi Aweso amewamwagia sifa kedekede wahitimu hao kwa kusema kuwa wanaajirika huku akitaka Wizara ya Maji kuwatumia katika miradi mbalimbali, pamoja na kukabidhii miradi mitano kwa chuo hicho ili miradi hiyo kuwa ya mfano na ya kuwajengea uwezo wanafunzi wa chuo hicho.

Waziri huyo ameitaja Wizara yake kuwa miongoni mwa Wizara zenye miradi lukuki kwa kubainisha kuwa hadi sasa Serikali ya Rais John Magufuli imetekeleza na kukamilisha miradi 1423, miradi 1268 ikiwa vijijini na 155 ikiwa maeneo ya mijini, miradi mingine zaidi ya 200 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji hivyo kuwataka wahitimu kuitazama miradi hiyo kama fursa ya kujiajiri kwa kuunda vikundi vya kusimamia na kuendesha miradi hiyo huku wakizikabili changamoto za maji mijini na vijijini.

ADVERTISEMENT

 

Katika hatua nyingine Aweso amewataka wataalamu hao ambao wametunukiwa madaraja mbalimbali ya kitaaluma kuwa tayari kufanya kazi mahali popote nchini tena kwa kujitoa, kufanyakazi kwa bidii, uweledi, uadilifu na uaminifu wakati wanapozitatua changamoto zinazohusiana na maji kote nchini.

ADVERTISEMENT
Ombeni Osward

Ombeni Osward

Related Posts

Zaidi ya Bilioni 800 kutumika ujenzi wa miundombinu ya maji nchini.
HABARI

Zaidi ya Bilioni 800 kutumika ujenzi wa miundombinu ya maji nchini.

by Ombeni Osward
Jan 20, 2021
0

Zaidi ya tsh.Bilioni 800 zitatumika katika kuboresha...

Read more
Bweni lililochomwa moto 2018 laungua tena,kura zapigwa kubaini mhusika

Bweni lililochomwa moto 2018 laungua tena,kura zapigwa kubaini mhusika

Jan 20, 2021
Dkt. Gwajima Akemea vikali Ubadhirifu wa Dawa

Vituo vya afya vyatakiwa kuwa na mkataba wa huduma Kwa wateja

Jan 20, 2021
Nyaraka za Serikali kuandikwa kwa Kiswahili

Nyaraka za Serikali kuandikwa kwa Kiswahili

Jan 20, 2021
Rais Magufuli ashuhudia utiaji saini mkataba wa uchimbaji wa madini ya Nickel

Rais Magufuli ashuhudia utiaji saini mkataba wa uchimbaji wa madini ya Nickel

Jan 19, 2021
Kijana amuua babu yake kumnusuru na mateso

Kijana amuua babu yake kumnusuru na mateso

Jan 19, 2021
Next Post
Nilijaribu Kumsaidia Özil Kadri ya uwezo wangu – Arteta

Nilijaribu Kumsaidia Özil Kadri ya uwezo wangu - Arteta

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

I agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.

Currently Playing

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

January 2021
M T W T F S S
« Dec    
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In