ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, July 3, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

BENKI YA CRDB YAHITIMISHA MASHINDANO YA “CRDB BANK SUPER CUP” 2021 KWA KISHINDO JIJINI ARUSHA

I am Krantz by I am Krantz
Dec 14, 2021
in HABARI
0
BENKI YA CRDB YAHITIMISHA MASHINDANO YA “CRDB BANK SUPER CUP” 2021 KWA KISHINDO JIJINI ARUSHA
0
SHARES
176
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 Mashindano ya CRDB Bank Super Cup 2021 yaliyoshirikisha timu za wafanyakazi wa Idara na Matawi ya Benki ya CRDB nchi nzima, Tanzania Bara na Visiwani, yamehitimishwa leo jijini Arusha ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela. CRDB Bank Super Cup mwaka huu ilihusisha michezo ya mpira wa miguu kwa wanaume na mpira wa pete kwa wafanyakazi wanawake.

Kwa upande wa mpira wa miguu mashindano hayo yalishirikisha timu 16 za mpira wa miguu, kati ya hizo 8 ziliundwa kwa kushirikisha vitengo mbalimbali vilivyopo Makao Makuu ya Benki hiyo, na 8 zingine ziliundwa kutoka katika kanda mbalimbali ambazo zilitokana na Matawi yote ya Benki ya CRDB Tanzania nzima.

RelatedPosts

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO

𝐖𝐀𝐙𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 WA ZANZIBAR 𝐀𝐈𝐏𝐀 𝐊𝐎𝐍𝐆𝐎𝐋𝐄 𝐀𝐊𝐈𝐁𝐀 𝐂𝐎𝐌𝐄𝐑𝐂𝐈𝐀𝐋 𝐁𝐀𝐍𝐊

Jul 3, 2022

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO

Jul 3, 2022

BENKI YA CRDB NA WAKALA WA SERIKALI MTANDAO ZANZIBARA WAINGIA MAKUBALIANO

Jul 3, 2022
Load More

Kwa upande wa wanawake timu 8 ziliundwa na kushiriki katika mchezo wa mpira wa pete zikijumuisha timu kutoka Makao Makuu na matawi. Timu zote zilipewa majina yatokanayo na bidha mbali mbali zinazotolewa na Benki hiyoikiwamo, timu za SimBanking, Tanzanite, Hodari, TemboCard, Nia Moja, Ulipo Tupo, nk.

Akizungumza malengo ya kuanzisha mashindano hayo ya “CRDB Bank Super Cup,” Mkurugenzi Mtendaji wa wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema, dhumuni kubwa la kuanzisha mashindano hayo ikiwa ni pamoja na burudani na kujenga afya ya mwili na akili kwa wafanyakazi, kuimarisha mahusiano baina ya wafanyakazi, pamoja na kuongeza uzalishaji kazini.

“Tunaamini mashindano haya ni hatua muhimu katika kufikia azma ya kuimarisha afya za wafanyakazi pamoja na kuongeza mshikamano na ushirikiano katika kutekeleza majukumu ya kikazi ili kutoa huduma bora kwa wateja wao. Leo Tunahitimisha mashindano haya kwa mafanikio makubwa ikiwa ni mara ya kwanza mashindano haya kufanyika katika historia ya Benki yetu”. amesema Nsekela.

Hitimisho la mashindano hayo liliambatana na utoaji wa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu na makombe kwa washindi mmoja mmoja na timu kwa ujumla. Mshindi wa kwanza alijinyakulia Shilingi Milioni 5 kwa mpira wa miguu na Shilingi Milioni 3 kwa mpira wa pete. Benki hiyo pia ilitoa zawadi kwa wachezaji binafsi waliofanya vizuri, ambapo mchezaji bora (Best Player) na mfungaji bora (Top Scorer) walipata Shilingi laki 2, na Shilingi laki 3 ilienda kwa mchezaji bora wa mechi ya fainali.

Nsekela aliwapongeza wafanyakazi wa Benki hiyo kwa kuitikia wito na kufanikisha mashindano hayo yaliyofana sana na kuleta upinzani baina ya timu shiriki hivyo kuleta chachu ya ubora wa ligi hiyo ya CRDB Bank Super Cup. “Huu ni mwanzo, mwaka ujao tutahakikisha tunayaboresha zaidi mashindano haya ikiwa pamoja na kuongeza timu za mpira wa kikapu katika ligi hii na kuongeza zawadi kubwa zaidi za washidi ili kuleta chachu za ushindani,” aliongezea Nsekela.

ADVERTISEMENT

Naye Mkurugenzi wa Rasiliamali watu, Siophoro Kishimbo aliwashukuru Wakurugenzi wa Idara, Mameneja wa Kanda na Matawi wa Benki hiyo kwa kutoa ushirikiano wa kutosha na kuwapa wafanyakazi wao ruhusa ya kushiriki katika mashindano hayo. Alisema mashindano hayo yameleta chachu kubwa katika Benki na kuwapa fursa wafanyakazi weke kuonyesha vipaji walivyonavyo.

Benki ya CRDB imekuwa kwa kipindi kirefu ikiipa michezo umuhimu mkubwa hivyo kufikia kuendesha programu mbalimbali za michezo ikiwamo CRDB Bank Bonanza lilnalojumuisha timu za wabunge na wizara, CRDB Bank Marathon ambayo mwaka huu imepata usajili wa kimataifa, pamoja na mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu “CRDB Bank Taifa Cup” ambayo yalifanyanyika mwezi Novemba mwaka huu yakishirikisha timu za kikapu za mikoa.

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO
BIASHARA

𝐖𝐀𝐙𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 WA ZANZIBAR 𝐀𝐈𝐏𝐀 𝐊𝐎𝐍𝐆𝐎𝐋𝐄 𝐀𝐊𝐈𝐁𝐀 𝐂𝐎𝐌𝐄𝐑𝐂𝐈𝐀𝐋 𝐁𝐀𝐍𝐊

by I am Krantz
Jul 3, 2022
NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO
BIASHARA

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO

by I am Krantz
Jul 3, 2022
BENKI YA CRDB KATIKA MAONESHO YA 46 YA SABASABA
BIASHARA

BENKI YA CRDB KATIKA MAONESHO YA 46 YA SABASABA

by I am Krantz
Jul 3, 2022
WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI
HABARI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
NEYMAR KUONDOKA PSG
HABARI

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.
BIASHARA

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

by I am Krantz
Jul 2, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
December 2021
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  
« Oct   Jan »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In