ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Monday, March 20, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NMB, Jubilee Life wazindua mpango wa uwekezaji, utunzaji na bima

I am Krantz by I am Krantz
Dec 21, 2021
in HABARI
0
NMB, Jubilee Life wazindua mpango wa uwekezaji, utunzaji na bima
0
SHARES
175
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Jubilee Life Insurance, Karim Jamal wakitiliana saini ya ushirikiano wa kuzindua mpango wa Bima kwa ajili ya watu wa kipato cha kati na wafanyabiashara nchini uitwao, NMB FANAKA PLAN uliofanyika Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Mkuu wa Idara ya Bima NMB, Martine Massawe na Mkuu wa Idara ya Bima kwa Mabenki wa Jubilee Life Insurance, Dereck Rwezaura.

RelatedPosts

RJ THE DJ VIFO VINAONGEZA MSONGO WA MAWAZO

ROMY JONS AOMBA MSAMAHA

Mar 20, 2023

MCHUNGAJI AFUNGA KANISA KISA ASHINDA MIL 100 ZA “KUBETI”

Mar 20, 2023

WAZIRI BITEKO ATAKA BAJETI YA 2023/24 KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA

Mar 20, 2023
Load More

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Jubilee Life Insurance, Karim Jamal wakibadilishana nyaraka baada ya kutiliana saini makubaliano hayo.


Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (wa pili kulia) na Mkurugenzi wa Jubilee Life Insurance, Karim Jamal wakionyesha nyaraka walizotia saini.

NA MWANDISHI WETU

BENKI ya NMB kwa kushirikiana na Jubilee Life Insurance, imezindua mpango wa utunzaji, uwekezaji na bima uitwao ‘Fanaka Plan,’ ambao licha ya kulinda maisha ya mteja aliyedhurika, pia unampa faida tele na uhuru wa kutunza fedha kwa utaratibu na muda atakaochagua.

Uzinduzi wa Fanaka Plan umefanyika jijini Dar es Salaam leo, ambako Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi na Mkurugenzi Mkuu wa Jubilee Life Insurance, Karim Jamal, walitiliana saini na kuutaja mpango huo kuwa ni kwa Watanzania wote – wenye akaunti NMB na wasio nazo.

Akizungumza kabla ya kuzindua mpango huo, Mponzi alisema Fanaka Plan ni mshirika sahihi wa watu wenye malengo ya muda mrefu na ya kati katika kujiimarisha kiuchumi na kufikia malengo binafsi, uwekezaji ukiwa ni wa kati ya miaka mitano hadi 20.

“Fanaka Plan” Ni uwekezaji ambao unakuwa na bima ya maisha kwa mteja. Hii inawawezesha Watanzania kuweka akiba kila mwezi katika vifurushi mbalimbali, ambavyo vinatoa faida kuanzia Sh. Mil. 5 na kuendelea, huku mteja akitakiwa kuchagua kifurushi ama ‘Plan’ kulingana na uwezo wake wa kuchangia kila mwezi.

“Hii maana yake utakuwa unajiwekea akiba, pesa yako itakupa bonasi na ikitokea mteja akapata ulemavu wa kudumu kabla ya wakati aliopanga, NMB na Jubilee Life tutalipa mchango wa miezi 36 (miaka mitatu), hata kama mteja alilipia miezi miwili tu na ikitokea akafariki, atalipwa bima kamili sawa na kifurushi alichochagua,” alisisitiza Mponzi.

Alibainisha kuwa, licha ya faida hizo kwa watakaopata ulemavu wa kudumu ama kifo wakiwa kwenye Fanaka Plan, mteja atakayemaliza muda aliochagua bila kupata ulemavu ama kifo, atalipwa kifurushi chake chote na atakuwa na bima ya maisha hadi atakapofikisha umri wa miaka 90 bila kuchangia kiasi kingine.

Aliwataka Watanzania kufika kwenye matawi ya NMB kote nchini, ili waweze kupata maelekezo muhimu ya namna ya kujiunga na Fanaka Plan, ambao aliutaja Kama mpango uliobeba Suluhu za changamoto zitokanazo na ukosefu wa uhakika wa kipato, lakini pia ukijihakikishia mwekezaji mnyororo sahihi wa mtiririko wa fedha.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Jubilee Life, Karim Jamal, alikiri kuwa wanajivunia aina ya ushirikiano uliozaa Fanaka Plan, ambao unazihusisha taasisi vinara – Kampuni yake ikiongoza miongoni mwa Kampuni za Bima Afrika Mashariki na NMB ambayo ni benki Bora na kinara wa taasisi za fedha Tanzania.

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

“Tunaishukuru NMB kwa aina hii ya ushirikiano chanya unaowahakikishia wateja usalama wa fedha na maisha yao, ushirikiano uliobeba tija na matarajio ya kesho iliyo njema kwa watoto na familia ya mteja iwapo atapata ulemavu ama kifo wakati akiwa ameshaanza kuwa mwekezaji kupitia Fanaka Plan,” alisema Jamal.

Jamal aliitaja Fanaka Plan kuwa ni mpango mzuri na wa aina yake, na kwamba kuenea kwa matawi ya NMB kote nchini na uzoefu mkubwa walionao wao katika nyanja ya Bima, unawapa Watanzania kimbilio sahihi lenye kila aina ya faida kwa vifurushi vyote na kwamba hakutakuwa na changamoto yoyote katika kupata huduma hiyo.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

RJ THE DJ VIFO VINAONGEZA MSONGO WA MAWAZO
HABARI

ROMY JONS AOMBA MSAMAHA

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
MCHUNGAJI AFUNGA KANISA KISA ASHINDA MIL 100 ZA “KUBETI”
HABARI

MCHUNGAJI AFUNGA KANISA KISA ASHINDA MIL 100 ZA “KUBETI”

by ALFRED MTEWELE
Mar 20, 2023
WAZIRI BITEKO ATAKA BAJETI YA 2023/24 KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA
HABARI

WAZIRI BITEKO ATAKA BAJETI YA 2023/24 KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
TMA YATOA TAHADHARI MVUA KUBWA MIKOA HII KUANZIA LEO NA KESHO
HABARI

TMA YATOA TAHADHARI MVUA KUBWA MIKOA HII KUANZIA LEO NA KESHO

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023
WATU 5 WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA WIZI MAFUTA SGR
HABARI

WATU 5 WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA WIZI MAFUTA SGR

by ALFRED MTEWELE
Mar 20, 2023
MARUFUKU KUTOA FEDHA UPATE DHAMANA POLISI
HABARI

MARUFUKU KUTOA FEDHA UPATE DHAMANA POLISI

by Shabani Rapwi
Mar 20, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
December 2021
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  
« Oct   Jan »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In