ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Wednesday, July 6, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

PROF. Mkumbo Azindua Benki Ya WHA Microfinance

ADAM CHAUYA by ADAM CHAUYA
Dec 5, 2021
in HABARI
0
PROF. Mkumbo Azindua Benki Ya WHA Microfinance
0
SHARES
156
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara  Pof. Kitila Mkumbo (katikati) akipiga makofi mara baada ya kuizindua benki ya WHA Microfinance, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kikundi cha kikoba cha Women Of Hope Alive, Janeth Mahawanga ambaye pia ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Dar es Salaam kupitia CCM. Tukio hilo lilifanyaka jana Disemba 04, 2021 katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo amezindua benki ya wajasiriamali wanawake inayo milikiwa na kikundi cha kikoba cha Women of Hope Alive.

Uzinduzi huo umefanyika jana Disemba 04,2021 katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, wakati wa kongamano la Mwanamke na Kikoba 2021 lililoandaliwa na kikundi hicho.

RelatedPosts

Vodacom Na d.light Kutoa Simu Janja Kwa Mkopo

Vodacom Na d.light Kutoa Simu Janja Kwa Mkopo

Dec 14, 2021
Load More

Wakati wa uzinduzi wa benki hiyo ijulikanayo kama ‘Women of Hope Alive Microfinance bank’, Prof. Mkumbo amesema kupitia benki hiyo wanawake wataweza kunufaika kwa kupata mikopo itakayosaidia kukuza vipato vyao na taifa kwa ujumla.

“Tunatambua katika tafiti kwamba wanawake wakifanikiwa katika biashara huwa 90% ya mapato yanainufaisha familia, na ukikopesha wanawake na wanaume, wanawake ni waaminifu zaidi hivyo basi benki kopesheni wanawake maana pesa zenu zitawahi kurudi”, amesema Prof. Mkumbo.

Kadhalika Prof. Mkumbo amekihakikishia kikundi hicho kuwa serikali itawaunga mkono katika utoaji wa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanawake bila malipo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi hicho ambaye pia ni Mbunge wa viti maalum (CCM) mkoa wa Dar es Salaam, Janeth Mahawanga, amesema benki hiyo itakuwa ikitoa mikopo kwaajili ya wanawake wajasiriamali, ikiwa ni jitihada za kuiunga mkono serikali katika kuwainua wanawake kiuchumi.

ADVERTISEMENT

“Benki ya Women of Hope Alive Microfinance itajikita zaidi katika kuweka na kutoa fedha pamoja na kutoa mikopo kwa wanawake wajasiriamali ndani na nje ya kikundi chetu na lengo ni kuiunga mkono serikali katika kumuinua mwanamke”, amesema Mahawanga.

Mwenyekiti wa Kikundi cha kikoba cha Women Of Hope Alive, Janeth Mahawanga akihojiwa na waandishi wa habari kuhusu Kongamano la Mwanamke na Kikoba 2021 lililofanyika jana Disemba 04, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Dar es Salaam. Kongamano hili linafanyika kila mwaka na hii ni kwa mara ya tatu ambapo huwakutanisha wanawake wajasiriamali na kuwapa elimu ya ujasiriamali.

Mahawanga ameongeza kuwa kikundi hicho kwasasa kitahakikisha kinawafikia wanawake wote katika jiji la Dar es Salaam lengo ikiwa ni kuwawezesha na kuwainua kiuchumi.

Kadhalika katika risala iliyosomwa na katibu wa kikundi, Saumu Mbwana, Benki ya WHA Microfinance itawafikia wanawake huku wakiamini kuwa benki hiyo itakuwa chachu ya maendeleo kwa wanawake nchini.

“Benki hii itakuwa msaada kwaakina mama, watapata mikopo na kulipa kodi kwaajili ya maendeleo ya nchi yetu” amesema Mbwana.

Kongamano hilo ambalo hufanyika kila mwaka na  ni la tatu kwa mwaka huu, limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mary Masanja, Naibu Waziri wa Wizara ya Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi pamoja na mkuu wa wilaya ya Ubungo, Kheri James.

 

ADVERTISEMENT

Related

Tags: HABARI ZA UCHUMI
ADVERTISEMENT
ADAM CHAUYA

ADAM CHAUYA

Related Posts

HABARI

by Pastory Kimaryo
Jul 6, 2022
HABARI

by Pastory Kimaryo
Jul 6, 2022
WIVU WA MAPENZI CHANZO CHA MAUAJI KIGOMA
HABARI

WIVU WA MAPENZI CHANZO CHA MAUAJI KIGOMA

by Shabani Rapwi
Jul 6, 2022
RIHANNA BILIONEA WA KIKE MDOGO ZAIDI
HABARI

RIHANNA BILIONEA WA KIKE MDOGO ZAIDI

by Shabani Rapwi
Jul 6, 2022
KISWAHILI LUGHA RASMI UGANDA
HABARI

KISWAHILI LUGHA RASMI UGANDA

by Shabani Rapwi
Jul 6, 2022
RICHARLISON AFUNGIWA NA KUPIGWA FAINI
HABARI

RICHARLISON AFUNGIWA NA KUPIGWA FAINI

by Shabani Rapwi
Jul 6, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
December 2021
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  
« Oct   Jan »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In