ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, July 3, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

Zantel yazindua duka jipya lililopo Michenzani Mall-Unguja

I am Krantz by I am Krantz
Dec 4, 2021
in HABARI
0
Zantel yazindua duka jipya lililopo Michenzani Mall-Unguja
0
SHARES
214
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

ADVERTISEMENT

Mkuu wa Wilaya ya Mjini-Unguja, Rashid Msaraka akikata utepe kuzindua duka jipya la Zantel lililopo eneo la biashara la Michenzani Mall.Kulia ni Mkuu wa Zantel-Zanzibar Mohammed Khamis Mussa na Emmanuel Joshua, Mkuu wa Mauzo, Usambazaji na Huduma kwa wateja.Duka hilo ni la tatu kwa Unguja na la tano kwa Zanzibar litakalosaidia kusogeza huduma karibu na wateja.

Mkuu wa Wilaya aipongeza kwa kuboresha huduma za Mawasiliano
Unguja.2 Desemba 2021.Katika kuhakikisha wateja wanapata huduma kwa urahisi, Kampuni ya Zantel imezindua duka jipya la huduma kwa wateja lililopo michenzania Mall mjini unguja.
Uzinduzi wa duka hilo ulifanyika jana na Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashid Msaraka na kushuhudiwa na wadau mbalimbali.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mkuu wa Zantel-Zanzibar Mohammed Khamis Mussa alisema duka hilo litasaidia kuongeza huduma za mawasiliano karibu na wateja kwani duka hilo lipo katikati ya mji.
“Duka hili litakuwa msaada mkubwa katika kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa wateja wetu hapa Unguja.Eneo hili la Michenzani ni rahisi zaidi kufikika kwa wateja wote wa maeneo ya karibu na wanaotembelea eneo hili,” alisema Mussa.
Duka hilo ni la tatu kwa Unguja ambapo mawili yapo maeneo ya Vuga na Mlandege.Pia, duka hilo ni la tano kwa Zanzibar ambapo mawili mengine yapo Pemba katika eneo la Chake na Wete.
Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Rashid Msaraka aliipongeza Zantel kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inaboresha huduma za mawasiliano visiwani Zanzibar.
“Huduma za Mawasiliano ni kiungo muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi yetu.Zantel imekuwa mfano bora katika kuboresha huduma za mawasiliano kwa kujenga miundombinu kama minara pamoja na maduka kama hili tunalozindua leo,” alisema
Zantel imekuwa ikifanya uwekezaji mkubwa katika kujenga miundimbinu mipya na kuboresha iliyopo ili kuhakikisha Zanzibar yote inakuwa na Mawasiliano ya uhakika.

RelatedPosts

No Content Available
Load More

Hadi mwaka huu, zaidi ya asilimia 65 ya Zanzibar ilikuwa imeunganishwa na mtandao wa 4G jambo linalotoa fursa kwa wananchi kupata na kuzitumia fursa za kiuchumi na kijamii kwenye ulimwengu wa kidigitali.
Hivi karibuni, Kampuni hiyo imekuwa ikiendesha kampeni ijulikanayo kama Pasua Anga Ki Zantel 4G ambayo ililenga kuelimisha umma juu ya umuhimu wa mtandao wa 4G kwa manufaa ya kijamii na kiuchumi.
“Tumeona mabadiliko chanya kupitia kampeni hii, ambapo tumeona watu wakianza kutumia mtandao kwa manufaa yao.Wapo waliofungua biashara mitandaoni na kuongeza ubunifu kwenye kazi zao kwa kutumia intaneti,” alisema Mussa.
Huduma zitakazopatikana kwenye duka hilo ni pamoja na usajili wa namba za simu, bidhaa za simu kamavile Smarta, huduma za 4G pamoja na huduma ya kifedha ya Ezypesa.
Uzinduzi wa duka hilo umekuja mara tu baada ya kufunguliwa kwa maduka (mall) ikiwa ni fursa kwa kampuni mbalimbali kusogeza huduma karibu na wateja wao.

ADVERTISEMENT

Related

Tags: ZANTEL
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO
BIASHARA

𝐖𝐀𝐙𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀 WA ZANZIBAR 𝐀𝐈𝐏𝐀 𝐊𝐎𝐍𝐆𝐎𝐋𝐄 𝐀𝐊𝐈𝐁𝐀 𝐂𝐎𝐌𝐄𝐑𝐂𝐈𝐀𝐋 𝐁𝐀𝐍𝐊

by I am Krantz
Jul 3, 2022
NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO
BIASHARA

NSSF YAWAHIMIZA WAJASIRIAMALI KUCHANGAMKIA FURSA KWA KUJIUNGA NA MFUKO HUO

by I am Krantz
Jul 3, 2022
BENKI YA CRDB KATIKA MAONESHO YA 46 YA SABASABA
BIASHARA

BENKI YA CRDB KATIKA MAONESHO YA 46 YA SABASABA

by I am Krantz
Jul 3, 2022
WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI
HABARI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
NEYMAR KUONDOKA PSG
HABARI

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.
BIASHARA

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

by I am Krantz
Jul 2, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
December 2021
M T W T F S S
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031  
« Oct   Jan »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In