TUNATAKA TTCL IWE KITOVU CHA MAWASILIANO AFRIKA MASHARIKI – WAZIRI NAPE NNAUYE – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, May 19, 2022
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

TUNATAKA TTCL IWE KITOVU CHA MAWASILIANO AFRIKA MASHARIKI – WAZIRI NAPE NNAUYE

I am Krantz by I am Krantz
Jan 28, 2022
in HABARI
0
TUNATAKA TTCL IWE KITOVU CHA MAWASILIANO AFRIKA MASHARIKI – WAZIRI NAPE NNAUYE
0
SHARES
99
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye (katikati) akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kufanya ziara yake ndani ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL – Corporation). Kulia ni Mjumbe wa Bodi ya TTCL, Bw. Rajabu Uweje Yacoub pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL – Corporation, Bw. Waziri W. Kindamba wakifuatilia mkutano huo.


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye (katikati) akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kufanya ziara yake ndani ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL – Corporation). Kulia ni Mjumbe wa Bodi ya TTCL, Bw. Rajabu Uweje Yacoub pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TTCL – Corporation, Bw. Waziri W. Kindamba wakifuatilia mkutano huo.


RelatedPosts

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022
Load More

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nape Nnauye amefanya ziara ndani ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL – Corporation) na kubainisha kuwa lengo la wizara yake ni kuifanya taasisi hiyo kuwa kitovu cha mawasiliano kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Waziri Nnauye amebainisha hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kutembelea TTCL – Corporation na kuzungumza na menejimenti ya shirika pamoja na kupokea taarifa na changamoto zinazolikabili shirika.

“Tageti yetu ni kuifanya TTCL – Corporation kuwa shirika bora la mawasiliano kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tunataka tutafute njia ya pamoja ya kuliboresha shirika hili,” alisema Waziri huyo wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Nnauye akizungumza na wanahabari.

ADVERTISEMENT

Alisema katika ziara hiyo aliyoiita ya kujifunza wamepokea taarifa ambapo, yapo mambo yaliyowasilishwa kama changamoto ambayo yanakwamisha shirika hilo kufanya vizuri zaidi, hivyo kama wizara inayoisimamia inakwenda kukaa na kuyachakata kabla ya kuyatolea maelekezo.

“Tumeyapokea na tunaenda kukaa na kuyachakata, yanayopaswa kufikishwa mamlaka za juu tutayawasilisha na yaliyochini yetu tunaenda kuyafanyia kazi kisha baadaye tutatoa maelekezo  yetu ili kusonga mbele,” alifafanua waziri huyo.

“…Alitolea mfano kuwa zipo sheria za manunuzi ya umma ambazo TTCL imekuwa ikilazimika kuzifuata mchakato wake unaweza kuchukua hadi miezi sita, wakati sekta binafsi ambao ni washindani wa TTCL unaweza hata kuchukua siku mbili…sasa ukimwacha hapo kushindana na wenzake lazima ataachwa mbali,” alisema Waziri Nnauye.

Aidha akifafanua zaidi alisema yapo baadhi ya mambo ya kimaamuzi ambayo TTCL haiwezi kufanya pekee hadi kushirikisha ngazi nyingine, jambo ambalo limekuwa kama changamoto kwenye shirika na kukwamisha baadhi ya mipango ya maendeleo ya shirika.

Aliongeza kuwa wamejipanga kukutana pia na wafanyakazi wa TTCL na kuzungumza nao ili kupata maoni na changamoto zao na kuangalia namna bora ya kushirikiana kuhakikisha shirika linasonga mbele kwa mafanikio zaidi. 

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA
BIASHARA

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU
HABARI

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

by I am Krantz
May 19, 2022
“PANYA ROAD” KAENI CHONJO SERIKALI IPO KAZINI
HABARI

“PANYA ROAD” KAENI CHONJO SERIKALI IPO KAZINI

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
RAIS SAMIA AMETOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU-MAJALIWA
HABARI

RAIS SAMIA AMETOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU-MAJALIWA

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
WATEJA WA HALOTEL KUJIPATIA ZAWADI KUPITIA MATUMIZI YA MTANDAO
BIASHARA

WATEJA WA HALOTEL KUJIPATIA ZAWADI KUPITIA MATUMIZI YA MTANDAO

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 19, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

January 2022
M T W T F S S
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
31  
« Dec   Feb »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In