Deni la Serikali Laongezeka Kwa Asilimia 13.7 – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, May 19, 2022
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Deni la Serikali Laongezeka Kwa Asilimia 13.7

I am Krantz by I am Krantz
Mar 31, 2022
in HABARI
0
Deni la Serikali Laongezeka Kwa Asilimia 13.7
0
SHARES
29
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Dodoma. Deni la Serikali Tanzania limeongezeka kutoka Sh56.76 trilioni mwaka uliopita hadi kufikia Sh64.52 trilioni kufikia Juni 30, 2021.

Hayo yamesemwa leo Jumatano Machi 30, 2021 na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere wakati akiwasilisha ripoti ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30, 2021 kwa Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu Chamwino.

RelatedPosts

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022
Load More

Kichere amesema hivyo kuna ongezeko la Sh7.76 trilioni sawa na asilimia 13.7.

Hata hivyo, amesema kipimo cha deni la Serikali kinachotumia pato la Taifa, kinaonyesha deni hili bado himilivu.

Aidha, Kichere amesema miradi ya kujenga na kuboresha viwanja vya ndege 12 yenye thamani ya Sh1.02 trilioni iliyotekelezwa katika kipindi cha kati ya mwaka 2016/17 hadi 2020 2021 ilikaguliwa.

Amesema ukaguzi ulibaini kuwa kuna mwingiliano wa mamlaka na majukumu ya uendelezaji wa viwanja vya ndege mwingiliano Tanroad na TAA unaosababisha mapungufu na uwajibikaji katika utekelezaji wa miradi hiyo.

ADVERTISEMENT

“Ukaguzi ulibaini kuna mwingiliano wa mamlaka na majukumu ya uendelezaji wa viwanja kati ya Tanroads (Wakala wa Barabara Nchini) na TAA (Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini) unaosababisha mapungufu ya uwajibikaji na utekelezaji wa bajeti,” amesema.

Pia Kichere amesema wamebaini kuna ongezeko la gharama ya Sh22.35 bilioni kutokana na kutolipa fidia kaya 1,125 katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere kwa zaidi ya miaka 23.

Amesema kuna watu wanatakiwa kulipwa fidia lakini kuna taratibu hazijakamilika kwa hiyo tangu mwaka 1997 na kwamba tathmini inaonyesha deni linaongezeka kutoka Sh7bilioni na hivyo Sh29 bilioni.

Hali kadhalika CAG, amesema wamebaini ucheleweshaji wa malipo ya wakandarasi iliyosababisha tozo za riba ya Sh14.14 bilioni, ambapo Sh11.39 bilioni za Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere na Sh2.75bilioni za Kiwanja cha Ndege cha Mwanza.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA
BIASHARA

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU
HABARI

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

by I am Krantz
May 19, 2022
“PANYA ROAD” KAENI CHONJO SERIKALI IPO KAZINI
HABARI

“PANYA ROAD” KAENI CHONJO SERIKALI IPO KAZINI

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
RAIS SAMIA AMETOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU-MAJALIWA
HABARI

RAIS SAMIA AMETOA KIPAUMBELE CHA AJIRA KWA WENYE ULEMAVU-MAJALIWA

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
WATEJA WA HALOTEL KUJIPATIA ZAWADI KUPITIA MATUMIZI YA MTANDAO
BIASHARA

WATEJA WA HALOTEL KUJIPATIA ZAWADI KUPITIA MATUMIZI YA MTANDAO

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 19, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In