ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Ishu ya Mkataba, MANULA Avunja Ukimya, Awatega Mabosi Simba

I am Krantz by I am Krantz
Mar 30, 2022
in MICHEZO
0
Ishu ya Mkataba, MANULA Avunja Ukimya, Awatega Mabosi Simba
0
SHARES
62
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

MABOSI wa Simba wanahaha kufanya mazungumzo na baadhi ya wachezaji ambao mikataba yao ipo ukingoni, huku Aish Manula akiwa miongoni mwa wachezaji hao na kipa huyo amevunja ukimya kuzungumza dili lake la kubaki Msimbazi.

Manula ambaye kiwango chake kimezidi kupanda tangu atue Simba akitokea Azam FC, amezungumza na Mwanaspoti na kuelezea hatma ya mkataba wake ndani ya klabu hiyo na kuanika uamuzi wake mpya.

RelatedPosts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

May 21, 2022

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

May 21, 2022

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

May 21, 2022
Load More

Manula alisema hawezi kufanya uamuzi wowote kwa sasa, kwani bado ni muajiriwa wa Simba ambayo imekuwa ikimpatia kila kitu ndani ya mkataba wake.

ADVERTISEMENT

Alisema anafahamu mwisho wa msimu huu anamaliza mkataba na klabu hiyo, ila amewaeleza viongozi wake hatafanya uamuzi mwengine wowote kwani wao ndio anawapa nafasi ya kwanza.

“Naonekana bora zaidi wakati huu kutokana na kupata nafasi kubwa ya kuaminiwa hapa Simba kutokana na mashindano mbalimbali tunayocheza, hivyo kabla ya kuamua chochote juu ya mkataba wangu mpya Simba nimewapa nafasi ya kwanza,” alisema Manula na kuongeza;

“Katika kuhakikisha nakubaliana na Simba nimefanya nao mazungumzo ya kuongeza mkataba mpya na kuna mahitaji nimewaeleza na tumaini langu yataenda sawa na nitaongeza mwingine mpya hapa.”

Manula alifafanua; “Hili jambo la kuja kuongea kabla ya mkataba wangu kufikia mwisho ni heshima kubwa wamenipatia ninaimani kubwa kila kitu kitakwenda vizuri nitakuwa hapa kwa misimu mingine ijayo.

“Sioni nafasi ya Simba kushindwa kuniongezea mkataba mpya kwani wanafanya mambo yao kwa weledi mkubwa ila kama ikitokea hivyo ndio nitafanya uamuzi mwingine ambao kwa sasa sijajipanga nao na sitarajii kama itakuwa hivyo.”

Awali Manula alisaini mkataba wa miaka mitatu uliokuwa na thamani isiyopungua Sh 90 milioni, ikiwa na maana mabosi wa Simba kwa mkataba mpya wanalazimika kutoa mkwanja mrefu zaidi ya huo ili kufanikisha kumbakisha klabuni.

Inelezwa mabosi wa Simba wanapambana kumalizana na Manula kutokana na presha kubwa wanayopata baada ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini kuelezwa inamnyatia kipa huyo aliyeokoa penalti mbili dhidi ya Asec Mimosas katika mechi ya Kundi D ya Kombe la Shirikisho Afrika nchini Benin.

HUYU HAPA TRY AGAIN

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema watambakisha Manula kwa namna yoyote kwani mazungumzo yanaenda vyema na hawajapokea ofa yoyote mezani ya kutakiwa kwake.

Mbali na Manula, wachezaji wengine ambao mikataba yao inamalizika mwisho wa msimu ni; Chriss Mugalu, Meddie Kagere, Hassan Dilunga, Mzamiru Yassin, Joash Onyango, Bernard Morrison na wengineo.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL
HABARI

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI
HABARI

NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI

by Ally Hamis Zingizi
May 14, 2022
Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa
HABARI

Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa

by I am Krantz
Apr 29, 2022
Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”
BURUDANI

Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”

by I am Krantz
Apr 27, 2022
AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE
BURUDANI

AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022
Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)
BIASHARA

Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In