Licha ya Mabomu Kurindima …Viongozi Watatu wa Ulaya Wafanya ziara Ukraine – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Monday, May 16, 2022
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

Licha ya Mabomu Kurindima …Viongozi Watatu wa Ulaya Wafanya ziara Ukraine

I am Krantz by I am Krantz
Mar 16, 2022
in HABARI
0
Licha ya Mabomu Kurindima …Viongozi Watatu wa Ulaya Wafanya ziara Ukraine
0
SHARES
70
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Viongozi watatu wa eneo la Ulaya Mashariki wamekutana na Rais wa Ukraine,Volodymyr Zelensky katika mji uliozingirwa wa Kyiv, katika kuonesha mshikamano wao huku mapigano yakiendelea.

Ukrainekrieg | Reise EU-Regierungschefs nach Kiew | Mateusz Morawiecki & Jaroslaw Kaczynski & Petr Fiala & Janez Jansa

RelatedPosts

WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUTANGAZA FURSA NA MATARAJIO YA MIPANGO YA SERIKALI- RC KUNENGE

WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUTANGAZA FURSA NA MATARAJIO YA MIPANGO YA SERIKALI- RC KUNENGE

May 16, 2022

WAZIRI MULAMULA ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO U.A.E

May 16, 2022

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI IBADA ABU DHABI FALME ZA KIARABU

May 16, 2022
Load More

Kutoka kushoto Waziri Mkuu wa Slovenia Janez Jansa, Waziri Mkuu wa Poland Mateusz Morawiecki na naibu wake Jaroslaw Kaczynski, na Waziri Mkuu wa Czech Petr Fiala, wakiangalia ramani ya Ukraine kabla ya kuondoka.

Viongozi hao watatu ni mawaziri wakuu wa Poland, Jamhuri ya Czech na Slovenia, walisafiri kwa kutumia treni hadi kuingia katika jiji hilo.Waziri Mkuu wa Poland, Mateusz Morawiecki alisambaza picha katika mitandao ya kijamii akiwa mjini Kyiv. Huku kukiwa na marufuku ya kutotoka nje mjini Kyiv, Rais Volodymyr Zelensky amekuwa mwenyeji wa mawaziri wakuu hao ikiwa ziara ya kwanza ya viongozi wa kigeni katika mji huo tangu uvamizi wa Urusi.

Katika eneo la kusini mwa Ukraine ofisi ya rais iliripoti mafanikio ya kibinadamu, baada ya wakazi wapatao 20,000 kuhama kutoka katika mji wa bandari uliozingirwa wa Mariupol ambako kuna ukosefu mkubwa wa chakula, maji na dawa.

Watoto 97 wauwawa tangu Urusi iingie Ukraine.

Ukraine-Konflikt | Präsident Selenskyj trifft sich mit drei EU-Regierungschefs in Kiew

Rais wa Ukraine akizungumza na viongozi wa Slovenia, Poland na Jamhuri ya Czech

Na katika hatua nyingine Zelensky amesema watoto 97 wameuwawa tangua majeshi ya Urusi yaingia katika ardhi ya nchi yake. Katika hotuba yake kwa bunge la Canada kiongozi huyo kwa mara nyingine ameitaka Canada ipanue wigo wa usaidizi wake kwa Ukraine.

Katika hotuba hiyo aliyoitoa kwa njia ya video Zelensky amelituhumu jeshi la Urusi kwa kuangamiza kila kitu nchini Ukraine kuanzia maeneo ya kihistoaria, shule, hospitali na makazi. Na kuongeza kusema si kwamba wanaomba sana lakini wanachokihitaji ni haki, uungwaji mkono wa kweli ambao utawawezesha kujitetea, kunusuru maisha yao.

Awali Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau alitangaza vikwazo dhidi ya maafisa 15 wa Urusi, wakiwemo wa serikala na maafisa wa kijeshi ambao wanatajwa kuhusishwa na vita ya sasa. Hatua hiyo inafanya idadi ya raia ya Belarus, Urusi na Ukraine kuwekewa vikwazo tangu kuanza kwa vita hivyo kufikia watu 500.

Urusi yatangaza kuanza mchakato wa kujiondoa katika Baraza la Ulaya

Wizara ya mambo ya nje ya Urusi imesema imeanza taratibu za kujiondoa katika Baraza la Ulaya katika kipindi hiki ambacho shinikizo limeongezeka la kutaka taifa hilo liondolewe kutoka kwa kundi la wapigania haki za watu wa Ulaya. Wizara hiyo imaendika katika ukurasa wake wa Telegram kwamba tayari imetoa taarifa kwa maandishi kwa Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Jenerali Marija Pejcinovic Buric.

Mapema Jumatatu Ukraine ilishinikiza Urusi ifukukwe haraka katika Baraza la Umoja wa Ulaya, ikisema haina haki ya kusalia kuwa mwanachama baada ya kuingiza majeshi katika taifa lake.

Urusi ilisimamishwa kutoka katika uwakilishi wake wote, siku moja baada ya kutuma vikosi vyane nchini Ukraine, Februari 24. Katika taarifa yake wizara ya mambo ya nje ya taifa hilo ilisema hatua hiyo ni ya kibaguzi na kuongeza kwamba taifa lao haliwezi kusalia katika Baraza la Ulaya.

Katibu Mkuu wa baraza hilo, Pejcinovic Buric mapema mwezi huu alililiambia shirika la habari la Ufaransa AFP kwamba sauti zaidi zinadai kwamba hatua inayofuata ni kufukuzwa kwa Urusi katika baraza hilo. Urusi ilijunga na Brazala la Ulaya mwaka 1996.

Related

I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUTANGAZA FURSA NA MATARAJIO YA MIPANGO YA SERIKALI- RC KUNENGE
HABARI

WAANDISHI WA HABARI TUMIENI KALAMU ZENU KUTANGAZA FURSA NA MATARAJIO YA MIPANGO YA SERIKALI- RC KUNENGE

by ALLY ZINGIZI
May 16, 2022
WAZIRI MULAMULA ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO U.A.E
HABARI

WAZIRI MULAMULA ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO U.A.E

by ALLY ZINGIZI
May 16, 2022
MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI IBADA ABU DHABI FALME ZA KIARABU
HABARI

MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI IBADA ABU DHABI FALME ZA KIARABU

by ALLY ZINGIZI
May 16, 2022
JOSE PESEIRO KOCHA MPYA WA NIGERIA
HABARI

JOSE PESEIRO KOCHA MPYA WA NIGERIA

by SHABANI RAPWI
May 16, 2022
SERIKALI YAZITAKA TAASISI KUWAJENGEA UWEZO WAKAGUZI WA NDANI
HABARI

SERIKALI YAZITAKA TAASISI KUWAJENGEA UWEZO WAKAGUZI WA NDANI

by I am Krantz
May 16, 2022
UKRAINE YATAKA KUUNGWA MKONO NA AFRIKA KATIKA VITA NA URUSI
HABARI

UKRAINE YATAKA KUUNGWA MKONO NA AFRIKA KATIKA VITA NA URUSI

by SHABANI RAPWI
May 16, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In