Uvamizi wa Rais wa Urusi Vladimir Putin nchini Ukraine umeingia wiki yake ya pili, huku msafara wa jeshi la Urusi ukiwa umbali mfupi kutoka mji mkuu wa Kyiv.
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, anaonekana hadi sasa kupambana na majeshi ya uvamizi. Lakini swali ni je, wanaweza kuendelea kupinga hadi lini?
Katika ufafanuzi huu tutaangalia makosa matatu yaliyofanywa na Zelensky, ambayo yalisababisha hali aliyonayo leo katika nchi yake ya Ukraine.
Kutarajia msaada kutoka mataifa ya Magharibi
Rais wa Ukraine alitarajia kuwa NATO itatoa usaidizi mkubwa kupamabana na uvamizi wa Urusi.
Ingawa NATO imeonyesha kuIunga mkono Ukraine lakini haijafikia matarajio.
Zelensky alisema mwaka 2021 kwamba anaamini Marekani, mshirika wa NATO, itairuhusu Ukraine kujiunga na jumuiya hiyo.
“Rais Biden amenihakikishia kwamba Ukraine haitaachwa peke yake,” alisema kuhusu imani yake kwa Marekani.
Aliongeza kusema kuwa Rais Biden anataka Ukraine kuwa mshirika wa Nato.
Vita ilipozuka Zelensky aliiomba NATO kufunga anga yake hadi Urusi ili taifa hilo lisiweze kufanya mashambulizi ya anga dhidi ya Ukraine.
Hilo halijafanywa na NATO hadi sasa haijakubali kutoa ndege za kivita kusaidia jeshi la Ukraine.
Urusi imetishia kwamba ikiwa itafunga anga yake kuelekea Ukraine au kusaidiwa na ndege za kivita, inaweza kumaanisha kuwa wahusika wake wamejiunga na vita.
Umuhimu wa Ukraine kwa Magharibi
Rais wa Ukraine amerudia kusisitiza umuhimu wa nchi yake kwa nchi za Magharibi, haswa kwa nchi za Ulaya.
Alielezea Ukraine kama “ngao ya Ulaya.”
Zelensky alisema vikosi vyake vimekuwa vikipambana na Urusi kwa miaka minane, akimaanisha vita vya kujitenga vyaa Urusi na mashariki mwa Ukraine.
“Kwa miaka minane, Ukraine imekuwa ngao. Wakati huo Ukraine imekuwa ikipinga mojawapo ya vikosi vyenye nguvu zaidi duniani. Hii ina maana kwamba iwapo mamlaka ya Ukraine hayatalindwa, hakutakuwa na usalama wa kudumu barani Ulaya,” alisema. . Zelensky.
Kutoelewa nia ya Putin
Wiki chache kabla ya uvamizi wa Urusi, rais wa Ukraine alisisitiza kwamba hakutakuwa na vita na kwamba Putin alitaka kuwatisha Kyiv ili kupata kile anachotaka.
Mnamo Januari 28, Zelensky aliviambia vyombo vya habari kuwa vinatia chumvi kuhusu hali ilivyo, na kwamba wanapaswa kuacha kukuza mambo.
“Hisia zinazotolewa na vyombo vya habari ni kwamba kutakuwa na vita kubwa na kwamba maandalizi makubwa ya kijeshi yanaendelea kwa sasa. Ni suala la vitisho na lisilo la lazima.”
Hakuna mtu ambaye angeweza kutabiri kwamba Putin angechukulia uvamizi huo kirahisi, kwani alikuwa ameonywa na viongozi wa Magharibi na kutishiwa kuwekewa vikwazo visivyo.
Zelensky haipatikani popote, na ana mambo mawili ya kuchagua: kuendelea na upinzani popote anapoenda, au kuruhusu Urusi kufanya kile anachotaka.
Kutuma barua ilikuwa ni hatua ya mwisho ilikuwa na ukomo wa kutoegemea upande wowote kwa Ukraine na kwamba nchi hiyo haiwezi kamwe kujiunga na Nato, lakini sasa inaonekana kwamba Moscow ina matakwa mengine, ikiwa ni pamoja na kwamba Kyiv inapaswa kuacha udhibiti wa mikoa ya Crimea na Donbas.