ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Miquissone Simba Tena?

I am Krantz by I am Krantz
Mar 25, 2022
in MICHEZO
0
Miquissone Simba Tena?
0
SHARES
53
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

KAMA ambavyo zilizuka tetesi za Clatous Chama kurejea Klabu ya Simba kutoka RS Berkane ya Morocco na baadaye ikawa kweli, sinema hiyo imeibuka tena, baada ya kiungo wa zamani wa timu hiyo anayeichezea Al Ahly ya Misri ambao ni Mabingwa wa Afrika, kudaiwa kutaka kurejea tena kwenye klabu hiyo.

Tetesi za Chama aliyeuzwa RS Berkane Agosti mwaka jana zilianza kama mzaha, lakini zilihitimishwa Desemba alipotangazwa kurejea akiwa ameitumikia timu hiyo kwa miezi minne tu.

RelatedPosts

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

May 22, 2022

19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

May 22, 2022

MANULA AKATWA NA KIOO

May 22, 2022
Load More

Klabu ya Al Ahly imetajwa kuwa inaweza kumtoa mchezaji wake raia wa Msumbiji, Miquissone kwa mkopo ili kupisha kusajiliwa mchezaji mwingine wa kigeni, huku Simba ikitajwa kupewa kipaumbele.

ADVERTISEMENT

Vyanzo mbalimbali nchini Misri vinasema kuwa Kocha Mkuu wa Al Ahly, Pitso Mosimane anatarajia kumtoa kwa mkopo kiungo mshambuliaji wake huyo mwenye umri wa miaka 26, msimu ujao kwa madai ya kushindwa kuelewa mfumo wa ufundishaji wake.

Taarifa zimedai kuwa mwenyewe Miquissone anapendelea kurudi klabu yake ya zamani ya Simba iliyomsajili Januari 2020 kipindi cha dirisha dogo kutoka UD Songo alipokuwa akicheza kwa mkopo, akiwa mali ya Mamelodi Sundowns.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa na Mabingwa wa Afrika, Al Ahly Agosti mwaka jana akiuzwa pamoja na Chama, amekuwa hana wakati mzuri ndani ya kikosi hicho ambapo licha ya kwamba amekuwa hapati nafasi ya kucheza, lakini baadhi ya mashabiki na wachezaji wa zamani wa klabu hiyo wanadai ni mchezaji mzuri, lakini siyo wa kiwango cha kuichezea timu kama Al Ahly, na alisajiliwa kwa mihemko tu, baada ya kuifunga bao kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa, Februari 23, mwaka jana kati ya mabingwa hao na Simba likiwa pekee kwenye mechi hiyo Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Kama ambayo viongozi wa Simba walivyokuwa wasiri kwenye mkakati wa kumrejesha Chama, wamekuwa wagumu pia kueleza kama wanaweza kumrejesha Miqussone au la kwa mujibu wa taarifa hizo.

Meneja Habari wa Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally alipoulizwa na Nipashe jana, alisema kuwa bado halijamfikia mezani kwake, na kama lipo basi litakuwa juu kwenye uongozi wa klabu hiyo.

“Sijui kama lipo au halipo, linasikikakwenye tetesi, labda kama lipo basi litakuwa kwenye uongozi wangu wa juu, na kama lipo na likawa tayari kwa kuambiwa wanachama na mashabiki, basi watanipa ili niwahabarishe, lakini kama litakuwa ni tetesi, basi litabaki kama tetesi, ila kwa sasa bado kwangu halijafika,” alisema Ahmed.

Viongozi wa Simba kwa miaka ya karibuni wamekuwa wakificha mno mikakati yao hususan ya usajili, kiasi hata suala la Chama lilionekana kama ni tetesi zisizo na mashiko na hekaya za Abunuwasi, lakini lilipofikia tamati likawekwa hadharani.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL
HABARI

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI
HABARI

NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI

by Ally Hamis Zingizi
May 14, 2022
Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa
HABARI

Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa

by I am Krantz
Apr 29, 2022
Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”
BURUDANI

Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”

by I am Krantz
Apr 27, 2022
AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE
BURUDANI

AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022
Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)
BIASHARA

Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In