ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Sunday, October 1, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

Miquissone Simba Tena?

I am Krantz by I am Krantz
Mar 25, 2022
in MICHEZO
0
Miquissone Simba Tena?
0
SHARES
378
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

KAMA ambavyo zilizuka tetesi za Clatous Chama kurejea Klabu ya Simba kutoka RS Berkane ya Morocco na baadaye ikawa kweli, sinema hiyo imeibuka tena, baada ya kiungo wa zamani wa timu hiyo anayeichezea Al Ahly ya Misri ambao ni Mabingwa wa Afrika, kudaiwa kutaka kurejea tena kwenye klabu hiyo.

Tetesi za Chama aliyeuzwa RS Berkane Agosti mwaka jana zilianza kama mzaha, lakini zilihitimishwa Desemba alipotangazwa kurejea akiwa ameitumikia timu hiyo kwa miezi minne tu.

RelatedPosts

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

CHAGUZI KUFANYIKA MTANDAONI SIKU ZIJAZO

Sep 29, 2023

TSO WAZINDUA GALA DINNER

Sep 29, 2023

CHANJO YA MBWA NI MUHIMU

Sep 29, 2023
Load More

Klabu ya Al Ahly imetajwa kuwa inaweza kumtoa mchezaji wake raia wa Msumbiji, Miquissone kwa mkopo ili kupisha kusajiliwa mchezaji mwingine wa kigeni, huku Simba ikitajwa kupewa kipaumbele.

Vyanzo mbalimbali nchini Misri vinasema kuwa Kocha Mkuu wa Al Ahly, Pitso Mosimane anatarajia kumtoa kwa mkopo kiungo mshambuliaji wake huyo mwenye umri wa miaka 26, msimu ujao kwa madai ya kushindwa kuelewa mfumo wa ufundishaji wake.

Taarifa zimedai kuwa mwenyewe Miquissone anapendelea kurudi klabu yake ya zamani ya Simba iliyomsajili Januari 2020 kipindi cha dirisha dogo kutoka UD Songo alipokuwa akicheza kwa mkopo, akiwa mali ya Mamelodi Sundowns.

Mchezaji huyo aliyesajiliwa na Mabingwa wa Afrika, Al Ahly Agosti mwaka jana akiuzwa pamoja na Chama, amekuwa hana wakati mzuri ndani ya kikosi hicho ambapo licha ya kwamba amekuwa hapati nafasi ya kucheza, lakini baadhi ya mashabiki na wachezaji wa zamani wa klabu hiyo wanadai ni mchezaji mzuri, lakini siyo wa kiwango cha kuichezea timu kama Al Ahly, na alisajiliwa kwa mihemko tu, baada ya kuifunga bao kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa, Februari 23, mwaka jana kati ya mabingwa hao na Simba likiwa pekee kwenye mechi hiyo Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Kama ambayo viongozi wa Simba walivyokuwa wasiri kwenye mkakati wa kumrejesha Chama, wamekuwa wagumu pia kueleza kama wanaweza kumrejesha Miqussone au la kwa mujibu wa taarifa hizo.

Meneja Habari wa Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally alipoulizwa na Nipashe jana, alisema kuwa bado halijamfikia mezani kwake, na kama lipo basi litakuwa juu kwenye uongozi wa klabu hiyo.

“Sijui kama lipo au halipo, linasikikakwenye tetesi, labda kama lipo basi litakuwa kwenye uongozi wangu wa juu, na kama lipo na likawa tayari kwa kuambiwa wanachama na mashabiki, basi watanipa ili niwahabarishe, lakini kama litakuwa ni tetesi, basi litabaki kama tetesi, ila kwa sasa bado kwangu halijafika,” alisema Ahmed.

Viongozi wa Simba kwa miaka ya karibuni wamekuwa wakificha mno mikakati yao hususan ya usajili, kiasi hata suala la Chama lilionekana kama ni tetesi zisizo na mashiko na hekaya za Abunuwasi, lakini lilipofikia tamati likawekwa hadharani.

Related

I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 
HABARI

TUNZAA YATANGAZA USHIRIKIANO MKUBWA NA KAMPUNI YA VODACOM KUPITIA M-PESA 

by I am Krantz
Sep 29, 2023
RAMADHAN BROTHERS WASHIKA NAFASI YA TANO AMERICA GOT TALENT
HABARI

RAMADHAN BROTHERS WASHIKA NAFASI YA TANO AMERICA GOT TALENT

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
MCHEZO WA MWAKINYO MPAKA HIVI SASA MAMBO BADO MAGUMU
HABARI

MCHEZO WA MWAKINYO MPAKA HIVI SASA MAMBO BADO MAGUMU

by SUZO SHUKRANI
Sep 29, 2023
TZ, KENYA NA UGANDA RASMI KUANDAA AFCON 2027
HABARI

TZ, KENYA NA UGANDA RASMI KUANDAA AFCON 2027

by SUZO SHUKRANI
Sep 27, 2023
SIMBA KUWAKOSA WACHEZAJI WATATU MCHEZO WA MARUDIANO
HABARI

SIMBA KUWAKOSA WACHEZAJI WATATU MCHEZO WA MARUDIANO

by SUZO SHUKRANI
Sep 27, 2023
USHINDI WA TWIGA STARS WAMLETA RAIS SAMIA
HABARI

USHINDI WA TWIGA STARS WAMLETA RAIS SAMIA

by SUZO SHUKRANI
Sep 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In