Tunaona picha za moshi mkubwa karibu na mnara wa Televisheni huko Kyiv.
BBC imethibitisha picha hizo lakini haijafahamika iwapo mnara huo uligongwa moja kwa moja.
Picha nyingine zinaonesha mlipuko katika eneo hilo.
Hapo awali wizara ya ulinzi ya Urusi ilionya wakaazi wa Kyiv kwamba inajiandaa kulenga maeneno maalumu katika mji mkuu.