ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Pesa za Zawadi NMB MastaBata zabaki Mil. 100/-

I am Krantz by I am Krantz
Mar 3, 2022
in HABARI
0
Pesa za Zawadi NMB MastaBata zabaki Mil. 100/-
0
SHARES
60
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Msimu wa Tatu wa Kampeni ya NMB MastaBata inayoendeshwa na Benki ya NMB, umezidi kushika kasi kuelekea ukingoni baada ya Alhamisi Machi 3 kufanyika kwa droo ya tisa, ambako washindi 100 walijinyakulia Sh. Milioni 10, hivyo kufanya pesa zilizopata washindi kufikia Sh. Milioni 140 kati ya Sh. Mil. 240 zinazoshindaniwa.

RelatedPosts

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

May 22, 2022

19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

May 22, 2022

MANULA AKATWA NA KIOO

May 22, 2022
Load More

NMB MastaBata – Kivyako Vyako, ni kampeni inayohamasisha matumizi na manunuzi kwa njia ya kadi badala ya pesa taslimu, ambayo inaendeshwa kwa kipindi cha wiki 10, zitakazoshuhudia wateja 1,080 wakijishindia pesa taslimu Sh. Mil. 240, wakiwamo washindi 1,000 wa wiki, washindi 50 wa mwezi na 30 wa ‘Grand Finale’.

ADVERTISEMENT

Ofisa wa Kitengo cha Kadi wa NMB, Lightness Zablon, alibainisha kuwa kampeni hiyo imekuwa na mafanikio makubwa, kwani imeongeza idadi ya miamala ya matumizi kwa njia ya kadi za MasterCard, Mastapass QR, vituo vya Mauzo (PoS) na mtandaoni.

Kampeni imeonesha mafanikio makubwa kwa kuwa imeongeza idadi ya miamala. Mwitikio wa matumizi ya kadi umekuwa mkubwa, kulingana na mahitaji ya kidijitali, ambako sasa unaweza hata kuagiza bidhaa nje ya nchini na kulipia kwa njia za kadi, badala ya pesa taslimu ambazo ni hatari kwa usalama.

Droo hiyo ilifanyika chini ya uangalizi wa Ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT), Elibariki Sengasenga, ambaye aliwahakikishia wateja wa benki hiyo kwamba kampeni hiyo inafanyika kwa kufuata vigezo, kanuni na sheria zinazotambulika na bodi yake na kuwatoa shaka wateja juu ya upatikanaji washindi.

Wakati washindi 100 wa kila wiki wakijishindia Sh. 100,000 kila mmoja, washindi 25 wa droo ya mwisho wa mwezi wa NMB MastaBasta hujishindia Sh. Milioni 1 kila mmoja, huku washindi 30 watakaopatikana kwenye ‘grande finale’ wakitarajia kujinyakulia Sh. Mil. 3, hivyo washindi 1,080 watazoa Sh. Mil. 240.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA
HABARI

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI
HABARI

19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
MANULA AKATWA NA KIOO
HABARI

MANULA AKATWA NA KIOO

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
NAMUNGO WAPEWA ALAMA TATU, KOCHA MAKATA AFUNGIWA MIAKA MITANO
HABARI

MAKATA, NAFTARI WAOMBA RADHI

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
VIFO MILIONI 8 KWA UVUTAJI WA SIGARA
HABARI

VIFO MILIONI 8 KWA UVUTAJI WA SIGARA

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO
HABARI

AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO

by Shabani Rapwi
May 22, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

https://www.youtube.com/watch?v=n2ZyFC8Lgig
KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In