ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Rais Joe Biden amwita Putin kuwa mhalifu wa kivita

I am Krantz by I am Krantz
Mar 17, 2022
in HABARI
0
Rais Joe Biden amwita Putin kuwa mhalifu wa kivita
0
SHARES
74
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

May 21, 2022

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

May 21, 2022

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

May 21, 2022
Load More

 

Wakatu hali ikiendelea kuwa mbaya nchini Ukraine, Rais Joe Biden wa Marekani amemwita rais wa Urusi Vladimir Putin kuwa ni mhalifu wa kivita.

Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Kreamlin Dmitry Peskov amesema kitendo cha rais wa Marekani Joe Biden kumwita Rais wa Urusi kuwa mhalifu wa kivita hakikubaliki na hakisameheki. Habari hizo ni kwa mjibu wa shirika la habari la taifa hilo TASS.

Rais Joe Biden wa Marekani amemwita rais wa Urusi Vladimir Putin kuwa ni mhalifu wa kivita, katika kipindi hiki ambacho matukio ya kikatili yakitajwa kuongezeka nchini Ukraine huku rais wa Ukraine akiliomba bunge la Marekani msaada zaidi.

Kauli hiyo inatazamwa kuwa kali zaidi kutoka Marekani tangu Urusi iivamie Ukraine. Wakati mataifa mengine yalitumia neno hilo lakini Marekani imekuwa ikijizuia.

Katika hotuba yake ya Jumatano Biden amesema vikosi vya Urusi vimeshambulia hosiptali na kuwachukua mateka madaktari. Hata hivyo ametoa ahadi zaidi kwa Ukraine katika kukabiliana kivita na Urusi. Amesema Marekani itatoa msaada wa nyongeza wa kijeshi wa kiasi cha dola milioni 800, na kufanya kiwango cha msaada kufikia jumla ya dola bilioni mbili tangu aingie madarakani mwaka mmoja uliopita.

Slovakia inatafakari kuipa Ukraine mfumo wa kujikinga na mashambulizi ya angani.

Maafisa wa ulinzi wa Slovakia wanatarajiwa kujadili uwezekano wa kupeleka mfumo wa ulinzi wa zama za uliokuwa umoja wa Kisovieti aina ya S-300 wa ulinzi wa anga, pale Waziri wa Ulinzi wa Marekani atakapo wasili nchini humo Alhamis hii kwa mashauriano zaidi.

Mfumo huo ndio ule ambao Rais wa Ukraine Volodymir Zelensky aliutaja pale alipozungumza na wabunge wa Marekani kwa kusema utaweza kuifunga anga ya Ukraine dhidi ya mashambulizi ya anga ya Urusi na makombora yake.

.

Ndani nchini Ukraine, wizara ya mambo ya nje imesema vikosi vya Urusi vimelishambalia jengo la micherzo la mji wa mji wa Mariupol, ambalo inadaiwa mamia ya watu wamepatiwa hifadhi baada ya makazi yao kuharibiwa na mapigano. Shambulizi kutoka angali linaelezwa kulipasua katikati jengo hilo.

Meya wa mji wa Kyiv Vitali Klitschko amesema makombora ya Urusi yameharibu maeneo kadhaa ya makazi ya watu na hasa katika kitongoji cha Podii, umbali wa kilometa 2.5 kutoka katika makao makuu ya serikali, ambayo pia yanajumuisha makazi ya rais, ofisi ya rais na ofisi nyingine muhimu.

Lakini taarifa hiyo haikuweza kufafanua juu ya athari zaidi zilizotokea kama kuna vifo au la. Wakazi wa Kyiv wamejificha katika makazi yao na maeneo maalumu baada ya kutolewa marufuku ya kutoka nje. Habari za mapema mjini humo zinasema jengo la ghorofa 12 liliwaka moto baada ya kushambuliwa na makombora ya Urusi.

Huko mjini Melitopol, Meya wa mji huo wa kusini/mashariki ameachiwa huru baada ya kutekwa na majeshi ya Urusisiku tano zilizopita. Andriy Yermak mkuu wa majeshi wa taifa hilo alitoa taarifa hizo pasipo ufafanuzi zaidi wa namna gani Fedorov aliachiwa huru.

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA
HABARI

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA
HABARI

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI
HABARI

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA
HABARI

ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA
HABARI

BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In