ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, May 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

SWIFT ni nini na Urusi kutengwa kutumia huduma za SWIFT kuna maana gani?

I am Krantz by I am Krantz
Mar 20, 2022
in HABARI
0
SWIFT ni nini na Urusi kutengwa kutumia huduma za SWIFT kuna maana gani?
0
SHARES
107
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

SWIFT, au Society for Worldwide Interbank Financial Telecommunication, ni mtandao salama wa kimataifa wa kutuma ujumbe ambao benki hutumia kufanya malipo yanayovuka mipaka. Mtandao huo unarahisisha taasisi za kifedha kusambaza pesa kwa kila mmoja, na kusaidia kuhakikisha kuwa biashara za kimataifa inaendelea vizuri.


Inatumiwa na zaidi ya taasisi za fedha 11,000 katika nchi na maeneo zaidi ya 200 kutuma maagizo salama ya malipo. Takriban jumbe milioni 40 zenye maagizo ya kuhamisha matrilioni ya dola zilitumwa kila siku mwaka wa 2020 kupitia mtandao huu, na kuifanya kuwa mtandao muhimu zaidi wa kutuma ujumbe wa malipo duniani, kufikia sasa.

RelatedPosts

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE

May 30, 2023

MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA

May 30, 2023

Legal Manager / Company Secretary Job Vacancy at BRAC Tanzania Finance LTD

May 30, 2023
Load More

Kwa sababu barua pepe zinazotumwa kwenye jukwaa huchukuliwa kuwa salama, husaidia benki kuheshimu maagizo ya malipo kwa haraka. Hii inahakikisha kwamba taasisi za fedha zinaweza kushughulikia kiasi kikubwa cha miamala kila siku.

Jumuiya hii yenye makao yake Ubelgiji, ilianzishwa mwaka 1973, inasimamiwa na benki kuu za Ulaya, Marekani, Kanada na Japan.

Urusi kupigwa marufuku kutumia SWIFT inamanisha nini?

Kuitenga Urusi kutoka kwenye mtandao kutasababisha usumbufu mkubwa kwa uchumi wake kwani kungezuia pakubwa ufikiaji wa nchi hiyo katika masoko ya kifedha ya kimataifa.

Marufuku hiyo itafanya iwe vigumu kwa makampuni na watu binafsi wa Urusi kulipia bidhaa zinazoagizwa kutoka nje au kupokea malipo ya mauzo yao, na hivyo kuleta pigo kubwa kwa sekta muhimu ya mafuta na gesi nchini humo, ambayo inategemea sana SWIFT kwa usafirishaji wa fedha. Pia itazuia uwezo wa Warusi kuwekeza au kukopa nje ya nchi.

Kunyakuliwa kwa benki za Irani kutoka kwenye mtandao mwaka 2012 kulichangia kwa kiasi fulani kupungua kwa mauzo ya mafuta nchini humo.

ADVERTISEMENT

Mashirika ya fedha ya Urusi yanaweza kutumia njia nyinginezo kama vile simu, programu za kutuma ujumbe au barua pepe kama njia mbadala na kushughulikia malipo kupitia benki katika nchi ambazo hazijaweka vikwazo. Lakini njia hizi mbadala hazitakuwa bora na salama kama SWIFT na zinaweza kusababisha gharama kubwa na kushuka kwa kiasi cha ununuzi.

Urusi imeunda mtandao wake wa kutuma ujumbe wa malipo, unaoitwa SPFS. Mfumo huu, ambao unashughulikia takribani moja ya tano ya malipo ya ndani, haufanyi kazi linapokuja suala la kiwango na ufanisi ambao SWIFT inatoa.

Chanzo: Deutsche Welle (DW)

ADVERTISEMENT

KUSOMA ZAIDI TEMBELEA http://TEKnolojia.co.tz

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE
HABARI

DIASPORA KUPEWA HADHI YA KIPEKEE

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA
HABARI

MAPACHA WALIOFARIKI ZIWANI WAKIOGELEA KUZIKWA MARA

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
Legal Manager / Company Secretary Job Vacancy at BRAC Tanzania Finance LTD
HABARI

Legal Manager / Company Secretary Job Vacancy at BRAC Tanzania Finance LTD

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
5 Various Job Vacancies at Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)
HABARI

5 Various Job Vacancies at Tanzania Agricultural Development Bank (TADB)

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
Digital Channels Manager Job Vacancy at Airtel Tanzania PLC
HABARI

Digital Channels Manager Job Vacancy at Airtel Tanzania PLC

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023
UMUHIMU WA KULA MATUNDA NA MBOGA MBOGA
HABARI

UMUHIMU WA KULA MATUNDA NA MBOGA MBOGA

by ALFRED MTEWELE
May 30, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In