ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Wednesday, June 7, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

USAID Kuisaidia Tanzania Shilingi Trilioni 3

I am Krantz by I am Krantz
Mar 26, 2022
in HABARI
0
USAID Kuisaidia Tanzania Shilingi Trilioni 3
0
SHARES
82
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na. Eva Valerian, WFM- Dodoma

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameliomba Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani – USAID, kuelekeza kiasi cha msaada wa dola za Marekani bilioni 1.3 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 3 inazotaka kuipatia Tanzania kupitia Asasi za kiraia, katika kipindi cha miaka 5 ijayo, zielekezwe kwenye miradi ya kipaumbele ya Serikali ya Awamu ya Sita.

RelatedPosts

TRA YASISITIZA WENYE UMRI MIAKA 18+ LAZIMA WAWE NA TIN NUMBER

TRA YASISITIZA WENYE UMRI MIAKA 18+ LAZIMA WAWE NA TIN NUMBER

Jun 7, 2023

BENZEMA AJIUNGA NA AL-ITTIHAD

Jun 7, 2023

KURASA ZA MAGAZETI LEO JUMATANO TAREHE 7 JUNI 2023

Jun 7, 2023
Load More

Dkt. Nchemba ametoa maombi hayo Mjini Dodoma, alipofanya mazungumzo kwa njia ya mtandao na Mkurugenzi wa Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani (USAID), Bi Kate Samvongsiri.

Alilishukuru Shirika hilo kwa uamuzi wake wa kutoa kiasi hicho cha fedha kupitia Asasi za Kiraia (NGOs) katika kipindi cha miaka mitano ijayo lakini akaeleza umuhimu wa miradi iliyokusudiwa kutekelezwa na asasi hizo za kiraia kuelekezwa katika vipaumbele vya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwemo sekta za afya, elimu, kilimo, na mingineyo itakayochochea ukuaji wa uchumi.

“Tunapoandaa ushirikiano mpya na mipango mipya tunaomba mzingatie vipaumbele vya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambayo amewekeza nguvu kubwa, sambamba na yale mnayofanya kwenye sekta ya afya, elimu, kilimo, mazingira, pamoja na sekta zingine”Alisema Dkt. Mwigulu

Dkt. Mwigulu alisema kwa sasa Mhe Rais anajenga vituo vingi vya afya na hivi karibuni ataajiri watumishi wengi wa sekta hiyo, pamoja na sekta zingine ambazo anazifanyia kazi kama sekta ya elimu na kuiomba USAID kuelekeza fedha hizo ambazo nitapitia kwenye mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs), kwenye maeneo hayo.

“Mfano, vituo vya afya vingi vimejengwa na watumishi wataajiriwa, mnaweza mkaweka nguvu kwenye vitendea kazi ambavyo bado havijakamilika ili huduma ziwe zinapatikana na lengo la Serikali pamoja na malengo mliyonayo ya kuendeleza huduma za jamii ambalo mnalo liweze kutimia” Alisema Mwigulu.

ADVERTISEMENT

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani -USAID, Bi Kate Samvongsiri, alisema kuwa wanapenda kushirikiana na Serikali ya Tanzania na watakaa pamoja na kuangalia shughuli zinazofanyika katika sekta hizo za elimu, afya, kilimo, maji pamoja na zingine na kuona namna watakavyoziwezesha.

Uhusiano kati ya Tanzania na Shirika hilo la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani USAID, limekuwa na uhusiano wa zaidi ya miaka 50, na kwamba tarehe 30 Septemba, 2016, Shirika hilo lilisaini mikataba mitatu ya msaada yenye thamani za zaidi ya dola za Marekani milioni 635.5, zilizotumika kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii, program ambayo itafikia tamati mwezi Septemba, 2022

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

TRA YASISITIZA WENYE UMRI MIAKA 18+ LAZIMA WAWE NA TIN NUMBER
HABARI

TRA YASISITIZA WENYE UMRI MIAKA 18+ LAZIMA WAWE NA TIN NUMBER

by ALFRED MTEWELE
Jun 7, 2023
KIKOSI KAZI MTEGONI/MEMBE AFUNGUKA/ACT YATEMA CHECHE/PABLO APATA KIGUGUMIZI……….MAGAZETINI LEO JUMATATU TAREHE 30 MEI 2022
HABARI

KURASA ZA MAGAZETI LEO JUMATANO TAREHE 7 JUNI 2023

by I am Krantz
Jun 7, 2023
BODI YA CHAI NA TMX ZAINGIA MAKUBALIANO YA MNADA WA CHAI
HABARI

BODI YA CHAI NA TMX ZAINGIA MAKUBALIANO YA MNADA WA CHAI

by ALFRED MTEWELE
Jun 6, 2023
TUNAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA SIKOSELI NCHINI – DKT. SHEKALAGHE
HABARI

TUNAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA SIKOSELI NCHINI – DKT. SHEKALAGHE

by ALFRED MTEWELE
Jun 6, 2023
EPUKA TABIA HIZI HATARISHI UNAPOENDESHA GARI YAKO
HABARI

EPUKA TABIA HIZI HATARISHI UNAPOENDESHA GARI YAKO

by ALFRED MTEWELE
Jun 6, 2023
AHMED ALLY-“TULICHEZA FAINALI CAF 1993, ITABAKI KUWA HIVYO”
HABARI

AHMED ALLY-“TULICHEZA FAINALI CAF 1993, ITABAKI KUWA HIVYO”

by ALFRED MTEWELE
Jun 6, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
March 2022
M T W T F S S
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031  
« Feb   Apr »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In