ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Ajitosa Baharini na Kufa Akiwakimbia Polisi Kwa Tuhuma za Kutishia Kumuua Mpenzi Wake

I am Krantz by I am Krantz
Apr 7, 2022
in HABARI
0
Ajitosa Baharini na Kufa Akiwakimbia Polisi Kwa Tuhuma za Kutishia Kumuua Mpenzi Wake
0
SHARES
49
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

MKAZI wa mtaa wa Sabasaba, Kata ya Jamhuri, Manispaa ya Lindi, Hassani Mussa M’buyu (27), amekufa maji, baada ya kujitosa baharini kwa madai ya kukimbia kukamatwa kwa tuhuma za kutishia kumuua mpenzi wake.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, ACP Mtatiro Kitinkwi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

RelatedPosts

WATU MILIONI 8 HUFARIKI KWA MWAKA KISA UVUTAJI WA SIGARA

WATU MILIONI 8 HUFARIKI KWA MWAKA KISA UVUTAJI WA SIGARA

May 22, 2022

AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO

May 22, 2022

ANAYETUHUMIWA KUMLAWITI BINTI YAKE AKAMATWA NA POLISI LINDI

May 22, 2022
Load More

Alisema M’buyu ambaye ni mwendesha bodaboda, alichukua uamuzi huo, Aprili 4, mwaka huu, saa 12:30 jioni.

ADVERTISEMENT

Kamanda Kitinkwi alisema, M’buyu alifikishwa Kituo cha Polisi Lindi mjini kwa tuhuma za kumpiga na kumtishia kumuua mpenzi wake Sharifa Zakaria Mussa (23).

Alisema baada ya mlalamikaji kuwasilisha madai hayo, askari kupitia dawati la jinsia lilichukua jukumu la kumuandikia M’buyu barua kumtaka kufika kituoni kwa mahojiano kuhusu madai yaliyowasilishwa na mpenzi wake.

“Huyu M’buyu baada ya kufika kituoni pale, alielekezwa aende chumba cha dawati la jinsia,” alisema Kamanda.

Kamanda alisema baada ya mlalamikiwa kufika mlango wa chumba cha dawati, alimkuta mpenzi wake akiwa ndani ameshawasili na kuamua kuchukua hatua ya kukimbia, askari walivyomuona walimkimbiza, lakini alikataa kusimama na kujitosa baharini na kufariki.

“Kituo chetu cha polisi hapa Lindi mjini kipo kama umbali wa mita 100 kufika baharini,” alisema Kitinkwi.

Sharifa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema yeye na M’buyu walikuwa wapenzi na kubahatika kubeba ujauzito, lakini hakuwa anampatia huduma yoyote.

Alisema hata alipolazwa hospitalini akisumbuliwa na maumivu ya tumbo hakuwahi kwenda kumuona kumjulia hali, huku gharama zote za matibabu zikitekelezwa na mama yake mzazi, hatua iliyomlazimu kukatisha mahusiano yao.

Sharifa alisema uamuzi huo ulimjengea uhasama na mpenzi wake kwa kumpa kichapo na kumtishia kumuua iwapo ataendelea na uamuzi wake wa kumkataa kwa kumkata mapanga, hali iliyomlazimu kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ya usalama wa maisha yake.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WATU MILIONI 8 HUFARIKI KWA MWAKA KISA UVUTAJI WA SIGARA
HABARI

WATU MILIONI 8 HUFARIKI KWA MWAKA KISA UVUTAJI WA SIGARA

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO
HABARI

AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
ANAYETUHUMIWA KUMLAWITI BINTI YAKE AKAMATWA NA POLISI LINDI
HABARI

ANAYETUHUMIWA KUMLAWITI BINTI YAKE AKAMATWA NA POLISI LINDI

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA
HABARI

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA
HABARI

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In