ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, February 7, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Askofu Bagonza: Taifa linahitaji miafaka, siyo muafaka

I am Krantz by I am Krantz
Apr 9, 2022
in HABARI
0
Askofu Bagonza: Taifa linahitaji miafaka, siyo muafaka
0
SHARES
130
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Mwanza. Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Karagwe, Dk Benson Bagonza amesema kuna umuhimu wa Watanzania kuwa tayari kufikia muafaka katika mambo ya msingi yanayoibua misigano kwa nia ya kuendelea kuwa Taifa lenye watu wamoja licha ya tofauti zao kisiasa, kijamii na kiuchumi.

RelatedPosts

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Feb 7, 2023

HAJI MANARA AIJIA JUU BODI YA LIGI KISA CLEAN SHEETS, SIMBA SC

Feb 7, 2023

DAYOO AFUNGUKA KWANINI ANASEMA “NAITWA MANGI…”

Feb 7, 2023
Load More

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu leo Ijumaa Aprili 8, amesema ili kufikia lengo hilo, ni lazima kila upande unaohusika uweke mbele maslahi ya jamii na Taifa kwa ujumla kwa kukubali kupata na kupoteza kwa faida ya wote.

“Taifa limegawanyika. Karibia kila eneo kunasikika kauli za wao na sisi. Siyo kwenye siasa pekee, bali pia hata kwetu viongozi wa dini tumeparaganyika, na kwa msingi huo, ni dhahiri tunahitaji miafaka na siyo muafaka,” amesema Askofu Bagonza

Akithibitisha na kufafanua ujumbe wake unaozunguka kupitia mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari “Inahitajika miafaka, siyo muafaka’, Askofu Bagonza amesema ni ukweli usiopingika kwamba mparaganyiko unaoshuhudiwa nchini hivi sasa hauko kwenye uwanja wa siasa pekee kati ya walioko madarakani na walioko nje ya madaraka, bali uko katika kila kundi la jamii, hali inayolazimisha uwepo wa miafaka mingi kutibu Taifa.

ADVERTISEMENT

“Katika kufikia miafaka hiyo, siyo lazima kukubaliana kila kitu kwa sababu muafaka siyo kukubaliana kila kitu, bali ni kukubaliana kutokukubaliana bila kuparaganyika,” amesisitiza kiongozi huyo wa dini.

Soma ujumbe mzima wa andiko la Askofu Bagonza

INAHITAJIKA MIAFAKA siyo MUAFAKA

Kuna harufu ya mparaganyiko kila mahali. Ni kama tuna nchi moja yenye mataifa mengi ndani yake. Badala ya muafaka wa kitaifa, inahitajika miafaka kadhaa ili kuunda muafaka mmoja.

1. CCM si moja. Kuna CCM-Mpina na CCM-January. Kuna CCM-Mwendazake na CCM-Samia. Kuna CCM-Asili na CCM-Yatima. Hizi CCM zote zinahitaji muafaka ili tupate CCM moja.

2. Wapinzani si wamoja. Kuna wapinzani-Katiba Mpya na Wapinzani-Nusu Katiba Mpya. Kuna wapinzani-Mtungi na Wapinzani-Mahela. Kuna Wapinzani-Zanzibar huru na Wapinzani-Zanzibar Mkoa. Unahitajika muafaka kati ya wapinzani kabla ya muafaka wa kitaifa.

3. Serikali si moja. Kuna serikali awamu ya 5 rais wa sita na Serikali awamu ya sita rais wa sita. Kuna serikali-2025 na Serikali-2030. Hizi serikali zinahitaji muafaka.

4. Kuna bunge-live na bunge-giza. Kuna bunge-haramu ndani jengo halali na bunge-halali nje ya jengo halali. Kuna sheria halali zilizotungwa na bunge haramu.

ADVERTISEMENT

5. Kuna Polisi-Tii sheria bila shuruti na Polisi-Tii shuruti bila sheria. Kuna IGP bila Polisi na Polisi bila IGP.

Unashangaa? Tanzania ni eneo la utalii. Kila kitu ni kiburudisho. Hatuambukizani Corona, tunaambukizana tabia. Mwenyekiti wa msiba anamuiga Spika namna ya kuongoza kikao cha mazishi. Askofu anamuiga OCD ili kuongoza kanisa. Kocha wa Simba anamuiga kocha wa Yanga lakini anafungwa mengi kuliko Yanga.

Bei ya mafuta imepandisha hata rushwa ya barabarani.

Mwananchi

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA
HABARI

HIZI HAPA JEZI MPYA ZA SIMBA ZA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
TANZANIA, UAE ZASAINI KUHIFADHI MAZINGIRA
HABARI

TANZANIA, UAE ZASAINI KUHIFADHI MAZINGIRA

by ALFRED MTEWELE
Feb 7, 2023
YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25
HABARI

HAMTAMUONA KOCHA NABI AIRPORT – ALLY KAMWE

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25
HABARI

YANGA KWENDA TUNISIA LEO NA WACHEZAJI 25

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
QUEIROZ KOCHA MPYA QATAR
HABARI

QUEIROZ KOCHA MPYA QATAR

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023
ATSU APATIKANA AKIWA HAI KUTOKA KWENYE VIFUSI
HABARI

ATSU APATIKANA AKIWA HAI KUTOKA KWENYE VIFUSI

by Shabani Rapwi
Feb 7, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In