ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

DKT. BITEKO AAGIZA UCHUNGUZI CHANZO CHA TETEMEKO LA ARDHI USHETU

Shabani Rapwi by Shabani Rapwi
Apr 30, 2022
in HABARI
0
DKT. BITEKO AAGIZA UCHUNGUZI CHANZO CHA TETEMEKO LA ARDHI USHETU
0
SHARES
31
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

 

RelatedPosts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

May 21, 2022

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

May 21, 2022

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

May 21, 2022
Load More

Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko ameagiza kuundwa kwa Kamati Maalum ya Wataalamu ili kuchunguza uwepo wa milipuko inayolalamikiwa na wananchi kuwa chanzo cha mitetemo wanayoipata katika eneo la Kijiji cha Ulowa kilichopo Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga.

ADVERTISEMENT

–

Dkt.Biteko ametoa agizo hilo leo Aprili 30, 2022 katika Kijiji cha Ulowa Halmashauri ya Ushetu Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga na akitaka kazi hiyo ifanyike ndani ya wiki mbili.

–

Dkt. Biteko amesema, Wizara ya Madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) itapeleka timu ya wataalamu inayohusika na mitetemo ya ardhi ambao watafanya kazi ya uchunguzi kwa muda wa wiki mbili.

–

Amesisitiza kuwa, tetemeko la ardhi haliwezi kuwa limesababishwa na shughuli za kibinadamu kwa kuwa hakuna ulipuzi wa miamba mikubwa unaofanyika katika eneo hilo.

–

Amesema GST itasimika kifaa maalum katika eneo la Ulowa kwa ajili ya kunakili mawimbi ya mitetemo mbalimbali itakayotokea katika eneo hilo ili kupata taarifa sahihi juu ya chanzo halisi cha mitetemo hiyo.

–

Naye, Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojojia na Utafiti wa Madini Tanzania, Dkt. Musa Budeba amesema, GST itafanya utafiti wa ziada ili kubaini chanzo cha mitetemo katika maeneo hayo na kusisitiza kuwa wataalamu watafika katika maeneo ya mitetemo ili kuondoa hofu walizonazo wananchi hao kuhusu matetemeko ya ardhi.

–

Kwa upande wake, Mjiolojia Mwandamizi, John Kalimenze akisoma taarifa kuhusu mitetemo ya ardhi inayosadikiwa kuwa tetemeko la ardhi amesema, jumla ya wananchi takribani mia moja walipatiwa elimu na mafunzo kuhusu tetemeko la ardhi, namna gani linatokea, jinsi ya kuchukua tahadhari kabla halijatokea, wakati linapotokea na baada ya kutokea.

–

“Mafunzo hayo yalisaidia sana kupunguza taharuki iliyokuwepo miongoni mwa wakazi wa Ulowa namba 8 na maeneo ya jirani kama ambavyo waliwaeleza wataalamu baada ya kupatiwa mafunzo,” amesema Kalimenze.

–

Taarifa za mitetemo kutoka Kituo cha GST cha kuratibu mitetemo ya ardhi kilichopo mjini Geita zinaonesha kwamba, hakuna matetemeko ya ardhi yaliyotokea katika eneo la Ulowa katika kipindi cha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2022 kama ilivyodaiwa na wananchi wa Ulowa.

–

Kikao hicho, kimehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Festo Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Emmanuel Cherehani, Diwani wa Kata ya Nyamilangano, Robert Mihayo na watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Madini na Tume ya Madini.

Related

ADVERTISEMENT
Shabani Rapwi

Shabani Rapwi

Shabani Rapwi (Kijana Mchapa Kazi) WhatsApp; 0689232546 Email ;shabanimohamed932@gmail.com

Related Posts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA
HABARI

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA
HABARI

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI
HABARI

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA
HABARI

ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA
HABARI

BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In