ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, March 28, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Dkt. Tulia aipongeza Benki ya CRDB kuuenzi mwezi Ramadhani

I am Krantz by I am Krantz
Apr 20, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
Dkt. Tulia aipongeza Benki ya CRDB kuuenzi mwezi Ramadhani
0
SHARES
115
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Dodoma 20 Aprili 2022 –Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Dkt. Tulia Ackson. Spika ameipongeza Benki ya CRDB kuuenzi mwezi Ramadhani kwa kuwa karibu na jamii katika kipindi cha mfungo wa Ramadhani. Spika ametoa pongezi hizo akipokea zawadi za mwezi wa Ramadhani kwa niaba ya wabunge ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa Benki ya CRDB kushirikiana na wateja wake na makundi mbalimbali katika jamii katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. Zawadi hizo zilikabidhiwa katika Ofisi za Bunge na Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile.

RelatedPosts

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA BENKI YA CRDB, AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA BENKI YA CRDB, AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA

Aug 9, 2022

BENKI YA CRDB YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE KITAIFA, JIJINI MBEYA

Aug 2, 2022

WAZIRI MBARAWA AWATAKA WAKANDARASI NA WAZABUNI KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEZESHAJI KUTOKA BENKI YA CRDB

Jul 21, 2022
Load More

 

Akizungumza wakati wa kupokea zawadi hizo Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson alisema kuwa Benki ya CRDB imekua mstari wa mbele kushirikiana na wadau na kuwataka kuendeleza utamaduni huo hata baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.

ADVERTISEMENT

“Nawapongeza sana Benki ya CRDB kwa kuendeleza utaratibu wao wa kuwa karibu na jamii katika kipindi hiki cha Mfungo wa Ramadhani na hasa kwa kugusa makundi mbalimbali hususani wahitaji na niwaombe waendeleze utaratibu huu hata baada ya mwezi Ramadhani” alisema Mh. Tulia

 

Kwa upande wake Afisa Mkuu wa Undeshaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile alisema Benki ya CRDB ni benki ya kizalendo inayotambua na kuyaishi maisha ya Mtanzania halisi ambapo kipindi hiki cha Ramadhani ni utamaduni wa Watanzania katika kujumuika pamoja kwa ajili ya ibada na futari.

“Pamoja na kuwa leo tupo hapa kwa ajili ya waheshimiwa wabunge lakini tumeendeleza utaratibu wetu wa kufuturisha wateja wetu na makundi yenye mahitaji maalumu ambapo tangu tumeanza mwezi Ramadhani tayari tumeshafanya hivyo kwa mikoa ya Tanga na Shinyanga na wiki hii tunarajia kufanya hivyo kwa mikoa ya Mtwara, Njombe, Mwanza na pia tutafanya hivyo visiwani Zanzibar” aliongeza Bruce.

Pamoja na ushiriki katika mfungo wa mwezi Ramadhan kupitia futari na misaada kwa wenye uhitaji, hivi karibuni Benki ya CRDB imeanzisha huduma maalum za fedha inayozingatia misingi ya kutotoa na kupokea riba inayoitwa Al Barakah. Hadi sasa huduma ya Al Barakah imevutia wateja zaidi ya elfu nane huku mikopo iliyotolewa kupitia huduma hiyo ikiwa na thamani zaidi ya Shilingi Bilioni 8.

 

ADVERTISEMENT

 

Related

Tags: CRDB
ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION  KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA
HABARI

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

by Ally Hamis Zingizi
Mar 27, 2023
NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
HABARI

NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

by I am Krantz
Mar 27, 2023
Naibu Waziri   aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya  michezo
HABARI

Naibu Waziri aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya michezo

by I am Krantz
Mar 27, 2023
MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA
HABARI

MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14
HABARI

BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL
HABARI

MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In