ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

‘Mfalme Zumaridi’, wenzake wafikishwa mahakamani, 8 waomba dhamana

I am Krantz by I am Krantz
Apr 1, 2022
in HABARI
0
‘Mfalme Zumaridi’, wenzake wafikishwa mahakamani, 8 waomba dhamana
0
SHARES
58
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Diana Bundala maarufu kama ‘Mfalme Zumaridi’ na wenzake 83 leo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili.

Zumaridi na wenzake wanakabiliwa na makosa matatu ikiwamo ya usafirishaji haramu wa binadamu, shambulio la kudhuru mwili na kuzuia maofisa wa Serikali kutimiza wajibu wao.

RelatedPosts

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

May 22, 2022

19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

May 22, 2022

MANULA AKATWA NA KIOO

May 22, 2022
Load More

Wakati wa kuwasili ndani ya chumba cha mahakama Zumaridi ameonekana akiwa amejifunika na kitenge wakati wote kisha akalazimika kukiondoa baada ya kupanda kizimbani kusomewa maelezo hayo.

ADVERTISEMENT

Hata hivyo, washtakiwa hao hawakusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yanayowakabili kutokana na Hakimu Mkazi mwandamizi, Monica Ndyekobora ambaye ndiyo mwenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kutokuwepo leo mahakamani jambo lililosababisha mashauri hayo kusikilizwa na Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza, Stela Kiama.

Washtakiwa baada ya kufikishwa mahakamani wamesomewa mashtaka yanayowakabili na wakili wa Serikali Mwandamizi anayeendesha mashtaka hayo, Emmanuel Luvinga akishirikina na Gisela Bantulaki.

Katika shauri hilo, kuna mashtaka matatu yanayowakabili washtakiwa hao ambayo ni kesi ya jinai namba 11/2022 ambayo ni usafirishaji haramu wa binadamu inayomkabili mfalme Zumaridi peke yake, kesi ya jinai namba 10/2022 ambayo ni kufanya shambulio la kudhuru mwili kwa lengo la kuzuia maofisa wa serikali kutimiza wajibu wao linalomkabili Zumaridi na wenzake 8.

Nyingine ni kesi ya jinai namba 12/2022 inayomkabili mhubiri huyo na wenzake 83 ambayo ni kufanya kusanyiko lisilo rasmi.

Baada ya Washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, wakili wa utetezi, Erick Mutta aliwasilisha maombi ya dhamana kwa washtakiwa wanane wanaoendelea kusota rumande na mhubiri huyo ambayo yalikubaliwa na mahakama hiyo baada ya washtakiwa kukidhiri vigezo na masharti ya dhamana.

Kwa upande wake, Mfalme Zumaridi kutokana na kukabiliwa na kesi ya usafirishaji haramu wa binadamu isiyo na dhamana anaendelea kusota rumande na washtakiwa wenzake nane ambao hawajakidhi vigezo vya kupewa dhamana.

Shauri hilo limeahirishwa hadi Aprili 4 mwaka huu litakapoitwa kwa ajili ya kusomwa maelezo ya awali kwa washtakiwa.

Katika hatua nyingine, wakili wa utetezi Erick Mutta ameiambia mahakama hiyo kwamba, mshtakiwa namba 67 (Elias Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na maofisa kutoka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kufika ofisi kwake kwa ajili ya kumfanyia ukaguzi.

Amesema mshtakiwa namba 38 (Maria Joseph) ameshindwa kufika mahakamani hapo kutokana na kulazwa katika hospitali ya rufaa ya Kanda ya Bugando akipatiwa matibabu ya majeraha aliyopata wakati wa ukatamaji uliofanywa na maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani humo.

Pia amesema mshtakiwa namba 84 (Kanyangi Mary) na 68 wameshindwa kuhudhuria shauri hilo kutokana na kuhudhuria matibabu katika hospitali

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA
HABARI

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA MAWE KIMIUJIZA

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI
HABARI

19 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
MANULA AKATWA NA KIOO
HABARI

MANULA AKATWA NA KIOO

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
NAMUNGO WAPEWA ALAMA TATU, KOCHA MAKATA AFUNGIWA MIAKA MITANO
HABARI

MAKATA, NAFTARI WAOMBA RADHI

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
VIFO MILIONI 8 KWA UVUTAJI WA SIGARA
HABARI

VIFO MILIONI 8 KWA UVUTAJI WA SIGARA

by Shabani Rapwi
May 22, 2022
AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO
HABARI

AMRI YATOLEWA WATANGAZAJI WANAWAKE WAFUNIKE NYUSO ZAO

by Shabani Rapwi
May 22, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In