Morrison habari nzito CAF – Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, May 19, 2022
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Morrison habari nzito CAF

I am Krantz by I am Krantz
Apr 7, 2022
in MICHEZO
0
Morrison habari nzito CAF
0
SHARES
49
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

KATIKA mechi 10 ambazo Simba imecheza kwenye michuano ya CAF msimu huu imefunga mabao 16 huku winga wao, Bernard Morrison ndiye mchezaji pekee aliyechangia idadi kubwa zaidi (saba), akifuatia Shomari Kapombe (matatu).

Morrison aliyeonyesha ukomavu CAF, anaongoza kwa asisti tano, huku akifunga mabao matatu na hiyo ilitokana na ujanja wake pamoja na wepesi wa kukabailiana na mabeki wa timu pinzani.

RelatedPosts

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

WATANZANIA TAYARI KULIPIA BIMA YA AFYA

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

May 19, 2022
Load More

Mchezaji huyo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika alitoa asisti moja na upande wa Kombe la Shirikisho alitoa asisti tatu huku akifunga mabao matatu.

Kwenye ligi hiyo, Simba ilicheza mechi mbili dhidi ya Jwaneng Galaxy na walishinda jumla ya mabao matatu baada ya mchezo wa kwanza Simba kushinda 2-0 na kwenye mchezo wa marudiano alifungwa 3-1 na kuondolewa katika kombe hilo na kwenda kushiriki Kombe la Shirikisho Afrika kuanzia hatua ya makundi.

Morrison alitoa asisti kwenye mchezo waliofungwa 3-1 huku Lary Bwalya akifunga bao la kufutia machozi.

Katika mchezo wa kwanza kwenye Shirikisho, Simba walianza na Red Arrows uliomalizika wakishinda 3-0, Morrison alifunga mabao mawili huku bao la tatu likifungwa na Meddie Kagere (asisti Morrison).

Morrison alisawazisha dhidi ya USGN (1-1) Simba ikiwa timu pekee kundi D kupata pointi ya ugenini.

ADVERTISEMENT

Mchezaji huyu alikuja kuhusika tena katika ushindi wa 4-0 dhidi ya USGN akitoa asisti mbili na kuifanya Simba itinge hatua ya robo fainali ya Kombe hilo kibabe.

Kocha msaidizi wa Kagera Sugar, Ulimboka Mwakingwe alisema Morrison ana uwezo wa kuamua mechi ngumu na kuutafsiri mchezo unataka nini, jambo analoamini linamng’arisha mechi za kimataifa.

“Anajua anachokitaka uwanjani, akiamua kuwekeza nguvu zaidi kwenye kazi, atafanya makubwa zaidi ya hayo tunayomuona anafanya,” alisema.

Kauli hiyo iliungwa mkono na beki wa zamani wa timu hiyo, Godwin Aswile aliyesema alichokigundua kwa Morrison ana maamuzi ya kucheza kwa kiwango cha juu ama chini.

“Ana maamuzi ya nini afanye, nimemwona kwenye mechi ngumu ambazo Simba inahitaji matokeo, anapambana na kujitoa, mfano alitengeneza nafasi nyingi dhidi ya USGN alipoona anaowapa asisti wafunge hawafungi akaanza kujaribu kupiga mwenyewe, tafsiri yake alihitaji kuona wanapata mabao, hiyo ndio maana ya mchezaji mkubwa,” alisema.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

Related Posts

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL
HABARI

BMT YAPOKEA UJUMBE KUTOKA SHIRIKISHO LA DUNIA LA MCHEZO WA BASEBALL

by Ally Hamis Zingizi
May 19, 2022
NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI
HABARI

NENDENI MKAPAMBANE TAIFA LINAWATEGEMEA WACHEZAJI

by Ally Hamis Zingizi
May 14, 2022
Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa
HABARI

Manula Afunguka ni Wapi Atacheza Msimu Ujao..Azam Yatajwa

by I am Krantz
Apr 29, 2022
Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”
BURUDANI

Wema Sepetu Atoa Neno “Lulu Michael ni Mdogo Wangu Naweza Mpiga Hata KOFI, Mkiona Tunagombana Tulia”

by I am Krantz
Apr 27, 2022
AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE
BURUDANI

AKAUNTI YA DIAMOND YAFUTWAA YOUTUBE

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022
Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)
BIASHARA

Absa Tanzania yakabidhi zawadi kwa mshindi wa kampeni ya Absa Card Assist ya ligi kuu ya Uingereza (EPL)

by Ally Hamis Zingizi
Apr 25, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Login to your account below

Forgotten Password?

Fill the forms bellow to register

*By registering into our website, you agree to the Terms & Conditions and Privacy Policy.
All fields are required. Log In

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In