ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Rais Samia ashinda tuzo Afrika

I am Krantz by I am Krantz
Apr 10, 2022
in HABARI
0
Rais Samia Kuchanjwa Covid-19, Ikulu
0
SHARES
163
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

Rais Samia ashinda tuzo Afrika

RelatedPosts

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Jumatatu Februari 6,2023

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Ijumaa Machi 24,2023

Mar 24, 2023

MESUT ÖZIL ATANGAZA KUSTAAFU SOKA

Mar 23, 2023

WABUNGE WAONYA KUWEKEA VIKWAZO SHERIA YA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Mar 23, 2023
Load More

RAIS Samia Suluhu Hassan ameshinda Tuzo ya Mwaka 2022 ya Babacar Ndiaye kwa mafanikio ya serikali yake katika ujenzi wa miundombinu ya usafi rishaji.

Tuzo hiyo hutolewa kwa watu mashuhuri barani Afrika ambao wameonesha dhamira ya kuendeleza miundombinu ya usafiri katika bara hilo. Hayo yalibainishwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika taarifa yao kwa vyombo vya habari jana.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Samia alitangazwa jana mjini Abidjan nchini Ivory Coast kuwa mshindi wa tuzo hiyo ya Babacar Ndiaye kwa mwaka huu. “Kamati ya uteuzi ilimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake binafsi, uwekezaji mkubwa na kujitolea katika kupanua mtandao wa barabara na reli nchini Tanzania.

Tunatuma pongezi zetu za dhati kwa Rais Samia na wananchi wa Tanzania,” ilisema taarifa hiyo. AfDB ilisema Kamati ya Uteuzi ilibaini kuwa kiasi cha Dola milioni 290 zilitolewa na benki hiyo kwa ajili ya kusaidia uboreshaji wa barabara, reli na usafiri wa anga Tanzania pamoja na kuzingatia mkataba wa Dola za Marekani milioni 172.2 uliosainiwa na Kampuni ya China (China Corporation Limited) kwa ajili ya ununuzi wa mabehewa ya mizigo 1,430 ili kutekeleza mpango kabambe wa Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, kamati pia ilibaini kuanza kwa ujenzi wa Mradi wa Barabara ya Mzunguko katika Jiji la Dodoma, ambao ulizinduliwa na Rais Samia Februari mwaka huu na kushuhudiwa na Rais wa AfDB, Dk Akinwumi Adesina. Rais Samia aliingia madarakani Machi mwaka jana kutokana na kifo cha Rais John Magufuli.

ADVERTISEMENT

Baada ya kuingia madarakani, Rais Samia aliweka bayana kuwa atakamilisha ujenzi wa miradi yote ikiwemo ya miundombinu ya usafiri na usafirishaji iliyoanzishwa na Serikali ya Awamu ya Tano, lakini pia serikali yake itaanzisha miradi mipya.

Baadhi ya miradi hiyo ni ukamilishaji wa ujenzi wa Daraja la Tanzanite Dar es Salaam, ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kimara Dar es Salaam hadi Kibaha mkoani Pwani, ujenzi wa Daraja la Kigongo- Busisi mkoani Mwanza, ujenzi wa Daraja la Wami, ujenzi wa Barabara ya Kidatu-Ifakara, ujenzi wa barabara ya mwendokasi kutoka Mbagala hadi Gerezani Kariakoo.

Miradi mingine ni ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Msalato jijini Dodoma, viwanja vya ndege katika mikoa mbalimbali, ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, Morogoro-Dodoma- Makutupora, Mwanza- Isaka na vipande vingine vilivyobaki pamoja na miradi mbalimbali ya barabara.

Ikifadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, Tuzo ya Africa Road Builders Babacar Ndiaye’ inaandaliwa na Acturoutes, Jukwaa la Habari kuhusu miundombinu na barabara katika Afrika na Taasisi ya Vyombo vya Habari kuhusu Miundombinu na Fedha Afrika (MIFA), ambao ni mtandao wa waandishi wa habari Afrika waliojikita katika miundombinu ya barabara.

ADVERTISEMENT

Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari alishinda tuzo hiyo mwaka jana. Tuzo hiyo ilianzishwa kwa heshima ya Babacar Ndiaye, Rais wa Kundi la Benki ya Maendeleo Afrika kuanzia mwaka 1985 hadi 1995.

Tuzo kwa mwaka 2022 inayokwenda kwa Rais Samia itakabidhiwa katika mkutano wa mwisho wa Africa Road Builders uliopangwa kufanyika sambamba na mkutano wa mwaka wa AfDB mwezi ujao mjini Accra, Ghana.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Jumatatu Februari 6,2023
HABARI

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Ijumaa Machi 24,2023

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
WABUNGE WAONYA KUWEKEA VIKWAZO SHERIA YA MAPENZI YA JINSIA MOJA
HABARI

WABUNGE WAONYA KUWEKEA VIKWAZO SHERIA YA MAPENZI YA JINSIA MOJA

by ALFRED MTEWELE
Mar 23, 2023
UWANJA WA NDEGE CHATO KUBORESHWA
HABARI

UWANJA WA NDEGE CHATO KUBORESHWA

by ALFRED MTEWELE
Mar 23, 2023
ASHTAKIWA MAHAKAMANI KUWAINGILIA MBUZI KIMWILI
HABARI

ASHTAKIWA MAHAKAMANI KUWAINGILIA MBUZI KIMWILI

by ALFRED MTEWELE
Mar 23, 2023
NMB yatoa msaada wa milioni 39 kuimarisha sekta ya afya na elimu Kanda ya Kati
HABARI

NMB yatoa msaada wa milioni 39 kuimarisha sekta ya afya na elimu Kanda ya Kati

by I am Krantz
Mar 23, 2023
Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Jumatatu Februari 6,2023
HABARI

Yaliojili Kwenye Kurasa za Magazeti ya Leo Alhamisi Machi 23,2023

by ALFRED MTEWELE
Mar 23, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In