ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Tuesday, March 28, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Vijana 10 wakamatwa kwa kujeruhi, kupora Dar

Ally Hamis Zingizi by Ally Hamis Zingizi
Apr 28, 2022
in HABARI
0
Vijana 10 wakamatwa kwa kujeruhi, kupora Dar

Prisoner holding metal cage in jail, no freedom concept

0
SHARES
108
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION  KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

Mar 27, 2023

NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

Mar 27, 2023

Naibu Waziri aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya michezo

Mar 27, 2023
Load More
ADVERTISEMENT
    
VIJANA
 Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema linawashikilia vijana 10 wanaodaiwa kuvamia nyumba kwenye mitaa mitatu ya Chanika wilayani Ilala, kupora mali na kujeruhi watu 23.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 28, 2022, Kamanda wa Kanda hiyo Jumanne Muliro amesema vijana wengi waliokamatwa umri wao unaanzia miaka 13 hadi 21.

Amesema baada ya kuhojiwa, vijana hao wamekiri kuhusika na matukio hayo na wamendelea kuisaidia Polisi kuhakikisha wenzao wanaotoka maeneo mbalimbali waliohusika na matukio hayo wanakamatwa.

“Vijana hao wamekuwa wakitumia mapanga kuwajeruhi watu na Jeshi la Polisi tuliongea na wenyeviti wa mtaa na mabalozi tumekubaliana hali hiyo haiwezi kuendelea lazima watapambana na mkono wa chuma vijana wanaojihusisha na matukio hayoa” amesema

Amesema mbali na vijana hao kuiba mali za watu katika tukio hilo la Chanika waliwajeruhi watu 23 kwa kuwakata mapanga sehemu mbalimbali na wengi wao wapo hospitali wakiendelea na matibabu.

“vijana hao ni wadogo wamekamatwa na wameongea mambo mengi naamini kulingana na uchunguzi tunaendelea kuufanya tutafika pazuri,”amesema

Katika hatua nyingine Jeshi hilo limemkamata mtu mmoja kwa tuhuma za kuwaua watu wawili waliokuwa wanajishughulisha na kazi ya bodaboda maeneo ya Kigamboni.

Amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa kupitia operesheni iliyoanza kufanyika Aprili Mosi mwaka huu hadi jana ambapo wamemhojiwa kwa kina na kukiri kutekeleza tukio hilo pamoja na wenzake wawili.

”Aprili 16 mwaka huu eneo la Mlandege Kigamboni walimkodi kijana huyo wakiwa safarini walimpiga na kitu kizito na kupoteza maisha na kufanikiwa kupora pikipiki yake na kuondoka nayo hadi maeneo ya Rufiji walikokamatwa na Polisi,”amesema

Mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake wawili walikiri Agosti 27 mwaka jana walimkodi kijana mwingine kwenye maeneo hayo ambaye alikuwa hafahamiki alipo hadi wanakamatwa.

“Lakini baada ya kuwakamata wamekiri kuhusika na tukio hilo la kumkodi kijana huyo na kumuua na kwenda kumutupa maeneo hayo hayo ya Kigamboni,”amesema

Watuhumiwa hao baada ya kuhojiwa walionesha hadi sehemu ilipo pikipiki ya marehemu aliyeuawa Agosti 27 mwaka jana na kwenda kuonesha walipoenda kutupa mwili wake.

“Tulipofika pale tuliona mifupa na fuvu linalodhaniwa kuwa la binadamu hata hivyo uchunguzi bado unaendelea na ukikamilika watuhumiwa watafikishwa kwenye vyombo vya dola,”amesema

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
Ally Hamis Zingizi

Ally Hamis Zingizi

Related Posts

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION  KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA
HABARI

TAASISI YA GREEN KIDS AND YOUTH FOUNDATION KUENDELEZA MAHUSIANO BORA NA WADAU KATIKA KUTETEA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

by Ally Hamis Zingizi
Mar 27, 2023
NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
HABARI

NALA kuwekeza zaidi ya Sh. Bilioni 2 baada ya kupata leseni ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

by I am Krantz
Mar 27, 2023
Naibu Waziri   aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya  michezo
HABARI

Naibu Waziri aipongeza Benki ya NBC kwa kusaidia maendeleo ya michezo

by I am Krantz
Mar 27, 2023
MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA
HABARI

MZEE WA MIAKA 92 AFUNGA NDOA YA TANO MWAKA MMOJA BAADA YA NDOA NNE KUVUNJIKA

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14
HABARI

BAKWATA YASHIKILIA MSIMAMO NDOA MIAKA 14

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023
MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL
HABARI

MOURINHO KOCHA BORA WA KARNE – ÖZIL

by Shabani Rapwi
Mar 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In