ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Wednesday, March 22, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

Wadau Wamshangaa Hamonize Kuangaika na Kajala, Huku Diamond Akipenya Ulaya

I am Krantz by I am Krantz
Apr 29, 2022
in HABARI
0
0
SHARES
199
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Harmonize akiwa na aliyekuwa mpenzi wake kajala kabla ya kutengana

Diamond Platnumz.

KAMA ilivyo kawaida, kwenye maisha, kila mtu ana nafasi au zamu yake ya kung’ara na kutaradadi. Ndivyo ilivyo katika maisha ya kila mtu, haijalishi taaluma.

RelatedPosts

MECHI ZITASIMAMA EPL KUPISHA ‘IFTAR’

MECHI ZITASIMAMA EPL KUPISHA ‘IFTAR’

Mar 21, 2023

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI

Mar 21, 2023

MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA

Mar 21, 2023
Load More

Katika ukanda wa Afrika mashariki, tasnia ya muziki ndiyo inaendelea kukua kila uchao, huku wasanii wapya wakikaribishwa kwenye tasnia hiyo kila siku.

Itakumbukwa tangu enzi za miaka ya 2000, kulikuwa na wasanii wengi, tena wazuri na wenye vipaji vikubwa na sauti tamu za kuimba na walijua kutunga mashairi, lakini wote hao kama ilivyo kawaida walitisha kwa muda wao na kunyauka kama vile maua.

Tasnia ya muziki nchini Tanzania kwa mfano; kulikuwa wasanii wazuri kama Mr Nice, Juma Nature, AY na wengine.

Ni uongo kusema hawakutisha na kuvuka mipaka mpaka kuijenga heshima ya majina yao katika mawimbi ya mataifa jirani.

Lakini pia muda wao wa kuondoka kwenye steji ulipofika walisepa na kuwapisha wasanii wapya kama kina King Kiba, Diamond Platnumz na wengine wengi ambao wameendeleza gurudumu hilo mpaka hivi sasa.

Hawa pia ni binadamu na muda wao bila shaka utafika, sasa mijadala mitandaoni ni kuhusu wale watakaovalia viatu vya wasanii wakubwa kwa mfano Diamond pindi mchezo wake wa usanii utakapomuonesha taa nyekundu.

Baada ya kutathmini kwa muda, wengi wanampigia upatu msanii Harmonize kuliziba pengo litakaloachwa na Diamond wakati atashuka viwango vya muziki mzuri.

Lakini pia licha na Harmonize kupigiwa upato, bado ana kazi kubwa sana ya kuifanya.

Kwa mujibu wa mdau mmoja anayekwenda kwa jina Hope Tyga kwenye Instagram, Harmonize ana mambo mengi tu anayostahili kuyazingatia ili kurithi nafasi ya Diamond kimuziki.

Tyga anaamini ipo siku moja tu ambapo Harmonize atampindua Diamond na umaarufu pamoja na utajiri wake utazidi hata ule wa sasa wa Diamond, ila kuna mambo ambayo yanayomhusu Harmonize kama anapania kupiku rekodi za Diamond.

Kwanza anasema asitegemee huruma ya Watanzania; Harmonize aache kuanika mabaya ya Diamond ili tu Watanzania wamuonee Huruma, afunge domo lake asimuongelee

vibaya Diamond. Hii itamsaidia kupata mashabiki wengi zaidi.

Pia Harmonize anatakiwa akubali kwamba Diamond ana mchango mkubwa kwenye muziki wake.

ADVERTISEMENT

Hata hivyo, Harmonize anakiri kabisa kwamba bila Diamond yeye asingekuwa hapo. Hii ni nzuri sana na inabidi asisahau kabisa umuhimu wa Diamond, hii pia itamsaidia kupata mashabiki na baraka tele.

Baada ya hapo anapaswa kupunguza kiki za kishamaba. Harmonize au Harmo asiendekeze kiki za kijinga, zinampotezea sana mashabiki. Pia watu wengi wataanza kumpuuza na wamuone kama mtoto vile, afanye kazi, asiendekeze kiki.

Harmonize anapaswa akomae kifikra. Kuna kolabo Harmonize anafanya ambazo hazina faida. Mfano; ile ya Mabantu na Omoyo; yaani alionekana kukurupuka na inabidi aangalie kimataifa zaidi, asiendelee kunga’nga’na hapahapa Tanzania.

Diamond aliamua kabisa kuvuka boda na akafanikiwa kweli hivyo Harmonize afuate nyayo hizohizo.

ADVERTISEMENT

Yafaa kabisa, Harmonize asiwe kama yule mfalme. Yaani katika vitu muhimu kabisa, isije ikatokea Harmonize akawa na bifu zito na Diamond kama ambavyo King Kiba na Diamond walivyo.

Ikibidi Harmonize amalize bifu kabisa na Diamond, maana Diamond ana mashabiki wengi, ukijenga naye bifu, watu wake kibao watakukataa na hutaendelea kimuziki hivyo Harmonize afanye juu chini bifu lake na Diamond lisiwe kubwa.

Hivi unajua tofauti kubwa kati ya Diamond na Harmonize, hasa katika kipindi hiki ambapo wengi wanajaribu kuwafananisha wawili hao kutoka mafanikio ya kimuziki, maisha, fasheni na utajiri?

Wengi wanajiuliza mbona Diamond ametia fora sana katika kutawala sanaa ya Bongo kimuziki kwa miongo kadhaa bila kufifia kama wenzake walioanza nao, lakini je, wamewahi kujiuliza ni nini kinamfanya Diamond kuzidisha umaarufu wake kutoka kwa vizazi vya jana hadi vizazi vya leo?

Majibu yote haya utayapata katika makala f’lani ambayo imeandikwa na mdau huyo aitwaye Hope Tyga kuhusu ni kwa nini itamgharimu Harmonize muda mwingi wa kujifunza kutoka kwa Diamond ili kumfikia katika ufanisi.

Kwa mujibu wa jamaa huyo, wakati Diamond ameelekea Ulaya katika shughuli rasmi za kimuziki, Harmonize bado yupo nyumbani anazidi kulilia mapenzi na kumfuata mwanamke ambaye hamtaki, nazungumzia Harmonize akizidi kumfuata Kajala Masanja kumrudia kimapenzi.

Tunaona hivi sasa Diamond yupo Bara la Ulaya, hajaenda kwa ajili ya kutalii, ameenda kikazi zaidi, tunaamini safari yake hii italeta faida kubwa katika muziki wake na biashara zake kwa jumla.

Wakati Diamond akipambana ili muziki wake upenye barani Ulaya tunamuona Harmonize akiwa Bongo anapoteza muda tu, yeye kila siku ni kulialia tu, mara aombe msamaha kwa Kajala, ni vituko tu.

Mdau huyo anazidi kumtaka Harmonize kuachana na kukimbizana na wanawake kwani hayo ni mambo ya kupita tu na badala yake kuelekeza muda wake mwingi katika kuipalilia nyota yake kwani asipofanikiwa atasahau kwamba hakutia bidi na kusingizia ulozi.

Hii ni tahadhari ili baadaye asipofanikiwa asilaumu kwamba anarogwa, wakati ukweli unaonesha kabisa kijana siyo mchapakazi, yeye anawaza wanawake tu, hana anachowaza zaidi.

Mwenzake Diamond amelamba ubalozi wa simu, yeye hajapata hata ubalozi wa chaki kwa sababu anajiita Teacher Konde.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI
HABARI

AFUNGIWA MIAKA 40 KUTOINGIA UWANJANI

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA
HABARI

MWANAFUNZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI KENYA

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI WATOA MWILI WA MAREHEMU NA KUONDOKA NA SEHEMU ZA SIRI
HABARI

WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI WATOA MWILI WA MAREHEMU NA KUONDOKA NA SEHEMU ZA SIRI

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
BIKIRA JANE APATA MTOTO
HABARI

BIKIRA JANE APATA MTOTO

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023
ASKARI ANAYETUHUMIWA KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE ASOMEWA MASHTAKA
HABARI

ASKARI ANAYETUHUMIWA KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE ASOMEWA MASHTAKA

by ALFRED MTEWELE
Mar 21, 2023
SEVILLA YAMFUTA KAZI KOCHA JORGE SAMPOLI NA KUMTEUA KOCHA HUYO
HABARI

SEVILLA YAMFUTA KAZI KOCHA JORGE SAMPOLI NA KUMTEUA KOCHA HUYO

by Shabani Rapwi
Mar 21, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
April 2022
M T W T F S S
 123
45678910
11121314151617
18192021222324
252627282930  
« Mar   May »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In