ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Day: May 20, 2022

TFS KANDA YA KUSINI YAPANIA KURUDISHA UOTO WA ASILI MIKOA YA LINDI,MTWARA NA RUVUMA

Na Muhidin Amri, Masasi ZAIDI ya miti milioni 4.3 imepandwa na Wakala wa huduma za misitu Tanzania(TFS)kanda ya kusini kuanzia Mwezi Disemba hadi April  2022 huku miti takribani milioni 2 ikigawiwa kwa  taasisi za Serikali ikiwamo  shule za msingi,Sekondari na Wananchi. Hayo yamesemwa jana na Kamanda wa TFS Kanda ya Kusini Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Uhifadhi wa misitu Manyise Mpokigwa,wakati akizungumzia kuhusu kampeni ya upandaji miti inayofanywa na TFS katika mikoa ya Kusini. Mpokigwa alisema,kanda ya kusini yenye mikoa ya Lindi,Mtwara na Ruvuma ina mashamba ya miti ambako katika mkoa  wa Ruvuma mashamba hayo ni Wino na Mpepo ambako wameotesha miti laini  kwa ajili ya kupandwa katika mashamba yao na kugawa kwa taasisi za Serikali. Alisema, TFS inasimamia aina mbili za misitu ambayo ni miti ya kupandwa na miti ya asili ambapo katika mkoa wa Ruvuma asilimia kubwa ya miti ni ya kupandwa ikilinganishwa na mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo miti yake ni ya asili pamoja na miti michache ya kupandwa inayostahimili sana katika ukanda wa joto kama vile mitiki. Alisema,katika bustani ya miti Ruangwa mkoani Lindi miti iliyozalishwa iligawiwa kwa Halmashauri zote zilizopo katika mkoa huo na wananchi na katika bustani ya Newala mkoani Mtwara miche iliyozalishwa kwa wingi ni ya matunda,miti ya vivuli,mitiki,mkongo na mpingo. Alisema,TFS inapanda miti kwa malengo mbalimbali kama kurejesha uoto mahali ulipopotea,kubadili mitazamo ya watu kuhusu misitu na miti na wanahimiza  jamii kupanda miti ili kupata mazao ya miti toka vyanzo vyao kwa ajili ya kupunguza kutegemea misitu ya asili. Alisema,wana jukumu la kusimamia na kulinda rasilimali za misitu kwa ajili ya faida ya vizazi vya sasa na  vinavyokuja,hivyo ni jukumu ya kila Mtanzania kupanda miti iwe ya mbao,matunda au kivuli kwani kufanya hivyo kutasaidia sana uwepo wa misitu ambayo faida zake ni nyingi. Alisema,kuna sababu kwa Watanzania kuendelea kupanda miti katika maeneo mbalimbali ili kukabiliana na kasi ya uharibifu wa mazingira inayoendelea kufanywa na baadhi ya watu. Alisema, katika msimu wa  mwaka 2020/2021 jumla ya miche ya miti milioni 4 kati ya hiyo miche zaidi ya milioni 2 iligawiwa kwa wananchi na taasisi za Serikali na Dini kama mkakati wa TFS kupanda miti kibiashara. Alisema, tathimini ya maendeleo ya miti iliyopandwa mwaka 2020/2021 iliyofanyika hivi karibuni imebaini kuwa, miti mingi iliyogawiwa  na kuoteshwa na wadau mbalimbali imeota vizuri kwa asilimia 75 na michache imeshindwa kuota kutokana na hali ya hewa. Alieleza kuwa,ile iliyopandwa kwenye  taasisi kama shule ilishindwa kuendelea kutokana na janga la Covid-19 ambapo wahudumiaji ambao ni wanafunzi hawakuwepo shuleni hivyo kushindwa kuhudumiwa vizuri. Alisema,katika  kazi zao wanashirikiana kwa karibu na jamii na taasisi za Serikali ambapo mwaka 2021 TFS ilitoa zaidi ya mizinga  50 ya nyuki kwa wananchi katika Tarafa  za Mchinga na Mtama. Alisema, mizinga hiyo imetumika kama sehemu ya kuzuia wanyama waharibifu kama Tembo wanaovamia mashamba na kuharibu mazao na kuvuna asali kwa ajili ya kuwapatia wananchi  kipato. Alisema, katika wilaya ya Songea mkoa wa Ruvuma wamegawa mizinga ya nyuki 100 kwa vikundi vinne vinavyojihusisha na ufugaji nyuki katika maeneo mbalimbali. ...

Read more

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

Welcome Back!

Login to your account below

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.