ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Thursday, November 30, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

ASKARI WA JESHI LA ZIMAMOTO ANUSURIKA KICHAPO BAADA YA KUFIKA NA BODABODA BILA GARI LA KUZIMIA MOTO NYUMBA IKIUNGUA MOTO

Shabani Rapwi by Shabani Rapwi
May 11, 2022
in HABARI
0
ASKARI WA JESHI LA ZIMAMOTO ANUSURIKA KICHAPO BAADA YA KUFIKA NA BODABODA BILA GARI LA KUZIMIA MOTO NYUMBA IKIUNGUA MOTO
0
SHARES
389
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

Watu nane wamenusiurika kifo wakati nyumba ambayo wanaishi mtaa wa Mwinamila Kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga ikiungua moto na kuteketeza kila kitu ndani. Tukio hilo limetokea leo jioni Jumanne Mei 10,2022.

–

Fred Paulo ambaye ni mtoto katika nyumba hiyo, amesema kuwa ilipofika majira ya saa 11 jioni, alitoka nje kwenda kununua vocha huku simu yake akiwa ameiacha kwenye chaji, aliporudi ndipo akaona moto unawaka ndani.

–

Amesema moto huo ulianza kushika kwenye sofa, ndipo ikabidi akimbie kwenda kuzima umeme (Main Switch), na kuanza kuomba msaada kwa wasamaria wema kusaidia kuuzima moto huo, na kufanikiwa kuuzima huku ukiwa tayari umeshateketeza kila kitu ndani, lakini nyumba yao ikisalimika kuteketea.

 

“Kwenye hii nyumba tunaishi jumla ya watu nane wakiwamo na wapangaji, na huu moto ulianza kuwaka kwenye chumba changu, nashukuru Mungu nyumba haijateketea yote bali zimepotea samani zote za ndani,”anasema Paul.

–

Naye shuhuda wa tukio hilo la Moto Oscar Kunze, amesema alikuwa amekaa jirani na nyumba hiyo akimsubiri mtu, lakini akasikia kelele nyumba hiyo inaungua moto, ndipo alipofika eneo la tukio na kuanza kusaidia kuuzima, huku watu wengine wakiendelea kwenda na kufanikiwa kuuzima.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa huo wa Mwanamila eneo ambalo nyumba imeungua moto Lukia Athumani, amewapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi na kuokoa nyumba hiyo isiteketee kwa moto, huku akilitupia lawama Jeshi la Zimamoto na uokoaji kwa kuchelewa kufika eneo la tukio, na moto huo kuzimwa na wananchi.

ADVERTISEMENT

–

Amesema amesikitishwa na Jeshi la Zimamoto na uokoaji kwa kutopokea simu kwa wakati, na baada ya kupata taarifa hawakwenda kwa haraka na kuchelewa kufika eneo la tukio, na walipofika walikuwa wamepanda kwenye bodaboda bila ya kuwa na gari, na kusababisha wananchi kutaka kuwashushia kichapo lakini alizuia tukio hilo.

–

Naye Afisa wa Zimamoto ambaye alinusurika kichapo kutoka kwa wananchi ambaye hakutaka kutaja jina lake, amesema Jeshi hilo linakabiliwa na uhaba wa magari ya kuzimia moto.

Related

ADVERTISEMENT
Shabani Rapwi

Shabani Rapwi

Related Posts

Tuliishi maisha ya shida sana kisa uchawi wa jirani!
HABARI

Tuliishi maisha ya shida sana kisa uchawi wa jirani!

by I am Krantz
Nov 30, 2023
EACOP Yakamilisha Utaratibu Wa Fidia Kwa Kukabidhi Nyumba Ya 339 Mkoani Tanga
HABARI

EACOP Yakamilisha Utaratibu Wa Fidia Kwa Kukabidhi Nyumba Ya 339 Mkoani Tanga

by I am Krantz
Nov 29, 2023
MAWAKALA WA USAJILI WA VODACOM TANZANIA WATEMBELEA AFRIKA YA KUSINI KUTOKANA NA UTENDAJI BORA WA KAZI.
HABARI

MAWAKALA WA USAJILI WA VODACOM TANZANIA WATEMBELEA AFRIKA YA KUSINI KUTOKANA NA UTENDAJI BORA WA KAZI.

by I am Krantz
Nov 29, 2023
NMB, Oryx Tanzania wazindua ‘Moto Mkali Bei Poa,’ kukopesha gesi ya kupikia
HABARI

NMB, Oryx Tanzania wazindua ‘Moto Mkali Bei Poa,’ kukopesha gesi ya kupikia

by I am Krantz
Nov 27, 2023
Kampeni Ya Serengeti Maokoto Ndani Ya Kizibo Yazidi Kusambaza Furaha Kwa Watanzania
HABARI

Kampeni Ya Serengeti Maokoto Ndani Ya Kizibo Yazidi Kusambaza Furaha Kwa Watanzania

by I am Krantz
Nov 27, 2023
NMB Mlipa Kodi Mkubwa na Bora Zaidi Tanzania 2023 🇹🇿
HABARI

NMB Mlipa Kodi Mkubwa na Bora Zaidi Tanzania 2023 🇹🇿

by I am Krantz
Nov 27, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TWEETS

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In