ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Wednesday, June 29, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

KUWA MAKINI NA HILI LASIVYO UTAKUWA UNALIA KILA SIKU KWENYE MAPENZI

Shabani Rapwi by Shabani Rapwi
May 20, 2022
in HABARI
0
KUWA MAKINI NA HILI LASIVYO UTAKUWA UNALIA KILA SIKU KWENYE MAPENZI
0
SHARES
123
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

 

RelatedPosts

R KELLY AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA

R KELLY AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA

Jun 29, 2022

POLISI 156 WAFUKUZWA MAFUNZONI

Jun 29, 2022

VIGOGO WA CHAMA CHA WALIMU WAHUKUMIWA MIEZI 6 JELA

Jun 29, 2022
Load More

Ukiwa mtu wa kuangalia mambo kwa juu juu basi kila kitu kwako kitakuwa kigumu. Kusoma unaweza kuona ni kugumu, kufanya kazi kugumu, hata kusubiri mshahara unaweza kuona ni kugumu.

Urahisi kwako unaweza kuwa katika kutumia pesa, pengine  na kula tu. Ila watu waerevu na wenye uvumilivu kwako kila kitu kinaweza kuwa tofauti na wewe.

1. Unachoona kigumu kwao wanahisi si ugumu bali ni changamoto za kuzidisha jitihada na umakini tu. Kwenye mapenzi pia hali haiko tofauti sana. Wale wanao achana kila siku si kama ndiyo wanakosewa sana kuliko wale ambao hawaachani, hapana. Suala ni lile lile tu.

2. Wakati wengine wakiona tofauti zao ni kama changamoto za kusomana tabia na kuamua kuishi kutokana na kila mmoja kumjua mwenzake. Wenzao wanaona suluhisho la yote ni kila mmoja kuwa na maisha yake. Suala la uvumilivu kwao hamna.

3. Hakuna mapenzi duniani yanayoweza kushamiri bila suala hili. Usipokuwa na moyo wa uvumilivu katika mapenzi basi kila mtu utamuona hafai. Utamuona hafai na kila siku utakuwa mtu wa kuanzisha mahusiano mapya. Hayo si maisha sasa!

4. Mahusiano yaliyodumu si kwa kuwa wahusika hawakoseani au makosa wanayokoseana ni madogo sana. Hapana. Kila binaadamu ana mapungufu yake. Wote huwa wanakoseana ila tofauti yake na wengine ni kwamba busara na uvumilivu huwa msingi wa mapenzi yao na ndiyo maana tunaona wanadumu mpaka leo.

ADVERTISEMENT

 

5. Ni binaadamu gani unaweza kuishi naye na msikosane? Ni nani mwenye uwezo wa kukupa unachotaka kila siku? Hakuna binaadamu wa aina hiyo.

6. Hivyo unavyotaka kuachana na uliye naye suala la kujiuliza ni kuwa mara ngapi umemueleza kuhusiana na suala unalotaka kumuachia. Na hiyo isitoshte tu pia jiulize ni sababu gani inayomfanya kutenda suala hilo. Ukimaliza hapo rudi nyuma na jiulize tena huwa unatumia maneno ya aina gani katika kumkanya.

7. Maana wengine baada ya kukosewa wao huwa hawawakanyi vyema wenzao wao bali huripuka kwa maneno makali na dharau. Matokeo yake sasa wahusika badala ya kuwasikiliza na kufanyia kazi maneno wanayoambiwa kutokana na makosa yao. wao huwapuuzia na kwaona ni wasema hovyo.

8. Ndiyo, kukosewa kunaumiza sana ila jiulize ni kitu gani kimetokea bila sababu? Kwenye makosa ya mpenzi wako kuna sababu nyuma yake, hebu itafute badala ya kulalamika.

ADVERTISEMENT

9. Mapenzi yasiyo kuwa na uvumilivu ndani yake hayana maisha marefu. Kwa sababu binaadamu ni kiumbe mwenye kukosea.

10 Badala ya kukimbilia kuachana ebu geuka kuwa mwalimu wa mpenzi wako angalau kwa mara chache.

11. Mpenzi wako ni furaha yako kwa maana ndiyo mtu uliyeridhia naye kuwa naye katika masuala nyeti yahusuyo maisha yako. Sasa kwanini uwe tayari kumpoteza kisa kachelewa kurudi.

 

12. Kuwa mvumilivu . Watu wenye hekima ni wavumilivu. Watu wenye kujielewa ni wavumilivu.

13. Ukiwa hauna uvumuilivu kila siku utatangaza ndoa. Leo utaachana na Mugambara kwa sababu anaongea sana na wasichana ila, jua huyo unaeenda kuwa naye anapenda sana kitu ambacho hukipendi. Anakunywa pombe je, utawezana naye? Jibu unalo.

14. Kwa kuwa huyo uliye naye unampenda kwa dhati basi amua kwenda naye taratibu ukijitahidi kumbadilisha tabia zake. Usiogope, inawezekana, suala ni uvumilivu na kujiamini tu. Kukubali kumpoteza unayempenda kwa kukosa uvumilivu ni kujitakia kuingia katika maisha ya kutanga tanga tu.

15. Kumbuka, siku zote wanaovumilia ndiyo huwa wanabaki na ushindi.Bila uvumilivu Mandela asingekuja kuwa raisi wa afrika kusini.Uvumilivu ni kila kitu katika maisha.

Related

ADVERTISEMENT
Shabani Rapwi

Shabani Rapwi

Shabani Rapwi (Kijana Mchapa Kazi) WhatsApp; 0689232546 Email ;shabanimohamed932@gmail.com

Related Posts

R KELLY AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA
HABARI

R KELLY AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022
POLISI 156 WAFUKUZWA MAFUNZONI
HABARI

POLISI 156 WAFUKUZWA MAFUNZONI

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022
VIGOGO WA CHAMA CHA WALIMU WAHUKUMIWA MIEZI 6 JELA
HABARI

VIGOGO WA CHAMA CHA WALIMU WAHUKUMIWA MIEZI 6 JELA

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022
MAHAKAMA YATOA AMRI KESI HALIMA MDEE NA WENZAKE
HABARI

MAHAKAMA YATOA AMRI KESI HALIMA MDEE NA WENZAKE

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022
RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI HUU
HABARI

RAIS SAMIA ATEUA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022
MPOLE AMFUNIKA MAYELE LIGI KUU YA NBC 2021/22
HABARI

MPOLE AMFUNIKA MAYELE LIGI KUU YA NBC 2021/22

by Shabani Rapwi
Jun 29, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In