ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

MGODI WA BULYANHULU WAKABIDHI TREKTA WILAYANI NYANG’ HWALE KUFANIKISHA OPERESHENI YA USAFI WA MAZINGIRA

I am Krantz by I am Krantz
May 8, 2022
in HABARI
0
MGODI WA BULYANHULU WAKABIDHI TREKTA WILAYANI NYANG’ HWALE KUFANIKISHA OPERESHENI YA USAFI WA MAZINGIRA
0
SHARES
220
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

Mar 24, 2023

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

Mar 24, 2023

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

Mar 24, 2023
Load More
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale ,Jamhuri David, (katikati waliokaa juu ya trekta mwenye miwani) akiwaongoza maofisa wa wilaya hiyo na Wananchi kupokea Trekta la kusomba taka lililotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu.
**

Wananchi wakazi wa wilaya ya Nyang’hwale, ambao walikuwa hatarini kukumbwa na milipuko ya magonjwa kutokana na mlundikano wa takataka katika maeneo yao sasa wamepata ahueni kutokana na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, kukabidhi trekta ya kusomba taka kwa Halmashauri ya Wilaya hiyo yenye thamani ya shilingi milioni 78 kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (CSR).


Akiongea katika hafla ya kukabidhiwa trekta hiyo, Afisa Mazingira wa Wilaya ,Ezekiel Ntiryo, alisema “Tunaishukuru kampuni ya Barrick Bulyanhulu, kwa Msaada huu wa Trekta , tunaamini sasa hali ya usafi katika Wilaya yetu itaboreka kwa kiasi kikubwa,kwani matarajio yetu ni kuondoa taka mara mbili kwa wiki katika siku za Alhamisi na Jumatatu pia tunatarajia kuongeza huduma kwa maeneo ya miji inayokuwa kwa kasi kibiashara kama vile Bosolwa, Nyijundu, Bukwimba na Maeneo ya migodini.Kabla ya msaada huu wa Trekta hali ya Uzoaji wa Taka katika mitaa yetu ilikuwa chini ya asilimia 15% lakini baada ya msaada huu itafikia asilimia 65% iwapo tutaongeza juhudi.”

Mkuu wa Wilaya hiyo,Jamhuri David ,aliishukuru Barrick Bulyanhulu kwa kuunga mkono jitihada za Serikali za kuleta maendeleo kwa Wananchi kupitia fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (CSR), ambazo zimechangia kufanikisha miradi mingi ya maendeleo Wilayani humo na kufanya maisha ya wananchi kuwa bora.

“Leo tupo hapa kupokea Trekta ambalo limenunuliwa na kampuni ya Barrick Bulyanhulu, kwa gharama ya Shilingi Milioni 78, Trekta hili ni maalum kwa kazi ya kuzoa uchafu na kupeleka dampo, kwa kweli ni msaada mkubwa kwa wilaya yetu kwani kwa miaka mingi sana tumekuwa na changamoto juu ya uzoaji wa taka katika mitaa yetu ukichukulia kwamba mji wetu unakua kwa kasi na kupelekea uzalishaji wa taka kuongezeka kwa kiasi, ni matarajio yangu sasa mazingira ya Wilaya yetu yatakuwa safi, nichukue fursa hii kuwaomba wananchi kufanya usafi kila siku kwani tayari kwa sasa tunalo trekta ambalo litakuwa linasomba taka mara kwa mara”, alisema.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Bulyanhulu, William Chungu, alitoa shukrani kwa viongozi wa Serikali na Wananchi kwa kuwa na uhusiano mzuri na Kampuni hiyo na kuongeza kuwa msaada wa Trekta lililokabidhiwa ni kwa ajili ya kusafisha mazingira. 

“Niwaombe ndugu zangu usafi ni jukumu letu sote,trekta hili tulitunze ili liweze kuboresha mazingira yetu ipasavyo ,milioni 78 ni pesa nyingi hivyo naamini tutakuwa tumefungua njia ya kuboresha mazingira ya usafi wilayani Nyang’hwale, haswa ikizingatia kampuni ya Barrick ni wadau wakubwa wa utunzaji wa mazingira”, alisisitiza Chungu.
Mwonekano wa Trekta mpya ya kusomba taka iliyotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa Halmashauri ya Nyang’hwale kwa ajili ya kufanikisha zoezi la kusafisha Mazingira.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale ,Jamhuri David,(kulia) akishiriki zoezi la kuzoa taka baada ya kupokea trekta la kusomba taka lililotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu.
Wafanyakazi wa Barrick wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Wananchi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Wananchi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Wafanyakazi wa Barrick wakifuatilia matukio katika hafla hiyo

ADVERTISEMENT
ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE
HABARI

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA
HABARI

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII
HABARI

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI
HABARI

WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI
HABARI

MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC
HABARI

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC

by I am Krantz
Mar 24, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In