ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, July 2, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

I am Krantz by I am Krantz
May 19, 2022
in HABARI
0
0
SHARES
35
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

  • Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna (wa pili kushoto), akizindua rasmi  dirisha la kupokea maombi ya ufadhili wa wanafunzi wanaotegemea kuingia kidato cha tano mwaka huu na wale wanaotarajia kuingia vyuo vikuu kwa ajili ya shahada ya kwanza ya masomo. Kushoto ni mjumbe wa Bodi, Juma Kimori na kulia ni Katibu wa NMB Foundation, Consolata Mosha na mjumbe wa Bodi, Filbert Mponzi.

RelatedPosts

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

Jul 2, 2022

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

Jul 2, 2022

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

Jul 2, 2022
Load More

Taasisi ya NMB Foundation imetangaza kuanza rasmi utaratibu wa kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa kidato cha tano, sita na elimu ya juu baada ya programu hiyo kuzinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mwishoni mwa mwaka jana

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna amesema wameanza kupokea maombi kupitia matawi yote ya benki hiyo yaliyopo nchi nzima na tovuti ya NMB Foundation.

“Kwa kuanzia tutatoa ufadhili kwa wanafunzi 200, ambapo 150 watakuwa wa kidato cha tano na sita, wanafunzi 50 watakuwa wa elimu ya juu. Fadhili utalipia gharama zote za masomo ikiwemo ada, fedha za kujikimu, vifaa na mahitaji mengine yatakayotajwa kweye fomu ya kujiunga na shule au chuo,” amesema Ruth.

Alifafanua kuwa kwa wanfunza wa sekondari watakaopata ufadhili watalipiwa ada, nauli, vifaa vya kujifunzia, fedha za kujikimu, bima ya afya na mahitaji mengie watakayotakiwa kutoka shule. Kwa upande wa elimu ya juu, wanafunzi watalipwa ada, fedha za kujikimu, fedha za mafunzo kwavitedo, Laptop na gharama nyingine watakazotakiwa kwenye fomu ya kujiunga na chuo.

Aidha, Zaipuna alisema wamejipanga kuweka masomo ya vipaumbele kwa wanafunzi watakaopata fursa ya udhamini. Lengo ni kuhakikisha wanashiriki mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kupitia malezi na mafunzo watakayopata wanafunzi hao.“

ADVERTISEMENT

Tutaangalia kwa kina masomo ya takwimu na mahesabu, biashara na uchumi, Teknolojia ya Mawasiliano ya Umma, uhandisi, mafuta na gesi pamoja na sayansi na teknolojia,” alibainisha Zaipuna na kuongeza:

“Nina imani kupitia programu hii tutaibua vipajij na tutatimiza ndoto za vijana. Kadiri tutakavyoendelea idadi ya wanafunzi watakaonufaika itaongezeka kulingana na mahitaji ambapo tutapanua wigo wa wadau wengine watakaotaka kushirikiana nasi kwenye jambo hili muhimu kwa maendeleo ya nchi.”

Katika hatua nyingine, Ruth alisema NMB Foundation itahakikisha watu watakaohusika kukusanya na kupitisha wanafunzi wanaofaa kwa kupewa ufadhili watakuwa makini kutimiza vigezo, ambapo kwa wale watakaokwenda kinyume na utaratibu watachukuliwa hatua za kinidhamu.

“Tunataka kulifanya zoezi hili liwe na uwazi na ukweli, ndio maana tumesema tutawashirikisha hata viongozi wa serikali za mitaa kuanzia kata hadi mitaa, lengo ni kuhakikisha wanufaika watakaopatikana ni kweli wana vigezo vinavyohitajka,” alisisitiza Zaipuna.

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI
HABARI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
NEYMAR KUONDOKA PSG
HABARI

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.
BIASHARA

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

by I am Krantz
Jul 2, 2022
AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNASA KWENYE NYAYA ZA UMEME
HABARI

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNASA KWENYE NYAYA ZA UMEME

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022
MTUMISHI WA TANESCO AKUTWA GUEST AMEFARIKI
HABARI

MTUMISHI WA TANESCO AKUTWA GUEST AMEFARIKI

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022
SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA JULAI 10, 2022
HABARI

SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA JULAI 10, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In