ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Friday, March 24, 2023
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

NMB FOUNDATION YATANGAZA UFADHILI SEKONDARI KIDATO CHA TANO , SITA NA ELIMU YA JUU

I am Krantz by I am Krantz
May 19, 2022
in HABARI
0
0
SHARES
93
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

  • Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna (wa pili kushoto), akizindua rasmi  dirisha la kupokea maombi ya ufadhili wa wanafunzi wanaotegemea kuingia kidato cha tano mwaka huu na wale wanaotarajia kuingia vyuo vikuu kwa ajili ya shahada ya kwanza ya masomo. Kushoto ni mjumbe wa Bodi, Juma Kimori na kulia ni Katibu wa NMB Foundation, Consolata Mosha na mjumbe wa Bodi, Filbert Mponzi.

RelatedPosts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

Mar 24, 2023

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

Mar 24, 2023

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

Mar 24, 2023
Load More

Taasisi ya NMB Foundation imetangaza kuanza rasmi utaratibu wa kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa kidato cha tano, sita na elimu ya juu baada ya programu hiyo kuzinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mwishoni mwa mwaka jana

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Bodi ya NMB Foundation, Ruth Zaipuna amesema wameanza kupokea maombi kupitia matawi yote ya benki hiyo yaliyopo nchi nzima na tovuti ya NMB Foundation.

“Kwa kuanzia tutatoa ufadhili kwa wanafunzi 200, ambapo 150 watakuwa wa kidato cha tano na sita, wanafunzi 50 watakuwa wa elimu ya juu. Fadhili utalipia gharama zote za masomo ikiwemo ada, fedha za kujikimu, vifaa na mahitaji mengine yatakayotajwa kweye fomu ya kujiunga na shule au chuo,” amesema Ruth.

Alifafanua kuwa kwa wanfunza wa sekondari watakaopata ufadhili watalipiwa ada, nauli, vifaa vya kujifunzia, fedha za kujikimu, bima ya afya na mahitaji mengie watakayotakiwa kutoka shule. Kwa upande wa elimu ya juu, wanafunzi watalipwa ada, fedha za kujikimu, fedha za mafunzo kwavitedo, Laptop na gharama nyingine watakazotakiwa kwenye fomu ya kujiunga na chuo.

Aidha, Zaipuna alisema wamejipanga kuweka masomo ya vipaumbele kwa wanafunzi watakaopata fursa ya udhamini. Lengo ni kuhakikisha wanashiriki mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kupitia malezi na mafunzo watakayopata wanafunzi hao.“

Tutaangalia kwa kina masomo ya takwimu na mahesabu, biashara na uchumi, Teknolojia ya Mawasiliano ya Umma, uhandisi, mafuta na gesi pamoja na sayansi na teknolojia,” alibainisha Zaipuna na kuongeza:

“Nina imani kupitia programu hii tutaibua vipajij na tutatimiza ndoto za vijana. Kadiri tutakavyoendelea idadi ya wanafunzi watakaonufaika itaongezeka kulingana na mahitaji ambapo tutapanua wigo wa wadau wengine watakaotaka kushirikiana nasi kwenye jambo hili muhimu kwa maendeleo ya nchi.”

Katika hatua nyingine, Ruth alisema NMB Foundation itahakikisha watu watakaohusika kukusanya na kupitisha wanafunzi wanaofaa kwa kupewa ufadhili watakuwa makini kutimiza vigezo, ambapo kwa wale watakaokwenda kinyume na utaratibu watachukuliwa hatua za kinidhamu.

“Tunataka kulifanya zoezi hili liwe na uwazi na ukweli, ndio maana tumesema tutawashirikisha hata viongozi wa serikali za mitaa kuanzia kata hadi mitaa, lengo ni kuhakikisha wanufaika watakaopatikana ni kweli wana vigezo vinavyohitajka,” alisisitiza Zaipuna.

ADVERTISEMENT

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE
HABARI

BABA MWENYE NYUMBA AFUMANIWA NA MKE WA MPANGAJI WAKE

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA
HABARI

WANAOKULA HADHARANI MCHANA WA RAMADHANI KUKAMATWA

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII
HABARI

HII KALI : KUISHI CHINI YA MAJI SIKU 100 KISA KUTAFUTA REKODI HII

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI
HABARI

WANAUME WANAONYANYUA VITU VIZITO WATAJWA RIJALI ZAIDI

by Shabani Rapwi
Mar 24, 2023
MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI
HABARI

MWALIMU JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MWANAFUNZI

by ALFRED MTEWELE
Mar 24, 2023
BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC
HABARI

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA MKEKA WA USHINDI NA ATM ZA NBC

by I am Krantz
Mar 24, 2023

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In