Rais Samia Suluhu Hassan ametajwa na jarida la Time la nchini Marekani miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi zaidi kwa mwaka 2022.
–
Katika orodha hiyo iliyojumuisha kuanzia wasanii, wafanyabiashara, wabunifu hadi wanasiasa, Rais Samia ameelezewa na Rais Mstaafu wa Liberia na mshindi wa tuzo ya Nobel, Ellen Sirleaf, kuwa kiongozi aliyechochea mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika mwaka mmoja alioiongoza Tanzania.
–
Sirleaf ameeleza kuwa chini ya uongozi wa Rais Samia, mlango wa majadiliano umefunguliwa kwa wapinzani wa kisiasa, hatua zimechukuliwa kurejesha imani katika mfumo wa kidemokrasia, jitihada zimefanyika kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari na waliokatisha masomo wamerejeshwa na wanawake wana mtu wa kumtazama.