ADVERTISEMENT
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv
Saturday, July 2, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result

SERIKALI YAZITAKA TAASISI KUWAJENGEA UWEZO WAKAGUZI WA NDANI

I am Krantz by I am Krantz
May 16, 2022
in HABARI
0
SERIKALI YAZITAKA TAASISI KUWAJENGEA UWEZO WAKAGUZI WA NDANI
0
SHARES
51
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali, Bw. Athumani Mwituka alipokuwa akizungumza kwenye warsha ya wakaguzi wa ndani iliyoandaliwa na Taasisi ya Ukaguzi wa Ndani nchini (IIA), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uelewa wa Wakaguzi wa ndani duniani.

Baadhi ya washiriki kwenye warsha ya wakaguzi wa ndani iliyoandaliwa na Taasisi ya Ukaguzi wa Ndani nchini (IIA), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uelewa wa Wakaguzi wa ndani duniani.


Viongozi wa Meza kuu kwenye warsha ya wakaguzi wa ndani iliyoandaliwa na Taasisi ya Ukaguzi wa Ndani nchini (IIA), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uelewa wa Wakaguzi wa ndani duniani, iliyofanyika mkoani Tanga.


Mwandishi Wetu, Tanga

RelatedPosts

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

Jul 2, 2022

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

Jul 2, 2022

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

Jul 2, 2022
Load More

SERIKALI inategemea kuwa na Wakaguzi 300 wa Mifumo kote nchini katika sekta za Umma ifikapo Mwaka 2026 ili kuhakikisha inaweka udhibiti wa mapato kwenye shughuli zinazofanywa na taasisi zake mbalimbali.

Wakati huo huo imezitaka sekta binafsi kuhakikisha zinatambua umuhimu wa wakaguzi wa ndani na kuwajengea uwezo wakaguzi wao ili waweze kufanya ukaguzi wa mifumo kwa ufanishi, huku wakiwa na vyeti vinavyotambulika kimataifa.

Kauli hiyo, imetolewa juzi jijini Tanga na Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali, Bw. Athumani Mwituka alipokuwa akizungumza kwenye warsha ya wakaguzi wa ndani iliyoandaliwa na Taasisi ya Ukaguzi wa Ndani nchini (IIA), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uelewa wa Wakaguzi wa ndani duniani.

ADVERTISEMENT

Katika warsha hiyo Serikali imeweka wazi mapungufu ambayo hung’amuliwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, CAG na nini kifanyike ili kupunguza hoja za mashaka ndani ya taasisi zao, amewataka wakaguzi hao kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na miongozo ya kimataifa, hivyo wana kila sababu ya kuongeza ujuzi wao kwa manufaa ya taasisi na taifa kwa ujumla.

Alisema kwa kuanzia aupande wa Serikali imeanzisha mifumo mingi ya ukusanyaji mapato ambayo inachangia katika udhibiti matumizi mabaya na pia imechangia kurahisisha utendaji kazi wa shughuli zake.

” Upande wetu serikalini tumejipanga ifikapo Juni 2026 tuwe na wakaguzi wa mifumo kwa sekta za umma takribani 300. Tunatoa wito kwa sekta binafsi nao kuhakikisha inawajengea uwezo wakaguzi wao ili waweze kufanya ukaguzi wa mifumo kwa ufanishi, huku wakiwa na vyeti vinavyotambulika. 

Serikali itaendelea kuongeza uwezo wa wakaguzi wa ndani ikiwemo kufanya ukaguzi wa miradi na tayari Waziri wa Fedha na Uchumi, ametoa maelekezo ya kuwa kila unapobuniwa mradi ndani ya taasisi zake itengwe fedha kwa ajili ya kufanikisha mkaguzi wa ndani kufanya ukaguzi wake. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya IIA, Bi. Zelia Njeza akizungumza alisema taasisi hiyo ya wakaguzi inaungana na wakaguzi wengine duniani kote kusherekea mwezi huu wa wakaguzi wa ndani,  na umejipanga kusherehekea kitofauti zaidi kwa kuhakikisha tunawajengea uwezo wakaguzi wa ndani.

Alisema maadhimisho ya mwaka huu pamoja na kuwajengea uwezo wanachama wao, lakini wamelenga zaidi kujumuika na kusherekea mafanikio ya ukaguzi wao ndani ya taasisi wanazofanyia kazi. 

Alisema bado kunachangamoto ya uelewa wa kazi za wakaguzi wa ndani katika jamii na changamoto hii ya uelewa haipo katika jamii ya Watanzania tu bali hata katika nchi zingine.

ADVERTISEMENT

“…Kwa ujumla ukitofautisha na fani zingine kama udaktari, mtu yeyote ukimuuliza kuhusu daktari atakujibu ni nani…tumekubaliana mwezi huu wa tano uwe ni mwezi maalum kuweza kusherehekea mafanikio yoyote tuliyoyaleta kwa kutumia kazi zetu.

“…Na ni kipindi ambacho tunatumia fursa hii kuweza kuwaelimisha wadau wetu kuhusu umuhimu wa wakaguzi wa ndani na ni kitu gani wategemee kutokana na kazi zetu, kutoa elimu kwa wadau ni muhimu kwani kama hawatajua nini tunakifanya wanaweza wakawa na kigugumizi hata kuitaji huduma zetu,” alisema.

Related

ADVERTISEMENT
I am Krantz

I am Krantz

👉 FOUNDER & CEO of KONCEPT 👉Serial & Self-made Entrepreneur 👉Digital media consultant 👉Pr & media Guru/Awards winner Blogger 👉Startuper of the year 2016 by TOTAL 👉TOP 50 Most influential young Tanzania 2017 👉General Secretary at Tanzania Bloggers Network 👉 UPG Sustainability Leader in the Class of 2021 👉 ALUMNI The Tony Elumelu Foundation 👉Chairman YOUNG CEO CLUB Tanzania 🇹🇿 ‘ 😊 Marketer BY Education, Entrepreneur BY Profession & Blogger BY Passion ”😊

Related Posts

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI
HABARI

WATU WATANO WAFARIKI DUNIA KWA AJALI

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
NEYMAR KUONDOKA PSG
HABARI

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI JULAI 2, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 2, 2022
Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.
BIASHARA

Benki ya NBC yawapiga jeki wakulima kwa mikopo ya trekta.

by I am Krantz
Jul 2, 2022
AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNASA KWENYE NYAYA ZA UMEME
HABARI

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNASA KWENYE NYAYA ZA UMEME

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022
MTUMISHI WA TANESCO AKUTWA GUEST AMEFARIKI
HABARI

MTUMISHI WA TANESCO AKUTWA GUEST AMEFARIKI

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022
SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA JULAI 10, 2022
HABARI

SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA JULAI 10, 2022

by Shabani Rapwi
Jul 1, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s
KONCEPT TV

KONCEPT TWEETS

ADVERTISEMENT
May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr   Jun »
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In