ADVERTISEMENT
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 22, 2022
  • Login
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
ADVERTISEMENT
  • Home
  • HABARI
  • BURUDANI
  • BIASHARA
  • MICHEZO
  • MAGAZETI
  • MAGAZETI TANZANIA
  • KIMATAIFA
  • KONCEPT TV
No Result
View All Result
Mwanaharakati Mzalendo
No Result
View All Result
ADVERTISEMENT

TFS KANDA YA KUSINI KUTUMIA FILAMU YA ROYAL TOUR KUONGEZA WATALII KUSINI

Ally Hamis Zingizi by Ally Hamis Zingizi
May 15, 2022
in BIASHARA, HABARI
0
TFS KANDA YA KUSINI KUTUMIA FILAMU YA ROYAL TOUR KUONGEZA WATALII KUSINI

OLYMPUS DIGITAL CAMERA

0
SHARES
16
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT

RelatedPosts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

May 21, 2022

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

May 21, 2022

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

May 21, 2022
Load More

Na Muhidin Amri,
Masasi

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)Kanda ya Kusini, imejipanga kutumia Filamu ya Royal Tour  kuendeleza na kutangaza  vivutio mbalimbali   vinavyopatikana katika misitu inayosimamiwa na TFS kwa lengo ka kuvutia watalii na kuleta ajira kwa vijana wa kanda ya Kusini.

Hayo yamesemwa na Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) Bi Manyise Mpokigwa wakati akizungumzia  walivyojipanga  namna watakavyotumia  Filamu hiyo iliyozinduliwa wiki iliyopita na Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuongeza mapato ya nchi kupitia sekta ya misitu.

Alisema,Filamu ya Royal Tour imekuja kwa muda muafaka kwani TFS  itahakikisha inatumia fursa hiyo kutangaza vivutio na maliasili  zinazopatikana katika misitu inayosimamiwa na wakala Kanda ya Kusini kwa ajili ya kuvutia watalii wa ndani na nje ambao watalipa fedha kwa ajili ya kutembelea na kuangalia vivutio na maliasili zilizopo Kanda ya Kusini.

Aidha Kamishina Mpokigwa, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuitangaza Tanzania Kimataifa na imani ya Watanzania Filamu hiyo itaongeza watalii wengi na wawekezaji katika sekta mbalimbali ikiwamo ya utalii.

Mpokigwa ambaye ni Kamanda wa  wakala wa Huduma za misitu(TFS)Kanda ya Kusini alisema, Kanda ya Kusini kuna vivutio vingi,hata hivyo bado havijafahamika sana kutokana na changamoto mbalimbali.

Kwa mujibu wa Kamanda Mpokigwa,TFS kanda ya Kusini ina misitu mitatu ya asili mojawapo ni Msitu wa Londo uliopo katika mkoa wa Lindi,ambako kuna maeneo mazuri ya kupumzika na Mti maarufu wa Nyerere  wenye Historia kubwa.

Alisema,mti huo umekuwa kivutio kikubwa tangu ulipogundulika hasa baada ya Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania hayati Mwalimu Julius Nyerere alipofika na kuchuna gamba  la mti huo na kuondoka nalo.

Alisema,kuanzia wakati huo jamii na watu  kutoka maeneo mbalimbali wanaendelea kutumia magamba ya mti huo kama tiba na kufanya matambiko ambayo kwa imani zao wanafanikiwa kutokana na shida zinazowakabili.

“sasa mti huo kupitia wakala wa huduma za misitu umewekewa utaratibu maalum ambao kila  anayefika katika eneo hilo kwa ajili ya kuchuna magamba analazimika kuchangia kiasi kidogo cha fedha kwa ajili ya kuchangia mapato ya nchi yetu”alisema.

Mpokigwa,alitaja kivutio kingine ni msitu wa Pindilo uliopo katika wilaya ya Kilwa ambao ni  sehemu nzuri kutokana na uwepo uoto wa asili unoafaa kwa ajili ya watu kupumzika.

Pia alisema,katika msitu huo kuna mto Nyange na Bwawa lenye Wanyama aina ya Boko ambao ni walemavu wa ngozi(Albino)wenye uwezo wa kuongea na mtu na ni kivutia kikubwa kwa watu wanaofika katika msituo huo.

Kwa mujibu wa Mpokigwa,katika mkoa wa Ruvuma kuna safu za Milima  maarufu ya Matogoro Manispaa ya Songea wenye aina mbalimbali za ndege na ndiyo chanzo cha mto maarufu wa Ruvuma unaotenganisha kati ya Tanzania na Nchi jirani ya Msumbiji.

Alisema, katika milima  hiyo kuna maeneo mazuri yanayofaa kwa ajili ya kufanya mikutano mbalimbali  kwa kuwa ni sehemu nzuri na tulivu ikilinganisha na maeneo mengine ya  katika mkoa huo.

Alitaja Msitu  mwingine ni Mwombesi(Mwombesi Nature Reserve) unaopatikana katika wilaya ya Tunduru wenye Wanyama wengi mchanganyiko kama vile Tembo,Nyati, Swala,Paka pori, Fisi,Nyoka na maporomokoya asili.

Alisema,Msitu wa Mwombesi  ni hifadhi iliyo mpakani mwa Tanzania na nchi jirani ya Msumbuji kupitia Mto Ruvuma na mwaka 2021 watalii zaidi ya 50 kutoka Mataifa mbalimbali walitembelea katika msituo huo na kufanya mkutano.

Alisema,kwa sasa kazi kubwa inayofanyika ni kuboresha mazingira hasa ya miundombinu ya barabara ili Watanzania na watalii kutoka nje ya nchi waweze kufika katika msituo huo.
MWISHO.

ADVERTISEMENT

Related

ADVERTISEMENT
Ally Hamis Zingizi

Ally Hamis Zingizi

Related Posts

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 6, 2022 / BEI YA PETROLI KILIO KILA KONA / WABUNGE WACHARUKA KUPAA BEI YA MAFUTA / MAKAMBA AMALIZA UTATA BEI YA MAFUTA
HABARI

BUNDI ATUA NCCR – MAGEUZI / TUNDU LISSU, LEMA WACHOKA MAISHA YA UGHAIBUNI / MAGAZETI YA LEO MEI 22, 2022

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
TUMEUMIZWA NA MATOKEO YA JANA – AHMED ALLY
HABARI

AFRIKA NZIMA ITAKAA KWENYE TV KUANGALIA SIMBA IKICHEZA FAINALI MICHUANO YA AFRIKA – AHMED ALLY

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA
HABARI

MADHARA YA KUPAKA MATE UKENI WAKATI WA TENDO LA NDOA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI
HABARI

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA NCCR-MAGEUZI

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA
HABARI

ALIYOFANYA MIQUISSON, SAKHO AMESHINDWA KUFANYA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022
BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA
HABARI

BOCCO ANASTAILI HESHIMA KATIKA SOKA LA TANZANIA

by Shabani Rapwi
May 21, 2022

KRANTZ MWANTEPELE (FOUNDER & CEO)

ADVERTISEMENT

KONCEPT TV

https://www.youtube.com/watch?v=0HP0mB_rtIU&t=7s

KONCEPT TV
ADVERTISEMENT
Mwanaharakati Mzalendo

Mwanaharakati Mzalendo ni mtandao namba moja kwa habari makini kutoka pande zote za dunia kuhusiana na Michezo, Siasa, Afya, Elimu, Mahusiano, Vituko, n.k

Wasiliana nasi kwa Email;krantzcharles@gmail.com
SIMU; 0658123310

Follow Us

May 2022
M T W T F S S
 1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031  
« Apr    
Currently Playing
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Biashara
  • Afya
  • Kisamkasa
  • Magazeti
  • Makala
  • Michezo
  • Teknolojia
  • Koncept Tv

All rights reserved © 2020 Mwanaharakati Mzalendo - Powered by Koncept.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In